Nawaunga Mkono Madaktari

I smell udini, missionary haijawahi kujenga hospitali zimjengwa naserikali ya kikoloni ambao walikuwa wakiongoza kikristo; walitumia kodi za wananchi wote wa Tanzania, "Hakuna hospitali ya missionary" kuna hospitali za zilizojengwa na serikali za wakoloni wakristo

Kumekucha!
Je zipo zilizojengwa na wafuga watumwa ambao hawakuwa wakristo?! Jamani udini huu mbona utatumaliza!KWANINI kila kitu tunajaribu kumtafuta mchawi na mara zote ni mkristo? Sasa hizo zilizo za serikali ya sasa zimeongeza ubora upi? Kwanini leo madaktari wanagoma? Kwanini huduma zimekuwa "mbovu" kwenye hospitali za serikali? Inakuwaje hospital za misheni za sasa hivi zimeendelea kuwa kimbilio la kila mtu hata asiyekuwa mkristo?

Back to the issue:
Huu mgomo wa madaktari una mengi ndani yake. Madai yao kama yatatekelezwa itakuwa faida hata kwa wagonjwa maana wananchi na serikali watakuwa na HAKI ya kuwataka wawajibike kikamilifu.Huwezi kutegemea huduma bora kutoka kwa daktari mwenye njaa, asiye na vifaa, mwenye hasira na uchungu!Tena ni hatari sana kuhudumiwa na daktari mwenye hasira.Hata wasingegoma, watu bado watakufa kwa kukosa huduma iliyotolewa kwa "moyo mmoja".Daktari anayetumia "ofisi" yake kujitafutia chochote siyo daktari mzuri hata kidogo na ni daktari hatari sana.Serikali ituepushie vifo visivyo vya lazima kwa kuwasikiliza madaktari.

Serikali itende haki kwa kila kundi na siyo kubagua baadhi. Huwezi kusema Wabunge kwa mfano ni bora kuliko madaktari au waalimu. Madhara ya madaktari kugoma ni kupoteza uhai.Madhara ya waalimu kugoma ni kushuka kwa elimu, madhara ya wabunge kugoma ni nini? ITAKULA KWAO WENYEWE!


 
Mkuu Godwine,
Ninalo swali moja tu,
Hospitali zote za Dar es Salaam ambazo nimewahi kwenda kuwatembelea marafiki zangu kitanda kimoja wanalala 3 na wengi wao wako chini. Huduma ni mbovu hakuna dawa, seuse maslahi ya madaktari? Wamesahauilika kabisa. Madaktari wenyewe wanasema tunawabadilishia wagojwa magonjwa. Ukija na Malaria unapewa dawa ya Malaria halafu unaondoka TB kwa sababu ya msongamano. Hali hii mpaka lini?

Madaktari maslahi yao yamebanwa - wako frastrated na hawawezi kutoa huduma bora, hali hii mpaka lini?

Rafiki yangu na ndugu yangu wa karibu alifanyia mama mjamzito operation kwa tochi ya simu majuzi hapo mwananyamala baada ya umeme kukatika. Alipomfuata Mganga mkuu wa hospitali aliambiwa, Sina pesa na Serikali imesema haina pesa. Sasa ameniambia anataka kuacha kazi kuliko kuona wagonjwa wanakufa mbele ya macho yake kwa magonjwa yanayotibika na maslahi yake duni sana. Hali hii hadi lini?

Ifahamike hapa Tanzania hao wagonjwa wa kipato cha chini unaowatetea kwa taarifa ambazo serikali inakubali yenyewe ni kwamba, kwa siku mmoja tu wanakufa wamama wajawazito kati ya 24 hadi 36( within 24 hrs) Sasa kuna vifo gani vipya unavyosema vitasababishwa na mgomo wa madaktari? Vifo vya kizembe vipo tu kabla ya mgomo.



​kwahiyo unadhani wakigoma nani ambae atapata matatizo ? serikali au wananchi masikini? unadhani hakuna njia nyingine ya wao kufikisha ujumbe?


