Nchi hii haitaendelea kamwe, unless CCM waondoke madarakani

The Prophet

JF-Expert Member
Mar 17, 2011
682
94
nimekuwa nikifuatilia kwa karibu taarifa kuwa wahisani wamepanda dau kwenye bajeti ya nchi yetu kutoka Bolioni 814 mwaka jana mpaka Bilioni 840 mwaka huu.

kinachonishangaza hapa ni kuona vyombo vya habari na baadhi ya wanasiasa kuliona kama hili ni jambo la kujivunia na kupewa headlines. kwamba wahisani 'wanaridhishwa na utendaji wa serekali'. tunaona matamshi haya kama ni fahari ya nchi na uhuru wetu. kwamba Canada, na nchi za Scandnavia na walafi wengine wa madini na misitu yetu kutupatia msaada wa pesa, kwetu ni ufahari wa kutangazwa kila mahali.

Tunafurahia misaada. Hatujiulizi kama wananchi wetu nao wanaridhika na utendaji wa serekali yetu! Wananchi ni mafukara, hawana elimu, hawana afya bora, hawana mambo ya msingi yanayowa-define wao kama wanadamu. Hatujiulizi na wala hatuyaoni haya. tunafurahia na kujivunia wahisani kutuongezea pesa za omba-omba.

Ngoja nipige Serengeti yangu baridi, labda akili yangu ita-relax.
 
unajua mzee wa ban muda mwingi hata huku kwetu huwa tunajiulizaga haya maisha wanayosema yamepanda I mean uchumi umeimarika ni kushuka kwa thamani ya shilingi au ni ktu kingine???

Anyhow umasikini wetu huwa tunajitakiaga wenyewe maana utakuta jitu linanguvu lakini linauza karanga kwenye vituo vya basi hiyo moja

Hapo halijui haki yake, halijui kesho litaishije na nyumbani lina familia inamngoja, nadiriki kusema na hata raisi wa burunfi alisema watanzania ni wajinga tea sanaaaa maana kama wote tungeamka kusingekuwa na huu uchoko unaoendelea sas hivi mtu kujilimbikizia mali
 
Back
Top Bottom