nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,862
- 5,797
KATIKA historia ya uchaguzi wa vyama vingi mkoani Kigoma, Oktoba mwaka jana NCCR-Mageuzi imeandika historia kwa kutumia mtaji wa wanachama wa Chama cha
Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kuibuka washindi.
Duru za kisiasa mkoani humo zimethibitisha kuwa kati ya wabunge wanne wa NCCR-Mageuzi, wawili walikuwa viongozi na wanachama wa Chadema. Chadema ilipoteza viongozi hao na
wanachama wake kutokana na sababu nyingi zikiwamo za kusimamisha baadhi ya wagombea
walioenguliwa au kuachwa na chama tawala au na vyama vingine.
Upande wa pili wa kushindwa kwa chama hicho, kunatokana na kunyemelewa na mdudu wa migogoro ndani ya chama, migogoro ambayo ilisababisha baadhi ya viongozi wa chama
hicho kususia wagombea na kushindwa kuwanadi.
Kutokana na mtafaruku huo ndani ya Chama, baadhi ya vijana waliokuwa wamejipanga kuingia bungeni, waliamua kuihama Chadema na kuingia kugombea ubunge kwa tiketi ya NCCR
Mageuzi.
Wabunge wa NCCR- Mageuzi ni Felix Mkosamali wa Muhambwe, David Kafulila wa Uvinza, Mosses Machali wa Kasulu Mjini na Zeitun Buyogela wa Kasulu Vijijini. Si kwamba NCCR-Mageuzi haikuwapo mkoani humo; ilikuwamo lakini haikuwa na wanachama wengi hivyo wa kuweza kukipa ushindi mkubwa kiasi kile.
Chama chenye wanachama wengi mkoani humo ni CCM ikifuatiwa na Chadema, ndipo kidogo kinakuja NCCR, Chama cha Wananchi (Cuf) na Sauti ya Umma (Sau) yenye wanachama
wachache kabisa.
Hivyo ushindi wa NCCR Mageuzi katika majimbo hayo manne mkoani Kigoma, mawili yakiwa
Kasulu, moja Kigoma na lingine Kibondo, ni mtaji wa wanachama wa Chadema. Ushindi huo ulitokana na migawanyiko ndani ya Chadema iliyoinufaisha NCCR nyakati za lala salama.
Ushindi huo ni sawa na mechi ya mpira, mshindi wa kweli ni yule anayeibuka na magoli mengi zaidi dakika ya tisini ikishafika. Unaweza kudhani umeshinda kabla mechi haijaisha, dakika za
mwisho mambo yakageuka.
Ndicho kilichowakumba Chadema. Chama kiliwaandaa wanachama kisaikolojia, lakini kutokana na mgawanyiko kuwasimamisha wagombea waliosuswa wasiouzika, wapigakura wakawachapa bakora kwa kuwachagua chipukizi wa NCCR-Mageuzi.
Miongoni mwao ni Mkosamali ambaye ni mbunge kijana zaidi kuliko wabunge wote nchini.
Mmoja wa wananchi wa Kigoma, Hamad Ahamed anasema kwamba pamoja na kura zao kuwapa wagombea wa NCCR-Mageuzi bado wao ni mtaji wa kambi ya mageuzi, wao wanaipinga CCM wala si chama kingine cha upinzani.
Hivyo mwaka mwingine ikitokea kuwa NCCR- Mageuzi imewachefua dakika za mwisho watakipigia kura chama kingine kiwe Cuf au Sau, ambavyo ndivyo vyenye matawi mkoani
humo.
Sau kinawika Ujiji na vijiji vinavyozunguka makao makuu ya mkoa, Cuf wapo Uvinza, Nguruka na maeneo mengine ya Kigoma Vijijini. Mwenyekiti wa NCCR, James Mbatia kwa kutambua fadhila za watu wa mkoa huo kumpa wabunge wanne, ameamua kuwatembelea na kuwashukuru wapiga kura mkoani humo.