Kuwa daktari ni kitu kigumu sana kwani kuna wakati unatakiwa kutoa ulichonacho hili kuokoa maisha ya wananchi masikini, Dada yangu ni miongoni mwa madaktari walio katika hospitali za serikali kutokana na kipato duni alifungua kampuni ya kusambaza madawa lakini bado ni mtumishi wa serikali lakini kuna wakati analazimika kusaidia dawa wagonjwa bure, kwani inafika wakati anaona hakuna sifa zaidi ya kuwa daktari bora na anataka kuendelea na sifa ya kuwa daktari aliyetibu wagonjwa wengi wakapona na wachache wataokufa mikononi kwake.


Madaktari lazima wajue kuwa wananchi masikini ndio wanaoteseka na sio serikali, je inamaana katika utitiri wa vyama vyote vya siasa na madaktari wameshindwa kutafuta mtu atayewapelekea hoja binafsi za madai yao pasipo kugoma?


Kama tuna Wabunge na wawakilishi kwenye Bunge ambao ndio wanaosimamia serikali lakini wamenyemaza mpaka madaktari wanafikia kugoma na kuua maisha ya watanzania masikini bila ya wawakilishi kuwatetea basi Tatizo si la serikali pekee bali ata Wabunge wetu na vyama vya siasa havina kazi wala msaada kwa wananchi masikini.

Tumeona miswada binafsi mingi ata ya kudai nyumba za serikali lakini sijaona muswada binafsi wa kuwatetea madaktari huu ni usaliti wa wanasiasa na wawakilishi wetu mpaka inafika madaktari wanafikiria kugoma na kuua masikini. sioni umuhimu wa kuwa na vyama vya siasa na wabunge kwani vyote vipo kwa maslahi ya matumbo yao. Nilidhani wabunge wangefikia wakati wa kutoka nje ya bunge kama kawaida yao kabla ya kufikia wakati wa madaktari kugoma
 
Uamuzi wa madaktari kugoma haukuwa uamuzi rahisi; ni uamuzi ambao umekuja ukiwa na gharama kubwa kwao na kwa taifa vile vile. Lakini uamuzi ambao umekuja kwa sababu umelazimishwa. Sera ambazo zimekuwa zikisimamia sekta ya afya zimeonekana kushindwa na sasa haya ni mavuno yake. Upo mgogoro katika sekta hiyo na licha ya kuongezwa kwa vitu bado inaonekana watawala wameshindwa kabisa kujenga mfumo wa kisasa wa afya.

Hivyo, naamini madai ya madaktari ni hatua ya mwanzo ya kudai huduma bora na mfumo wa kisasa. Siamini kama ni suala la mishahara na maslahi ya madaktari tu; binafsi naamini ni suala linalohusiana na a comprehensive healthcare reform.

a. Hatuwezi kuendelea kuwa na serikali inaendesha mahospita mengi ambayo haina uwezo wa kuyahudumia - wakati umefika wa kufikiria serikali kuachia hospitali - ibakie na hospitali kama za jeshi n.k Tunaweza vipi kuzitoa hospitali kutoka kwenye mikono ya serikali na kuzileta kwenye sekta binafsi au ushirikiano wa sekta binafsi na ya umma?

b. Mfumo wa sasa wa centralized policy ya afya kwa taifa zima hata kwa mambo madogo umepitwa na wakati. Ipo haja katika kuangalia mfumo wetu wa afya kufikiria jinsi ya kufanya healthcare kuwa na a local outlook zaidi na hivyo kuwa ni ya sehemu ilipo.

c. Kuboresha maslahi ya watendaji wa sekta ya afya kwa kuweka motisha zaidi, uhuru zaidi na vile vile kuinua elimu. Mojawapo ya matatizo ambayo ni wazi yapo ni jinsi gani madaktari na wauguzi wetu wanakuwa upgraded katika ujuzi na elimu yao.

