kilimasera
JF-Expert Member
- Dec 2, 2009
- 3,068
- 268
CHAMA cha NCCR Mageuzi kimeiomba Serikali kuwafutia mashitaka viongozi na wafuasi wote wa Chadema waliokamatwa wakati wa maandamano yaliyozimwa kwa risasi, mabomu na virugu juzi mjini Arusha.
Karibu viongozi wote wa juu ndani ya Chadema, wakiongozwa na Mwenyekiti wake, Freeman Mbowe na Katibu Mkuu, Willibrod Slaa, walikuwa miongoni mwa waliokamatwa, kuswekwa rumande na hatimaye juzi kufikishwa mahakamani.
Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Kaimu Katibu Mkuu wa chama hicho, Faustine Sungura alisema kuwa, kutokana na madai ya Chadema kuwa ya msingi, NCCR imemtaka Waziri Mkuu, Mizengo Pinda kuhakikisha ndani ya siku tatu anachukua hatua za kumaliza mgogoro uliosababisha maandamano hayo.
Ikiwa hatofanya hivyo tumepanga kufikisha hoja binafsi katika kikao cha Bunge kitakachoanza Februari 8, mwaka huu ambapo kwa kupitia muwakilishi wetu tutaiwasilisha hoja hiyo siku tatu baada ya kikao hicho kuanza ya kumtaka awajibishwe kwani matukio hayo yamechafua taswira ya taifa alisema Sungura.
Katika mkutano na wanahabari, Sungura amedai kuwa, Chadema ilikuwa na sababu za msingi za kulalamikia uchaguzi wa Meya wa Jiji la Arusha kwa kile alichodai ukiukwaji wa kanuni ikiwa pamoja na kuruhusu madiwani kutoka nje ya Jiji hilo.
Sungura alitumia nafasi hiyo kulaani matumizi mabaya ya madaraka yaliyofanywa na Jeshi la Polisi yaliyosababisha uvunjifu wa amani na haki za msingi za binadamu na hivyo kuitaka Serikali kuwalipa fidia wananchi wote walioathirika na uzembe huo wa polisi.
Haiingii akilini na hasa kwa watu makini, polisi kuzuia maandamano kwa hoja hafifu kuwa hakuna askari wa kulinda maandamano, lakini polisi hao hao wakawa na askari wa ziada wakatumia risasi za moto, mabomu na marungu kuzuia maandamano ni vizuri nguvu hii ingetumika kulinda maandamano hayo alisema Sungura.
Alisema kwa matumizi ya nguvu na mabavu hayajawahi kuleta suluhu katika migogoro ya kisiasa na kulitaka Jeshi la Polisi kuacha mara moja kutumika kulinda uharamia na ujambazi wa kisiasa unaofanywa na baadhi ya viongozi wa CCM.
Karibu viongozi wote wa juu ndani ya Chadema, wakiongozwa na Mwenyekiti wake, Freeman Mbowe na Katibu Mkuu, Willibrod Slaa, walikuwa miongoni mwa waliokamatwa, kuswekwa rumande na hatimaye juzi kufikishwa mahakamani.
Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Kaimu Katibu Mkuu wa chama hicho, Faustine Sungura alisema kuwa, kutokana na madai ya Chadema kuwa ya msingi, NCCR imemtaka Waziri Mkuu, Mizengo Pinda kuhakikisha ndani ya siku tatu anachukua hatua za kumaliza mgogoro uliosababisha maandamano hayo.
Ikiwa hatofanya hivyo tumepanga kufikisha hoja binafsi katika kikao cha Bunge kitakachoanza Februari 8, mwaka huu ambapo kwa kupitia muwakilishi wetu tutaiwasilisha hoja hiyo siku tatu baada ya kikao hicho kuanza ya kumtaka awajibishwe kwani matukio hayo yamechafua taswira ya taifa alisema Sungura.
Katika mkutano na wanahabari, Sungura amedai kuwa, Chadema ilikuwa na sababu za msingi za kulalamikia uchaguzi wa Meya wa Jiji la Arusha kwa kile alichodai ukiukwaji wa kanuni ikiwa pamoja na kuruhusu madiwani kutoka nje ya Jiji hilo.
Sungura alitumia nafasi hiyo kulaani matumizi mabaya ya madaraka yaliyofanywa na Jeshi la Polisi yaliyosababisha uvunjifu wa amani na haki za msingi za binadamu na hivyo kuitaka Serikali kuwalipa fidia wananchi wote walioathirika na uzembe huo wa polisi.
Haiingii akilini na hasa kwa watu makini, polisi kuzuia maandamano kwa hoja hafifu kuwa hakuna askari wa kulinda maandamano, lakini polisi hao hao wakawa na askari wa ziada wakatumia risasi za moto, mabomu na marungu kuzuia maandamano ni vizuri nguvu hii ingetumika kulinda maandamano hayo alisema Sungura.
Alisema kwa matumizi ya nguvu na mabavu hayajawahi kuleta suluhu katika migogoro ya kisiasa na kulitaka Jeshi la Polisi kuacha mara moja kutumika kulinda uharamia na ujambazi wa kisiasa unaofanywa na baadhi ya viongozi wa CCM.