Nbc kinondoni wezi!!! {atm}

Mc Kihiga

Member
Mar 17, 2011
36
3
Hii imenitoke tarehe: 21.03.2011 saa: 1437hrs.

Nilifika eneo la Bank hiyo muda huo kwa lengo la kuchukua pesa kweny Mashine pesa {ATM}zilizopo nje ya jengo hilo kamailivyo kawaida.

Awali nilitoa laki nne Tshs: {400,000/=} nilifanikiwa lengo ni kutoa laki tano {500,000/=} ikabaki laki moja, {100,000/=} kumbuka ni mashine ya kushoto kama unaingi.

Kimbembe kilianzia kwenye utoaji wa laki moja ya mwisho mashine ili maliza proccess zote kama kawaida wakati wa kutoa ilito elfu themanini Tshs {80,000/=} tofauti na kiwango kilicho kuwa kwenye listi kwenye listi imesoma laki moja kawaida.

Picture: wakati pesa inatoka elfu Sabini 70,000/= zilikuwa noti za elfu kumi na noti mbili zilikuwa ni elfu tano {5,000/} wakati zinatoka zote kwa pamoja ziliruka nusu ya kudondoka chini noti mbili za elfu tano tano zilionekana kukunjwa kwa marefu zikiwa zimeambatanishwa vyema mara baada ya kuhesabu nikapata kiasi cha elfu themanini badala ya ya laki moja kama nilivyo command.

Ufuatiliaji: Nikaenda kutaka kuingia ndani lakini tayari walikuwa wamesha funga na askari mlinzi aliekuwepo muda ule alikataa kabisa kuonesha ushirikiano kwa madai kuwa muda umeisha hakuna ruhusa ya kuingia ndani mpaka kesho.

Mashaka: Mimi mashaka yangu ni kama ifuatavyo:

i)«» Kwa sasa siwezi kutembea umbali mrrefu kwa usafiri wa umma kwa sababu nilipata ajali hivyo ni lazima nitumie taxi, hivyo kutoka ninapo ishi hadi Kinondoni kwenda na kurudi ni wastani wa elfu Thelathini {30,000/=} kitu amacho akiwezekani kupoteza elfu Thelathini sababu ya kuokoa elfu ishilini?

ii)«» Ni nini kilicho tokea je, ni ubovu wa mashine, na kama ndiyo kwa nini inatumika?

iii)«» Ni mpango mbaya wa fedha ktk mashine husika, na kama ndiyo je, wanaopanga hawana-elimu ya kutosha juu ya kazi hiyo na kama ndiyo ni Wanajamii wangapi watapata hasara na kiasi gani na kwa muda gani, na hiyo pesa inayo salia ktk mashine inatumika vipi?

iv)«» Je, ni hujuma ya Bank ambayo inafanywa na sehemu ya wafanyakazi wasio na maadili katika maslahi binfsi, {Mpango unaoeleweka na baadhi viongozi wakubwa ktk Bank hiyo}?

v)«» Je, siku nikienda watanielewa wakati sina usibitisho au kielelezo muhimu cha makato hayo ambayo si halali, ukizingatia risiti inaonenyasha kuwa nimetoa laki moja?

Uchunguzi binafsi: Mara baada ya kuona juhudi zangu zimekwama nilisubiri ili nione kama kuna Mtu mngine atatokewa na ttz kama langu, lakini cha ajabu watu karibu wote nilishuhudia wakiikwepa mashine ile na kudai si nzuri inakata pesa na kumeza kadi mara kwa mara alisikika mmoja kati ya wateja walio kuwa wakingojea kuchukua pesa ktk mashine hizo.

Mwisho kabisa: Nashkuru sana kwa wana "jf" wote walio shiriki kusoma na watakao kuwa na ushauri mauni wanakaribishwa kuchangia swala hili nilifanikiwa kumpata Chief Security Officer NBC TZ na akashauri niende kesho yake kwa ajili ya ufuatiliaji zaidi katika branch hiyo.