Ni kwa sababu hizi na nyingine naamini kuunga mkono mgomo wa madaktari ni jambo la kizalendo zaidi kuliko kuendelea kukaa kimya. Wao madaktari wanapodai maslahi zaidi na mafao zaidi wajue kabisa kuwa wananchi nao wanajiandaa kuwadai wao zaidi katika huduma na ubora wa huduma wanazotoa. Hivyo, wasikubali kuachilia kirahisi hadi wawe na uhakika kuwa madai yao ya msingi kabisa yameangaliwa na yanalenga katika kuboresha sekta ya afya nchini.

Nawaunga mkono madaktari katika mgomo wao!

1. Hatuwezi kuendelea kuwa na serikali inaendesha mahospita mengi ambayo haina uwezo wa kuyahudumia - wakati umefika wa kufikiria serikali kuachia hospitali - ibakie na hospitali kama za jeshi n.k Tunaweza vipi kuzitoa hospitali kutoka kwenye mikono ya serikali na kuzileta kwenye sekta binafsi au ushirikiano wa sekta binafsi na ya umma: Serikali ilikuwa na mpango wa kuanzisha mpango huu ambao ungkuwa na bodi za uendeshaji zinazosimamiwa na wananchi. Lakini inaonekana baada ya kuja Katibu Mkuu Mpya na Mganga Mkuu wa Serikali wameacha kabisa mpango huo ambao ulikuwa ndiyo mwokozi wa sekta hiyo. Wilson Mkama anafahamu vizuri hili.

2. Kwa muda mrefu sasa hospitali za mikoa sasa maarufu kama hospitali za rufaa za mikoa zinatumia Ikama za zamani za 1989 kitu ambacho kinafanya uwezo wa hospitali kuongeza watumishi kukidhi mahitaji kuwa mdogo.


3. Hospitali hizi za mikoa kiutendaji ziko chini ya Ofisi za Makatibu Tawala wa Mikoa. Hivyo hutengewa bajeti (Ceilings) zake kulingana na ukomo wa mahitaji ya Ofisi hizo za makatibu tawala wa Mikoa na kufanya zishindwe kujiendesha. Utaratibu wa kuzitoa kwenye ofisi hizi na kuzifanya zijitegemee kama agencies nyingine za serikali ungefanya ziwe na uhuru zaidi wa kupanga bajeti halisi na kuwajibika kwa matumizi mbalimbali. Kwa wastani kwa mwezi sasa hospitali hizi hupokea Tshs. 15M tu.
4. Kuna mkanganyiko mkubwa wa utayarishaji wa miundo ya utumishi wa kada mbalimbali kwenye serikali inayotoa mwanya kwa baadhi ya kada kubebwa zaidi na nyingine kuonekana kuwa hazina maana. Hii imefanya watumishi kukata tamaa. Yapo mabadiliko mengi kwenye sekta ya elimu ambayo hayako kwenye sekta ya afya na sekta nyingine. Miaka ya nyuma Menejimenti ya Utumishi wa Umma waliweza kudhibiti hili. Siku hizi ni bora liende.

Ipo haja kwa serikali kukaa na kutafakari upya dhana nzima ya ajira, miundo ya utumishi na maslahi ya watumishi kulingana na taaluma zao. Vinginevyo tujitayarishe kuona Maafisa Kilimo nao wakigoma.
 
Inawezekana unaamini kabisa kuwa unesema kitu profound! Kweli unafikiri nimechukua msimamo kwa sababu sijawahi kuuguliwa? Kwa vile ndugu zangu wameumbwa kwa mawe? Hivi tunapuzungumza ndugu yangu wa karibuanatakiwa kufanyiwa upasuaji ijumaa hii hapohapo nyumbani. Sasa nichukue msimamo tofauti baada ya kuangalia maslahi yangu kwanza?

