NBC LTD waleta mpya!

kachumbari

Senior Member
Nov 1, 2010
125
8
Leo nilikuwa na shida ya vijisenti kwa hiyo kama kawaida nikapita kwa ATM ya NBC LTD ,nikakuta a/c haifanyi kazi kuingia ndani nauliza wanasema wametufungia A/C zetu, mpaka mwenyekiti wa serikali ya mtaa ajaze upya fomu hii hapa.Hii manaake nini? sasa je kwa wale wasafiri ambao wako nje ya matawi yao na wanategemea hizo A/C itakuwaje,hivi pesa yako halafu bank wanaamuua watakavyo wao hii ni halali na si mateso kwa sie tunaojikomba na hawa NBC LTD?View attachment NBCltd.pdf
 
kwa kutumia atm kadi gani mpya au za zamadi..
Haijalishi,halafu haya maswali yote yalisha jibiwa toka tunafungua A/C zetu pale miaka zaidi ya 20 sasa leo wanatuletea ukhanithi kama huu,halafu kama picha tulipofungua tuliwapa picha,juzi tunabadili kadi tuliwapa picha na leo ukijaza form hii uweke picha,mimi nafikiri wanampaka hisa kwa hizi studio.
 
ina maana hela kwenye akaunti haitoki hadi ujaze hizo form?sasa kwa wale ambao hawapo nchini inakuwaje?hii sasa ni kali ya mwaka!ni kwa nbc peke yake au ni benki zote?
 
ina maana hela kwenye akaunti haitoki hadi ujaze hizo form?sasa kwa wale ambao hawapo nchini inakuwaje?hii sasa ni kali ya mwaka!ni kwa nbc peke yake au ni benki zote?

Yaani hawa jamaa sidhani kama wako kwa ajili sisi wateja,ila kwa mishahara yao na matumbo yao tuu,ukiwa nje au ndani wao haliwahusu.
 
Hawa NBC kwa kweli wagumu sana kubadilika...wanafanya kazi kama robot, yaani maamuzi yao mengi huwa hayana logic wala tija kwa mteja..na huwa hawapo flexible kabisa wakisha sema hivyo ndio basii tena mteja unakuwa kama **** inabidi utekeleze tuu..nilifikiri kungekuwa na mabadiliko makubwa baada ya kupata CEO Mpya lakini yale yaleeeee...
 
Back
Top Bottom