Elections 2010 NCCR Mageuzi wameniduwaza...

Mkuu Mtanzania,

Pamoja na factors nyingine, uongozi wa CCM mkoa wa Kigoma una matatizo. Kwenye baadhi ya majimbo kulikuwa na madai kwamba fedha nyingi zilitumika kwenye kura za maoni na hivyo kuna wagombea ambao hawana sifa walishinda. Nadhani kuna mgombea mmoja aliandikwa sana magazetini kwamba ana kashfa za ujambazi, mambo ya albino na ufisadi pia. Lakini mgombea huyo alikuwa kipenzi cha Mwenyekiti wa Mkoa. Kwenye jimbo hilo wananchi walionyesha hasira za wazi kwa kumpa mpinzani 97% ya kura, kitu ambacho ni nadra sana kwa mgombea wa CCM .... watanzania si mabwege tena.

Kama unakumbuka Katibu Mkuu wa mkoa alipewa barua ya uhamisho saa sita usiku, siku ambayo JK alienda kupiga kampeni mkoani Kigoma. Mama wa watu alitakiwa akaripoti Makao Makuu Dodoma. Sasa hivi huyo Mama atakuwa anashangilia tu maana alikuwa mstari wa mbele kuwapinga baadhi ya wagombea Ubunge na Udiwani kwenye majimbo ya mkoa na alikuwa na valid reasons ambazo Mwenyekiti wa mkoa hakuziona.

Tatizo la mafisadi wa CCM wanaamini kwamba fedha inaweza kununua kura, which is wrong maana watu wameamka na wana uelewa wa kutosha. Mgombea yeyote akienda kujikita huko vijijini kwa miaka 2 anawasomesha wapiga kura, ukija uchaguzi lazima wampe kura hata kama kuna mtu ataenda kumwaga fedha, khanga, fulana na kofia.

Mkuu Keil,

Lakini mbona hiyo haikutokea sehemu mbalimbali? Kwa mfano najua yule jamaa wa CHADEMA kule Mbeya vijijini ni mzuri sana na ni kiongozi wa CHADEMA wa mkoa na pia muda mwingi kajichimbia kule Mbeya lakini bado hakuweza kushinda. Kuna majimbo mengine pia ambayo kuna vijana ambao walipiga kampeni za nguvu lakini hawakufanikiwa.

Hii ya Kigoma naona kama ni pekee kwa siasa za Tanzania mwaka huu. Huenda kujijenga kwa hao vijana wakiwa ndani ya CHADEMA kumewasaidia maana tayari walikuwa wanajulikana lakini pia kuna hao wengine wawili ambao nao wameshinda.

Kama kuna mtu anajua matokeo ya udiwani kwenye hizo wilaya ingesaidia.

Kigoma Mjini CHADEMA alikuwa anagombea bwana mdogo mmoja ambaye tumesoma naye nchi moja. Nilisikitika kuona alishindwa dakika za mwisho tena kwa kura chache sana zenye utata. Nafikiri angelikuwa na muda wa kutosha wa kujijenga kule kama wenzake huenda angeshinda kwa kura nyingi.
 
Mkuu Shalom,

Sawa unaweza kwenda kufanya utafiti wako lakini majimbo kama Kyela yako mengi tu Tanzania ambako wananchi waliamua kuwabakiza walioko madarakani.

I hope uwezo wako ni zaidi ya vijembe vya JF. Wengine tulijitolea kugombea, tumeshindwa na tunasonga mbele na maisha, nafikiri ndio demokrasi tunayohubiri hapa JF.

Kama kufanya hivyo ni tatizo kwako, well, that is and will not be my problem! Uzuri wake, tulioshindwa mwaka huu tuko wengi tu ikiwa ni pamoja na hao unao waabudu!

Poti,

Kunatofauti ya kushindwa kwa kura au kushindwa kwa kuiba kura. Wewe poti nakupa pole kwa sababu walichakachua kura zako ila hawa ninao waabudu wameshindwa kwa kura. Sitasahau pale mgombea mmoja alipomaliza kuongea na watu wakaanza kutawanyika na kuwaacha wangombea wengine wakishangaa du hii ndiyo demokrasia.

Naona watu wamekujibu la NCCR lakini na mimi bado sijapata majibu ni kwa nini Kyela walikuwa wanampenda dr vile na kuwafanya muonekane vile wanajamii wenzetu!
 