Unavyosema hapohapo nyumbani inaoneka uko nje ya nchi. Kama unazungumzia maslahi ya Taifa Ungetakiwa uwe hapa Bongo
 
​kwahiyo unadhani wakigoma nani ambae atapata matatizo ? serikali au wananchi masikini? unadhani hakuna njia nyingine ya wao kufikisha ujumbe?
Kwani unafikiri serikali hii ukiifikishia ujumbe kwa njia nyingine wataelewa? Kama jk anajua davos kuna kikao cha urozone ameenda kufanya nn kama sio kwenda kutangaza kuwa tz kuna mapande ya ardhi ya bure? Na ujumbe kuhusu posho za wabunge kila mtu amepiga kelele hawakusikia.,?

Tusiangalie hili suala kwa jicho moja,wagonjwa kila siku wanakufa kwa sababu ya huduma mbovu zilizopo ila huwa haitangazwi. Kumbuka madactari nao ni watu,wamechoka kufiwa na wagonjwa kila siku sababu ya huduma zilizotelekezwa! Daktari unakuwa frustrated mpaka maisha yako ya kawaida yanakuwa ruined!.. Imagine ni wewe kila siku unafiwa na wagonjwa kwa sababu ya ukosefu wa dawa, vipimo utafurahi!

Angalia bajeti za serikali, mislineous charges zinakuwa kubwa kuliko matumizi yanayofahamika.,unataka kuniambia vitu usivyotegemea kutokea ni muhimu kuliko vinavyofahamika? Wamegeuza haspitali zote kuwa dispensary kwa ajili ya first aid tutafika. Mgonjwa wa hiv akiingi mnh ambako kuna specialist kibao haponi, wanashindwa hata na consolata yenye md 1, AMOs na COs. Tatizo hakuna rehabilitation facilities kwa ajili ya wagonjwa.
 
Naunga mkono hoja!! Totally unfair, haya ndio yanapelekea watu kuingia msituni au barabarani kudai haki yao. Bora basi wangekuwa wanayatumia hayo masaa 7 kuwatengenezea wapiga kura wao fursa za maisha bora.

Wakati Wabunge wamejiongezea posho ya 200 kwa siku na kikao chao ambacho ni masaa 7, wanaanzia saa 3:00 mpaka saa 7:00 mchana na kurudi saa 11jini mpaka saa 2:00 usiku, huku wamekaa kwenye kiti cha luxury wengine wakisinzia tuu au bila kuchangia chochote, huku wengine wakishinda canteen au just kurandaranda viwanja vya bungeni kuamkua jamaa!. Madaktari wao 10,000! kwa shift ya 8 hours usiku mpaka asubuhi!.

Hata vile vi little brown envelopes vya usafiri wa waandishi wa habari minimum ni 20,000! kwa press conference ya 30 min!

Hii ni dharau kwa madakitari wetu!, Acha wagome!.
 
TATIZO LA KUWA NA SERIKALI LEGEVU NA SI SIKIVU.
Hivi kuna shida gani kuwatimua walioshindwa kuwajibika katika sakata hili huko nyuma kama Jonathan alivyomtimua mkuu wa maafande uko Nigeria kwa uzembe, hadi hivi sasa ndio PM anaomba kuonana na Madaktari ili awaombe warudi kazini,na si kutaka kutatua kiini cha migogoro?
 
Itakuwa a very interesting subject kama utafiti utafanyika kulink vifo vinavyotokea kila siku mahospitalini kwetu na
1. Ukosefu wa vifaa
2. Wataalam kulipwa vibaya
3. Ukosefu wa proper training
4. Ukosefu wa dawa n.k.
bila kujali madaktari wako kwenye mgomo au la!
 
hii ni siasa tu
Tanzania haipo sawa na Egypt wala Libya

kama wanasiasa wameshindwa kutoa shinikizo kwa watala
madaktari wasitumike kufanya siasa huku 'watu wasiokuwa na hatia' wanakufa...

serikali iliyopo ni kama viziwi

walijaribu chama cha wafanyakazi na wakazimwa.....

kilichopo sasa ni kujaribu kutoa maji kwenye jiwe while wasio husika ndo watakufa.....

