BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,790
- 288,005
Hongera NCCR! Hakuna ubaya wowote kuchukua points kutoka hapa ukumbini na kuzifanyia kazi
NCCR yahoji hotuba za mwezi za JK
na Mobini Sarya
Tanzania Daima~Sauti ya Watu
CHAMA cha NCCR-Mageuzi kimemtaka Rais Jakaya Kikwete kutoa tamko la kupanda kwa bei ya mafuta akirejea ahadi zake za maisha bora kwa kila Mtanzania aliyowaahidi Watanzania.
Aidha kimehoji sababu ambazo zimemfanya Rais Kikwete aache kuhutubia taifa kupitia vyombo vya habari kama ilivyokuwa kawaida yake kila mwezi ambapo kwa miezi miwili sasa, hajalihutubia taifa.
Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, Mkuu wa Idara ya Itikadi na Mafunzo, George Kahangwa, alisema chama hicho kinawapa pole Watanzania kwa ugumu wa maisha unaosababishwa na kupanda bei ya mafuta.
Alisema ni vema Rais Kikwete akatoa tamko la ufumbuzi wa tatizo hilo ili wananchi waweze kufikia ahadi iliyotolewa ya kupatiwa maisha bora.
Kahangwa alibainisha kuwa, malumbano yanayoendelea hivi sasa kuhusu sababu za kupanda kwa bei za mafuta, kunawachanganya wananchi, hivyo ni vema Rais Kikwete akaliweka wazi.
Alisena watu wengine wanadai hali hiyo inatokana na kushamiri kwa migogoro katika nchi zinazozalisha mafuta, hivyo kutokuwa na uwezo wa kuzalisha kwa kiwango kinachohitajika.
Aidha NCCR-Mageuzi imepinga vikali hatua ya serikali kubadili matumizi ya ardhi yenye rutuba kwa chakula na kuwapatia wawekezaji wapande mimea ya kuzalisha nishati mbadala ya dizeli.
Serikali kupitia ubinafsishaji wake usio na hekima imekwishakujiingiza katika uuzaji wa ardhi ya rutuba ili wawekezaji waendeshe kilimo cha miwa na mibono kwa ajili ya nishati hatua za namna hii zitasababisha taifa kuingia kwenye baa la njaa, lilisema tamko la chama hicho.
Katika tamko hilo wametolea mfano mwekezaji aliyeuziwa bonde la Usangu wilayani mbarari ili aoteshe mibono baadala ya mpunga uliokuwa ukioteshwa katika bonde hilo ambapo asilimia 60 ya mchele unaouzwa nchini ulikuwa unatoka huko.
NCCR yahoji hotuba za mwezi za JK
na Mobini Sarya
Tanzania Daima~Sauti ya Watu
CHAMA cha NCCR-Mageuzi kimemtaka Rais Jakaya Kikwete kutoa tamko la kupanda kwa bei ya mafuta akirejea ahadi zake za maisha bora kwa kila Mtanzania aliyowaahidi Watanzania.
Aidha kimehoji sababu ambazo zimemfanya Rais Kikwete aache kuhutubia taifa kupitia vyombo vya habari kama ilivyokuwa kawaida yake kila mwezi ambapo kwa miezi miwili sasa, hajalihutubia taifa.
Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, Mkuu wa Idara ya Itikadi na Mafunzo, George Kahangwa, alisema chama hicho kinawapa pole Watanzania kwa ugumu wa maisha unaosababishwa na kupanda bei ya mafuta.
Alisema ni vema Rais Kikwete akatoa tamko la ufumbuzi wa tatizo hilo ili wananchi waweze kufikia ahadi iliyotolewa ya kupatiwa maisha bora.
Kahangwa alibainisha kuwa, malumbano yanayoendelea hivi sasa kuhusu sababu za kupanda kwa bei za mafuta, kunawachanganya wananchi, hivyo ni vema Rais Kikwete akaliweka wazi.
Alisena watu wengine wanadai hali hiyo inatokana na kushamiri kwa migogoro katika nchi zinazozalisha mafuta, hivyo kutokuwa na uwezo wa kuzalisha kwa kiwango kinachohitajika.
Aidha NCCR-Mageuzi imepinga vikali hatua ya serikali kubadili matumizi ya ardhi yenye rutuba kwa chakula na kuwapatia wawekezaji wapande mimea ya kuzalisha nishati mbadala ya dizeli.
Serikali kupitia ubinafsishaji wake usio na hekima imekwishakujiingiza katika uuzaji wa ardhi ya rutuba ili wawekezaji waendeshe kilimo cha miwa na mibono kwa ajili ya nishati hatua za namna hii zitasababisha taifa kuingia kwenye baa la njaa, lilisema tamko la chama hicho.
Katika tamko hilo wametolea mfano mwekezaji aliyeuziwa bonde la Usangu wilayani mbarari ili aoteshe mibono baadala ya mpunga uliokuwa ukioteshwa katika bonde hilo ambapo asilimia 60 ya mchele unaouzwa nchini ulikuwa unatoka huko.