kinyoba
JF-Expert Member
- Jun 2, 2011
- 1,267
- 718
Habari zenu wana JF? Sina hakika Kama ni matawi yote ya NBC au ni hapa tu. Nashangaa kuona watu wamekaa chini sakafuni wazee na akina mama kusubiri foleni iende, inamaana wameshindwa kununua hata mabench watu wakalie hasa ukizingatia foleni ni ndefu? Mwisho wa kazi ni saa9 kamili mchana, hii nayo ni kero maana kutoka ofisini rasmi ni saa 9:30 sasa na wao wakifunga ofisi saa10 kamili kuna ubaya gani? Hili tawi la ubungo ni muhimu kwa wafanyabiashara wasafiri, ingefaa wafunge ofisi hata saa 12 jioni maana magari mengi yanafika Ubungo muda huo! Sikuhizi crdb kuna matawi yanafanya kazi hadi jumapili. Binafsi naona kama hawa NBC wapo nyuma sana sijui ninyi wadau mnasemaje?