tunajidanganya mno na kuiga Misri na Egypt.....ukweli sisi bado saana.....

wamefukuzwa wanafunzi chuo kikuu hakuna mwanasiasa aliekwenda kuwasaidia.....
tusiwaponze hawa madaktari

utawala huu unahitaji 'political interverntion...na sio madaktari'

Nakuunga mkono isipokuwa hukutoa mawazo kwa madaktari wao (kama binadamu wenye mahitaji sawa na watu wengine) wafanyeje? Serkali ndiyo hiyo imekataa kuwasikiliza waende wapi?
 
hii ni siasa tu
Tanzania haipo sawa na Egypt wala Libya

kama wanasiasa wameshindwa kutoa shinikizo kwa watala
madaktari wasitumike kufanya siasa huku 'watu wasiokuwa na hatia' wanakufa...

serikali iliyopo ni kama viziwi

walijaribu chama cha wafanyakazi na wakazimwa.....

kilichopo sasa ni kujaribu kutoa maji kwenye jiwe while wasio husika ndo watakufa.....

tunajidanganya mno na kuiga Misri na Egypt.....ukweli sisi bado saana.....

wamefukuzwa wanafunzi chuo kikuu hakuna mwanasiasa aliekwenda kuwasaidia.....
tusiwaponze hawa madaktari

utawala huu unahitaji 'political interverntion...na sio madaktari'

pole sana na huo ujima aka ujamaa wako. kila mtu lazima apiganie haki yake. kama wamiliki wa daladala wakigoma wanasikilizwa na kutimiziwa madai yao iweje serikali ishindwe kuwasikiliza watu muhimu kama madaktari? Lakini kumbuka pia, kugoma ni moja ya njia ya kutaka kusikilizwa na sio haki ya walimu, mahouse girl, madereva, lecturers pekee.

Kumbuka pia wao ni binadamu, wana mahitaji muhimu na majukumu kama uliyo nayo wewe. Usidhani wajibu wao ni kukutibu ugonjwa wako wewe tu, na wao wana matatizo yao hivyo kama hayatimizwi, basi maslahi yao yana-take precedence of over your sickness and problems. Itakuwa ujinga tena uliopitiliza kiwango kama unaamua wewe uendelee kupata taabu na kuangamia eti kwa sababu ya uzalendo wa nchi ambayo viongozi wake wanaendelea kushibisha matumbo yao na famioia zao. Ni ujinga usio na kikomo huo na zama zake zilikuwa ni zile za ujamaa na kujitegemea.

Utawala na serikali umemwaga mboga, mimi nawashauri madaktari wamwage ugali na kuutia mafuta ya taa kabisa!
 
Tunaweza vipi kuzitoa hospitali kutoka kwenye mikono ya serikali na kuzileta kwenye sekta binafsi au ushirikiano wa sekta binafsi na ya umma:.

Nsaji Mpoki chonde chonde hapa si utaturudisha tena kule kwa MOU ya serkali na makanisa ambayo sasa imeligawa taifa katika mapande 2?
 
kabla ya mgomo watu walikuwa wanapata hudumu kwa kiwango fulani, lakini kama mgomo ukiendelea basi huduma zitasimama kabinsa na vifo vitaongezeka mara dufu, na vifo vyenyewe vitakuwa vya watanzania masikini wasioweza kwenda hospitali za gharama kubwa. uwepo wa hospitali za umma unasaidia kwa kiwango kikubwa kuliko kutokuwepo kabisa

Wakifa wagonjwa kwa sababu ya mgomo wa madaktari wa kulaumiwa ni aliyesababisha madaktari wetu wagome (serikali kiziwi)! Na ndio itakuwa accountable!
Huduma zinazotolewa ni hafifu na zinagharimu maisha yetu kila siku, ni bora wagome sasa, na wagome kikweli na wapate yooote wanayodai ndipo nasi tuanze kuwadai kupewa huduma nzuri kutoka kwao, leo hii unakwenda hospitari unaangaliwa kama umejinyea kama huna hela ya kuhonga!
Ila wakilegalega kugoma afu na wasipewe wakitakacho itabidi tuwawajibishe kwani wanafanyia mzaha maisha yetu!
 