Mc!
 
Jomba machine to hata gari sometyms huwa gear zinaruka, na ukienda itarudi coz huwa kuna camera l do hope, al n al pole nami ilishanitoke crdb
 
Pole sana Mckihiga, na mie imewai kunitokea pale NBC Mlinani city. Nilikomandi laki 2, kwanza ikachukua mdaa sio wa kawaida kutoa pesa, badae sana ikatoka laki na nusu (notes za elf 10), ila what saved me kwenye reciept ikatoa ujumbe, sikumbuki the exact words, kwamba kuna hela yangu imebaki. nilipo enda ndani wale ma 'customer cares', as usual, they never care for customers, wakadai mie ni muongo, tukabishana hadi nikawambia twende kwa manager. manager akosoma reciept, mwishoni sasa ndo naambiwa niandike barua, toa P/copy ya ATM card na ya receipt. Baada ya wiki 3 nilipo check statment yangu hela ilikua imeingia.
Tangu then, najitaidi kutumia ATM ya Branch A/C yangu ilipo, and i never use ATM za 'vibandani'.
This happened to me last year, kama paka leo yanatokea, kuna shida kubwa
 
tatizo ilo lipo katika bank zetu kwani NBC mashine wameingiza mashine zilizotumika huko ulaya........cha msingi ni kuwa wahangalifu na kutokubali kutoa fedha bila risiti..............pole ila unaweza kuliwasilisha tatizo lako kwenye uongozi wa bank au ukiwa na nguvu unaweza kuliwasilisha mahakama ya biashara
 
Pole sana. Mimi nakushauri tatizo lililokupata uwajulishe viongozi wa tawi husika ili wakague mashine zao na ikiwezekana wakupe kiasi ambacho kilikosekana. Hata hivyo bado nakupongeza kwa kuwa mtulivu naamini pamoja na adha uliyopata ila umechukulia kuwa ni tukio la bahati mbaya pengine, ila nasisitiza uwajulishe wa husika ili kama mashine hizo zina tatizo au kuna wafanyakazi wasio waadilifu hatua ziweze kuchukuliwa ili kuepusha watu wengine kupata tatizo la aina yako.
 
Kwa hiyo vamera itaonesha luwa alipata 80 badala ya moja!
Jomba machine to hata gari sometyms huwa gear zinaruka, na ukienda itarudi coz huwa kuna camera l do hope, al n al pole nami ilishanitoke crdb
 
Jomba machine to hata gari sometyms huwa gear zinaruka, na ukienda itarudi coz huwa kuna camera l do hope, al n al pole nami ilishanitoke crdb
wacha mawazo ya kizembezembe ya kutetea uzembe! Kwanini nchi nyingine haya matatizo hayatokei mara kwa mara kama Tanzania!
 
Dah, siombei yanikute. Hela yenyewe ya mawazo.
Peleka taarifa kwa wakuu.
Kutumia elf 30 kudai 20 ni upupu ila kumbuka ile ni haki yako na utawaokoa wengine endapo utafatilia hadi tatizo likawa solved. Huwezi jua, leo wamekata 20 ipo siku watakata pesa yote. Fatilia tu.
 
atm ya kinondoni,ilishawahi kutoa elfu 10 feki.kwa kweli hela yangu iliniuma ila ndio ni kama niliingizwa mjini.
 
Kama haikukupa risiti yoyote ambayo inaonesha kulikuwa na tatizo katika utoaji wa pesa, uwezekano mkubwa ni kuwa katika tawi hilo kuna mtu ambaye si mwaminifu na alichanganya noti za elfu kumi pamoja na za elfu tano. Kwa kawaida noti za thamani mbalimbali zinawekwa kwenye trei tofauti na mashine inazitambua kutokana na trei ambayo pesa hizo zinakuwa zimewekwa. Ndiyo maana mara nyingi kama kuna hitilafu ya kiufundi mashine inatoa risiti moja kwa moja hata kama haujahitaji. La msingi ni kuwa mwangalifu kwani kwa sasa kama kuna ATM ambazo zinatambua noti kwa alama zilizo kwenye noti hizo kulingana na thamani yake basi zitakuwa ni chache MNO (ndani ya Tz). Kwa kifupi uwezekano mkubwa ni kuwa kuna mtu asiyemwaminifu hapo ulipotoa fedha. Ila bila kithibitisho ngoma inakuwa ngumu kwelikweli.
 