Katika ziara yake hiyo, Mbatia aliwapa asante wabunge wake na watu waliokipigia kura chama chake na kuibuka na ushindi katika majimbo manne. Nzuri zaidi katika majimbo hayo manne ni kwamba mmoja wa wabunge hao ni mwanamke ambaye kutokana na uhodari wake, amechaguliwa kuwa mmoja wa makamishna saba wa kumshauri Spika Anne Makinda.
Kwa nyakati tofauti, Machali na Zaituni waliahidi kuwa chachu ya maendeleo na kukiendeleza chama mkoani Kigoma. Pamoja na kukidumisha chama, watakuwa mstari wa mbele kuhakikisha wanatetea maslahi ya wanachama na wananchi kwa ujumla, ili kuhakikisha haki zao, mfano za kuporwa ardhi zinarudishwa.
Kitu cha ajabu si wanachama wa Chadema mkoani humo tu waliokiacha chama solemba karibu na wakati wa uchaguzi, hata wanachama wa CCM walikipiga bakora chama chao kwa mtindo huo huo baada ya kusimamisha wagombea wasiouzika.
Mtindo huo wa watu wa Kigoma, umeibuka pia katika sehemu nyingine nchini, ambapo wanachama wa vyama mbalimbali bila kujali itikadi zao waliamua kuchagua wagombea wa
chama chochote walioonekana kuuzika.
Uchaguzi wa mwaka jana, ulikuwa na msukumo wa aina yake, kwamba katika maeneo ambayo watu waliokuwa wamechoshwa na mbunge au wabunge waliotangulia, waliamua kuziacha pembeni itikadi za vyama na kumchagua mtu waliyeamini atatetea maslahi yao badala ya kupoteza muda bungeni.
Mkoa wa Kigoma umeweka historia kutokana na uamuzi wa dakika za mwisho dhidi ya vyama ambavyo vilikuwa na sera, wafuasi na wanachama wengi.
Vimejikuta vikipoteza majimbo kutokana na uchaguzi uliofuata zaidi hisia badala ya si uwezo au kukubalika kwa mgombea. Mfano hai ni katika jimbo la Muhambwe ambalo CCM ilimsimamisha Jamal Tamimu, Chadema wakamsimamisha Arcado Ntagazwa baada ya kujiengua CCM ambako alihudumu kwa miaka 25 na NCCR ikamsimamisha Mkosamali.
Chadema ilishindwa kusoma alama za nyakati, kama ambavyo CCM haikubaini kwamba imechanga karata vibaya kwa kudharau nafasi ya wanachama katika uchaguzi.
Kizazi kipya vijana, ambacho ndicho wapiga kura wengi kinataka mageuzi; kinaona wazee hawawezi kuleta mageuzi, na kama chama kimoja kinasimamisha wazee basi ni rahisi chama hicho kupoteza jimbo hilo, kutegemeana na mhusika mwenyewe lakini.
Ndicho kilichotokea katika jimbo hilo, wanachama wa CCM ambao wamekerwa na mfumo wa
umangimeza, waliamua kuvunja kanuni na miiko ya chama, wakampigia kura Mkosamali, wakijikita katika misingi ya kuwa hiyo ndiyo damu chama itakayoleta mageuzi ya kweli jimboni humo.
Wanachama wa Chadema ambao hawakupoteza muda kumpa ulaji mgombea wao, alihamishia
nguvu zao kumuunga mkono Mkosamali, akashinda kwa ushindi wa kishindo. Katika majimbo mengine vile vile, wagombea waliokuwa wamepitwa na wakati, haikuwa rahisi kupenya
kwenye tundu la sindano, hivyo wakaambulia kugalagazwa.
Ushindi wa Kafulila, Machali na Zeitun pamoja na Mkosamali, umeipa uhai NCCRMageuzi
mkoani Kigoma ambayo ilikuwa inachungulia kaburi kwa idadi ndogo ya wanachama.
Ndiyo maana kutokana na ushindi huo, NCCR imeamka usingizini kwa nguvu mpya ya kushika majimbo mengi mkoani humo na kuanzia hapo cheche zimeanza kusambaa katika majimbo mengine ndani na nje ya mkoa huo.
Siasa ni sawa na kuchanga karata, unaweza kuwa bingwa wa kuandaa karata, lakini mchangaji mzuri akishika, akakufunga bao, hilo ndilo lililowakumba Chadema kupoteza vijana wake dakika za mwisho.
Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kuibuka washindi.
Duru za kisiasa mkoani humo zimethibitisha kuwa kati ya wabunge wanne wa NCCR-Mageuzi, wawili walikuwa viongozi na wanachama wa Chadema. Chadema ilipoteza viongozi hao na
wanachama wake kutokana na sababu nyingi zikiwamo za kusimamisha baadhi ya wagombea
walioenguliwa au kuachwa na chama tawala au na vyama vingine.
Upande wa pili wa kushindwa kwa chama hicho, kunatokana na kunyemelewa na mdudu wa migogoro ndani ya chama, migogoro ambayo ilisababisha baadhi ya viongozi wa chama
hicho kususia wagombea na kushindwa kuwanadi.
Kutokana na mtafaruku huo ndani ya Chama, baadhi ya vijana waliokuwa wamejipanga kuingia bungeni, waliamua kuihama Chadema na kuingia kugombea ubunge kwa tiketi ya NCCR
Mageuzi.
Wabunge wa NCCR- Mageuzi ni Felix Mkosamali wa Muhambwe, David Kafulila wa Uvinza, Mosses Machali wa Kasulu Mjini na Zeitun Buyogela wa Kasulu Vijijini. Si kwamba NCCR-Mageuzi haikuwapo mkoani humo; ilikuwamo lakini haikuwa na wanachama wengi hivyo wa kuweza kukipa ushindi mkubwa kiasi kile.
Chama chenye wanachama wengi mkoani humo ni CCM ikifuatiwa na Chadema, ndipo kidogo kinakuja NCCR, Chama cha Wananchi (Cuf) na Sauti ya Umma (Sau) yenye wanachama
wachache kabisa.
Hivyo ushindi wa NCCR Mageuzi katika majimbo hayo manne mkoani Kigoma, mawili yakiwa
Kasulu, moja Kigoma na lingine Kibondo, ni mtaji wa wanachama wa Chadema. Ushindi huo ulitokana na migawanyiko ndani ya Chadema iliyoinufaisha NCCR nyakati za lala salama.
Ushindi huo ni sawa na mechi ya mpira, mshindi wa kweli ni yule anayeibuka na magoli mengi zaidi dakika ya tisini ikishafika. Unaweza kudhani umeshinda kabla mechi haijaisha, dakika za
mwisho mambo yakageuka.
Ndicho kilichowakumba Chadema. Chama kiliwaandaa wanachama kisaikolojia, lakini kutokana na mgawanyiko kuwasimamisha wagombea waliosuswa wasiouzika, wapigakura wakawachapa bakora kwa kuwachagua chipukizi wa NCCR-Mageuzi.
Miongoni mwao ni Mkosamali ambaye ni mbunge kijana zaidi kuliko wabunge wote nchini.
Mmoja wa wananchi wa Kigoma, Hamad Ahamed anasema kwamba pamoja na kura zao kuwapa wagombea wa NCCR-Mageuzi bado wao ni mtaji wa kambi ya mageuzi, wao wanaipinga CCM wala si chama kingine cha upinzani.
Hivyo mwaka mwingine ikitokea kuwa NCCR- Mageuzi imewachefua dakika za mwisho watakipigia kura chama kingine kiwe Cuf au Sau, ambavyo ndivyo vyenye matawi mkoani
humo.
Sau kinawika Ujiji na vijiji vinavyozunguka makao makuu ya mkoa, Cuf wapo Uvinza, Nguruka na maeneo mengine ya Kigoma Vijijini. Mwenyekiti wa NCCR, James Mbatia kwa kutambua fadhila za watu wa mkoa huo kumpa wabunge wanne, ameamua kuwatembelea na kuwashukuru wapiga kura mkoani humo.
Katika ziara yake hiyo, Mbatia aliwapa asante wabunge wake na watu waliokipigia kura chama chake na kuibuka na ushindi katika majimbo manne. Nzuri zaidi katika majimbo hayo manne ni kwamba mmoja wa wabunge hao ni mwanamke ambaye kutokana na uhodari wake, amechaguliwa kuwa mmoja wa makamishna saba wa kumshauri Spika Anne Makinda.