Ukweli ni kwamba Samweli Ruhuza tajiri mkubwa na katibu wa NCCR-Mageuzi ni mwenyeji wa Kigoma. Huyu jamaa ameishi Kigoma muda mrefu na anafahamu watu gani wangefaa na mahali gani. Ukiondoa David Kafulila wengine wote wametokana haswa na juhudi za Samweli Ruhuza wala sio kina Mbatia.
 
Poti,

Kunatofauti ya kushindwa kwa kura au kushindwa kwa kuiba kura. Wewe poti nakupa pole kwa sababu walichakachua kura zako ila hawa ninao waabudu wameshindwa kwa kura. Sitasahau pale mgombea mmoja alipomaliza kuongea na watu wakaanza kutawanyika na kuwaacha wangombea wengine wakishangaa du hii ndiyo demokrasia.

Naona watu wamekujibu la NCCR lakini na mimi bado sijapata majibu ni kwa nini Kyela walikuwa wanampenda dr vile na kuwafanya muonekane vile wanajamii wenzetu!

Mkuu Shalom,
Kule kwetu Kyela kuna matatizo makubwa mno ya umaskini na ujinga. Badala ya kushambulia kila post yangu hapa JF, utakuwa umetimiza wajibu wako kama mwana Kyela na Mtanzania ukitumia hata dakika chache kuangalia namna ya kupambana na hayo matatizo.

Nani anapendwa zaidi ya mwingine haitakusaidia maana siasa ndivyo zilivyo miaka yote. Si umeona kuna wagombea wamejaza watu mpaka pa kukaa pakakosekana na bado kura hazikutosha? Kura kama 1600 nilizopata tena bila kuchakachua au kumwaga makadi feki zinanitosha na ninasonga mbele na life yangu. Kama unaona ni chache basi kajaribu na wewe tuone.

Tuache kupotezeana muda hapa JF bila sababu za msingi. Kuna mambo mengi ya kufanya zaidi ya politics.
 
K. amanda uliyotangulia mwanzoni, kweli unafahamu kilichojiri Kigoma...kama lilivyojina langu Zitto anajifanya ndio kingmaker wa Kigoma na alikisaliti chama na kuwapigia kampeni hao mentee wake wazi wazi. Alimrubuni Mzee wa watu Ntagazwa kuhamia chadema na amekuwa akimpiga chenga kwenda kufungua kampeni zake. Hata Dr. Slaa alipoenda hakwenda hata kuzungumza nae na Dr. Slaa alimwambia arudi kutibu majeraha na kuona kwanini Ntagazwa hakubaliki na Zitto wala hakurudi. Yeye alikuwa tayari kwenda Mtwara kupigia wanachadema wengine lakini mkoani kwake ambako amwekea mapandikizi wake hakukanyaga mguu..sitoshangaa akikosa kuwa Kiongozi wa Upinzani bungeni na masuala mengine akaanzisha chama chake au akaenda huko NCCR...what goes around comes around...
 
Kamanda uliyotangulia mwanzoni, kweli unafahamu kilichojiri Kigoma...kama lilivyojina langu Zitto anajifanya ndio kingmaker wa Kigoma na alikisaliti chama na kuwapigia kampeni hao mentee wake wazi wazi. Alimrubuni Mzee wa watu Ntagazwa kuhamia chadema na amekuwa akimpiga chenga kwenda kufungua kampeni zake. Hata Dr. Slaa alipoenda hakwenda hata kuzungumza nae na Dr. Slaa alimwambia arudi kutibu majeraha na kuona kwanini Ntagazwa hakubaliki na Zitto wala hakurudi. Yeye alikuwa tayari kwenda Mtwara kupigia wanachadema wengine lakini mkoani kwake ambako amwekea mapandikizi wake hakukanyaga mguu..sitoshangaa akikosa kuwa Kiongozi wa Upinzani bungeni na masuala mengine akaanzisha chama chake au akaenda huko NCCR...what goes around comes around...

Well said, na hao wote sitashangaa kusikia Zitto kabwe ni mentor wao au aliwapa msaada mkubwa. Chadema inapaswa kutulia na kushikamana kama ilivyokuwa wakati wa kampeni. miaka mitano ni mingi ccm hawatanyamaza watajitahidi kuisambaratisha. maumizi ya kupoteza jimbo la kawe ambako wakuu wote wa cccm, serikali, mabalozi, matajiri wakubwa na usalama wa taifa wanaishi si madogo. hawawezi kutulia, watajitahidi kuivuga CHADEMA ili kulipa kisasi.
 
Back
Top Bottom