Pole sana kaka yangu, nimeshangazwa sana na taarifa yako kwa sababu tatizo hilo limewahi tokea kwa mama pale Muhimbili ATM ya NBC na ilitoa pungufu ya 80,000 na bahati mbaya ilikuwa wkend na hawakumrudishia pesa yake hata baada ya kuzidai, nafikiri kuna kaujanja wanafanza kwa sababu wanatime muda ambao sio wakazi na lazima wako wengi wameisha umizwa. THANKS
 
Me ctakt kusema mengi ila hakuna benk yenye huduma mbovu kn nbc, mara nyingi atm hazifanyi kazi, kuipata iyo atm kadi ni miezi 2, customer care wana lugha mbaya kuptiliza, iliwahi kunitokea mlimani city, tumekaa masaa 2 kwenye folen ya atm pesa hazitoi 2lipoenda kuuliza reception inakuaje hali hii jibu walo2pa ni "mwenye haraka aende kwenye atm zingine" yani najuu.......................ta kuifahamu manake pesa yako kuipata kimbembe, mpaka 2tarudi zama za kuweka pesa chini ya magodoro.
 
Jamani suala la Customer Care kwenye mashirika mengi mbona ni issue jamani?
Tunaomba sana hasa kwenye mabenki mnapoajiri hata kama ni kwa kujuana hao watu wapelekeni kwenye kozi za Customer Care. Sina muda mwingi wa kuelezea kwa mifano niliyokutana nayoni lakini mabenki mengi mteja anajibiwa ovyo.
Hivi suala la kumthamini mteja na kujua kwamba mteja ndo anakufanya uwepo hapo wao hawalijui.
 
Kama haikukupa risiti yoyote ambayo inaonesha kulikuwa na tatizo katika utoaji wa pesa, uwezekano mkubwa ni kuwa katika tawi hilo kuna mtu ambaye si mwaminifu na alichanganya noti za elfu kumi pamoja na za elfu tano. Kwa kawaida noti za thamani mbalimbali zinawekwa kwenye trei tofauti na mashine inazitambua kutokana na trei ambayo pesa hizo zinakuwa zimewekwa. Ndiyo maana mara nyingi kama kuna hitilafu ya kiufundi mashine inatoa risiti moja kwa moja hata kama haujahitaji. La msingi ni kuwa mwangalifu kwani kwa sasa kama kuna ATM ambazo zinatambua noti kwa alama zilizo kwenye noti hizo kulingana na thamani yake basi zitakuwa ni chache MNO (ndani ya Tz). Kwa kifupi uwezekano mkubwa ni kuwa kuna mtu asiyemwaminifu hapo ulipotoa fedha. Ila bila kithibitisho ngoma inakuwa ngumu kwelikweli.

Uko sahihi kabisa, risti imeonesha kiasi sahihi pesa imetoka pungufu je, hiyo Jumatatu nitadai kwa kumbukumbu gani? Ila nakubaliana na wewe kuwa huu ni mchezo mchafu umeanzishwa na Bank hii ili chain iliyo jipanga inufaike hakika kuna Watu ambao si waaminifu wanahusika kwahili!

Mc!
 