Kwa nyakati tofauti, Machali na Zaituni waliahidi kuwa chachu ya maendeleo na kukiendeleza chama mkoani Kigoma. Pamoja na kukidumisha chama, watakuwa mstari wa mbele kuhakikisha wanatetea maslahi ya wanachama na wananchi kwa ujumla, ili kuhakikisha haki zao, mfano za kuporwa ardhi zinarudishwa.
Kitu cha ajabu si wanachama wa Chadema mkoani humo tu waliokiacha chama solemba karibu na wakati wa uchaguzi, hata wanachama wa CCM walikipiga bakora chama chao kwa mtindo huo huo baada ya kusimamisha wagombea wasiouzika.
Mtindo huo wa watu wa Kigoma, umeibuka pia katika sehemu nyingine nchini, ambapo wanachama wa vyama mbalimbali bila kujali itikadi zao waliamua kuchagua wagombea wa
chama chochote walioonekana kuuzika.
Uchaguzi wa mwaka jana, ulikuwa na msukumo wa aina yake, kwamba katika maeneo ambayo watu waliokuwa wamechoshwa na mbunge au wabunge waliotangulia, waliamua kuziacha pembeni itikadi za vyama na kumchagua mtu waliyeamini atatetea maslahi yao badala ya kupoteza muda bungeni.
Mkoa wa Kigoma umeweka historia kutokana na uamuzi wa dakika za mwisho dhidi ya vyama ambavyo vilikuwa na sera, wafuasi na wanachama wengi.
Vimejikuta vikipoteza majimbo kutokana na uchaguzi uliofuata zaidi hisia badala ya si uwezo au kukubalika kwa mgombea. Mfano hai ni katika jimbo la Muhambwe ambalo CCM ilimsimamisha Jamal Tamimu, Chadema wakamsimamisha Arcado Ntagazwa baada ya kujiengua CCM ambako alihudumu kwa miaka 25 na NCCR ikamsimamisha Mkosamali.
Chadema ilishindwa kusoma alama za nyakati, kama ambavyo CCM haikubaini kwamba imechanga karata vibaya kwa kudharau nafasi ya wanachama katika uchaguzi.
Kizazi kipya vijana, ambacho ndicho wapiga kura wengi kinataka mageuzi; kinaona wazee hawawezi kuleta mageuzi, na kama chama kimoja kinasimamisha wazee basi ni rahisi chama hicho kupoteza jimbo hilo, kutegemeana na mhusika mwenyewe lakini.
Ndicho kilichotokea katika jimbo hilo, wanachama wa CCM ambao wamekerwa na mfumo wa
umangimeza, waliamua kuvunja kanuni na miiko ya chama, wakampigia kura Mkosamali, wakijikita katika misingi ya kuwa hiyo ndiyo damu chama itakayoleta mageuzi ya kweli jimboni humo.
Wanachama wa Chadema ambao hawakupoteza muda kumpa ulaji mgombea wao, alihamishia
nguvu zao kumuunga mkono Mkosamali, akashinda kwa ushindi wa kishindo. Katika majimbo mengine vile vile, wagombea waliokuwa wamepitwa na wakati, haikuwa rahisi kupenya
kwenye tundu la sindano, hivyo wakaambulia kugalagazwa.
Ushindi wa Kafulila, Machali na Zeitun pamoja na Mkosamali, umeipa uhai NCCRMageuzi
mkoani Kigoma ambayo ilikuwa inachungulia kaburi kwa idadi ndogo ya wanachama.
Ndiyo maana kutokana na ushindi huo, NCCR imeamka usingizini kwa nguvu mpya ya kushika majimbo mengi mkoani humo na kuanzia hapo cheche zimeanza kusambaa katika majimbo mengine ndani na nje ya mkoa huo.
Siasa ni sawa na kuchanga karata, unaweza kuwa bingwa wa kuandaa karata, lakini mchangaji mzuri akishika, akakufunga bao, hilo ndilo lililowakumba Chadema kupoteza vijana wake dakika za mwisho.