Hakuna viongozi wanaojali healthcare yetu, kwanza wao sio watumiaji wa hizi Hospital zetu na wala hawajali kama kuna walalahoi watakaopata shida na huu mgomo wa Madaktari.

Kama ingekuwa madaktari wa Apollo wamegoma wakina Vasco wangeongea nao. Hospital za mafisadi au Viongozi wa Tanzania zipo India sio Tanzania.
 
Mwanakijiji,
Nakubaliana na maoni yako kwa ujumla. Lakini hili la mgomo sina uhakika kama ndiyo njia sahihi na ndiyo maana humu jamvini kumetokea mawazo yanayotofautiana. Hoja yako ni vizuri ikapanuliwa. Tatizo kubwa ni la kimfumo; serikali inataka kufanya kila kitu. Mfumo wa centralised policies ndio unachangia kwa kiasi kikubwa katika umasikini wetu. Wananchi wanabakia kuwa watazamaji badala ya kushiriki katika maamuzi na hata kuwajibisha watendaji mambo yanapokwenda kombo.

Tunaweza kuiga kwa kiasi fulani mifumo ya afya ya mataifa yanayoendelea ambako kuna hospiatli/kliniki za umma na watu binafsi. Na madkatari vile vile, bila kujali wanafanyakazi katika hospitali za umma au binafi, wana uhuru wa kufungua kliniki zao. Wengine kiliniki ziko hata nyumbani kwao. Tujaribu kuanzia hapo. Madaktari wataweza kujiongezea kipato chao badala ya kutegemea tu mishahara na posho. Utaratibu shirikishi utaandaliwa namna ya kutekeleza hili. Wakati huo, serikali itakuwa inaboresha huduma pamoja na vifaa katika hospitali za umma. Sekta binafsi nayo ihamasishwe katika kufungua hospitali na kliniki. Wale wenye uwezo wataenda huko.

Mgomo wa madaktari utufungue macho na tuanzishe mjadala mpana jinsi tunavyotaka kuendesha mambo yetu na kuwajibishana. Kuendelea kutegemea maamuzi ya Dar es Salaam kwa kila kitu siyo utaraibu unaotumika katika ulimwengu wa leo. Dhana kubwa ni decentralisation katika maamuzi na kuwajibishana. Kutegemea kila kitu kufanywa na Rais au Wizara ni kuendelea na hadithi za kialinacha kwa sababu maendeleo hayatapatikana na huduma zitaendelea kuwa duni huku tukilalamika kila kikicha. Na kuendesha mambo yetu kwa amri kutoka juu na kutishana hakutajenga. Wanataaluma ya sosiologia na saikoloji watalijua hilii. YUanzisha mjadala mpana na bila jazba kwa lengo la kujenga.
 
hii ni siasa tu
Tanzania haipo sawa na Egypt wala Libya

kama wanasiasa wameshindwa kutoa shinikizo kwa watala
madaktari wasitumike kufanya siasa huku 'watu wasiokuwa na hatia' wanakufa...

serikali iliyopo ni kama viziwi

walijaribu chama cha wafanyakazi na wakazimwa.....

kilichopo sasa ni kujaribu kutoa maji kwenye jiwe while wasio husika ndo watakufa.....

tunajidanganya mno na kuiga Misri na Egypt.....ukweli sisi bado saana.....

wamefukuzwa wanafunzi chuo kikuu hakuna mwanasiasa aliekwenda kuwasaidia.....
tusiwaponze hawa madaktari

utawala huu unahitaji 'political interverntion...na sio madaktari'

Ni kweli Tanzania si sawa na Egypt,naomba nikukumbushe Egypt haikukombolewa na wanasiasa ni wananchi kama wewe,wanasiasa waingia baadae,na ndiyo maana unaona kuna mgawanyiko,kwani wanasiasa waliingia bila kujipanga na kuweka strategic plan.