Jomba machine to hata gari sometyms huwa gear zinaruka, na ukienda itarudi coz huwa kuna camera l do hope, al n al pole nami ilishanitoke crdb

Nashukuru sana Jomba,
Zingatia mambo yafuatayo: i} Hakuna usibitisho wa kimaandi juu ya mapungufu hayo. ii}Natarajia kwenda hapo siku ambayo naenda Hospital ilikuepuka gharama zisizo za lazima kwani nitakua nimepiga ndege wawili kwa jiwe moja Hospital na NBC je, wataniamini vipi kwa kigezo gani je camera inaweza kuhesabu pesa?

Mwisho hakuna kawaida inayo umiza!!!

Asante sana kwa Mchango wako.

Mc!
 
Pole sana Mckihiga, na mie imewai kunitokea pale NBC Mlinani city. Nilikomandi laki 2, kwanza ikachukua mdaa sio wa kawaida kutoa pesa, badae sana ikatoka laki na nusu (notes za elf 10), ila what saved me kwenye reciept ikatoa ujumbe, sikumbuki the exact words, kwamba kuna hela yangu imebaki. nilipo enda ndani wale ma 'customer cares', as usual, they never care for customers, wakadai mie ni muongo, tukabishana hadi nikawambia twende kwa manager. manager akosoma reciept, mwishoni sasa ndo naambiwa niandike barua, toa P/copy ya ATM card na ya receipt. Baada ya wiki 3 nilipo check statment yangu hela ilikua imeingia.
Tangu then, najitaidi kutumia ATM ya Branch A/C yangu ilipo, and i never use ATM za 'vibandani'.
This happened to me last year, kama paka leo yanatokea, kuna shida kubwa

Asante nimeshapoa,
Nashukuru kwa ushauri wako asante sana infuture nitatumia Samora branch ndiyo nilipo fungulia account.

Mc!
 
tatizo ilo lipo katika bank zetu kwani NBC mashine wameingiza mashine zilizotumika huko ulaya........cha msingi ni kuwa wahangalifu na kutokubali kutoa fedha bila risiti..............pole ila unaweza kuliwasilisha tatizo lako kwenye uongozi wa bank au ukiwa na nguvu unaweza kuliwasilisha mahakama ya biashara

Asante sana Mwana "jf"
Mimi si kwamba risiti sikupata risiti nilipata ila inaonesha kuwa nimechukua laki moja na si themanini kama ilivyo {kiasi nilicho pokea}

Asante sana kwa ushauri!

Mc!
 
Dah, siombei yanikute. Hela yenyewe ya mawazo.
Peleka taarifa kwa wakuu.
Kutumia elf 30 kudai 20 ni upupu ila kumbuka ile ni haki yako na utawaokoa wengine endapo utafatilia hadi tatizo likawa solved. Huwezi jua, leo wamekata 20 ipo siku watakata pesa yote. Fatilia tu.

Ni ushauri mzuri sana nitafuatilia alafu nitakujulisha kupitia safu hii hii!

Mc!
 
Kama haikukupa risiti yoyote ambayo inaonesha kulikuwa na tatizo katika utoaji wa pesa, uwezekano mkubwa ni kuwa katika tawi hilo kuna mtu ambaye si mwaminifu na alichanganya noti za elfu kumi pamoja na za elfu tano. Kwa kawaida noti za thamani mbalimbali zinawekwa kwenye trei tofauti na mashine inazitambua kutokana na trei ambayo pesa hizo zinakuwa zimewekwa. Ndiyo maana mara nyingi kama kuna hitilafu ya kiufundi mashine inatoa risiti moja kwa moja hata kama haujahitaji. La msingi ni kuwa mwangalifu kwani kwa sasa kama kuna ATM ambazo zinatambua noti kwa alama zilizo kwenye noti hizo kulingana na thamani yake basi zitakuwa ni chache MNO (ndani ya Tz). Kwa kifupi uwezekano mkubwa ni kuwa kuna mtu asiyemwaminifu hapo ulipotoa fedha. Ila bila kithibitisho ngoma inakuwa ngumu kwelikweli.

This is uniqe style kuna mjanja kaingia NBC ni utapeli wa nguvu si mchezo.

Mc!
 
Back
Top Bottom