Unapotoa mfano wa vyuo vikuu wanafunzi kugoma,wanasiasa hawawezi kuingilia kitu bila mpangilio or let me say kushirikishwa,ni kwasababu hujui tu pale wanasiasa waliposhirikishwa wametetea kwa nguvu zote ikiwa ni pamoja na kuwawekea wanasheria.

Tuachane na mawazo mgando,ni sisi wananchi tunaopata huduma za madaktari,ni lazima tuungane na wauguzi na madaktari kuishinikiza serikali kuweka masikio sawa.Malalamiko yao si kwa ajili yao tu bali hata kwetu ni msaada,Nenda Muhimbili wodini wagonjwa wamelazwa chini,je ni haki yatu kulala chini ndani ya miaka hamsini?

jana nimesikiliza Dr akizungumza anasema ameletewa two pairs of gloves for the all day kwa ajili ya theatre.imagine hata kama ni wewe unamgojwa wako, can you accept the same pair of gloves used by someone else to be used for your patient?

Na ukiangalia gloves zinazo nunuliwa ubora wake uko chini sana,unapovaa tu inachanika,am using them for my job,therefore you are forced to double them.

Kumbuka they have families,and they are exposed to several risks.

Tuache kuandika bila kuwazaa kwa makini,ni lazima ni lazima wananchi tuungane sasa kuilazimisha serikali kuwa sikivu vinginevyo madhara ni kwetu sote.

This goverment doesn't need political intervetion as the first thing,it needs community intervetion, let the society come together join hands together and fight for their future,i mean everybody the political leader who always put things open for you to understand what the government is doing will join and support the move.
 
I strongly support them MDs....inasikitisha madaktari na wauguzi wanaoshinda wakihangaika na mavi, mkojo,damu,mifupa, sifongo, viungo vyote na uhai wa wagonjwa, wanapodai haki zao hawatekelezewi(wacha tu kusikilizwa)wakati wabunge wanaoshinda wamekaa kitako siku nzima na matumbo yao dodoma (huku wengine wakilala usingizi)wanaongezewa posho bila jasho.

Inasikitisha zaidi unapomwona hata waziri mkuu eti ana support wabunge kuongezewa posho(kwa kuwa na yeye atanufaika)huku akisema eti atajitahidi kuwasikiliza ma drs!!.....

kuwasikiliza madaktari ni tofauti na kutekeleza matakwa yao......hizi siasa ndio tunatakiwa kuzipinga....nawasihi madaktari wasikubali tu eti kusikilizwa na PM bali watekelezewe matakwa yao kama wabunge.......kukubali kusikilizwa kuendane na utekelezaji wa matakwa yao otherwise mambo yatabaki kuwa business as usual....angalizo kwa drs.....
 
Inatosha nadhani historia ilimpita mbali kidogo. Mchangia aliyepita amemkata shule ya kutosha kwenye hu mchango wa ufahamu wake, hata mimi nimeelewa naamini naye ameelewa pia. Mmi siyo mchangiaji lakini michango mingi inaelimisha sana ila matusi asiyekuwa anjua kitu siyo mazuri maana inaibua jazba na kuendeleza mabiso badala ya yeye kuelewa.


Pumbafu wewe... umejaaa udini tuuu pasipo kujua unachoandika... Yaani nia yako ilikuwa kuuponda ukristo na mfumo wa kikrustu uliokuwepo kisa wakoloni wa kijerumani walikuwa wakristo... Hujui kama na waarabu walitawala... wao wameacha nini ambacho kinaonekana?? Wameacha shule ngapi au hospitali ngapi.... iwe Znz au Bara... Acha uzuzu kabisa... Na by the way hospitali za missionary si lazima ziwe za wakristu hata waislam wanazo... ni charitable institutions, mwehu wewe..
 
Back
Top Bottom