Nawashukuru na kuwapongeza wana-CCM hapa JF, wana-CHADEMA hapa JF tuige haya....

Logical and substantive words to be found in the thread and even though some people might tend to controvert and disparage it the purport of its message has directly been comprehended. It's true that the Africans and particulary Tanzanians are groomed and grown to respect and cherish other people's values and dignity before thinking about anything else. We traditionally come together and join our hands during ceremonies but also we always express our sympathy at those who are in misery. So it turns out to be deplorably disappointing thing to see some of apparent unrefined quarters come out unabashedly to express their ectasy at the death of our fellow citizen just because they are coming from the opposite political side. This uncouth habit should better be reproved and discouraged as early as possible before it develops to become deep-rooted.
 
Pole sana kamanda feki kwa kufiwa na mbunge wako,ni kweli inauma bana.

Nashukuru mkuu nimefiwa na mtanzania mwenzangu,nauhuzunika sana,nilitegemea hawepo ili tuendeleze mapambano yetu dhidi yake kupitia hoja,lakini ndio hivyo...thanx indeed!!
 
Hata iweje siwezi badili huu msimamo mpaka kifo...kifo cha mwenzako si cha kushangilia,kila mmoja anaenda kufa,na kwa kweli usije ukakufuru Mungu na ukamfuata Jerimiah Sumari...Hoja yangu ni kuwa tuwe wavumilivu hasa kwenye vifo na sitaacha kuwa CHADEMA na kadi yangu ya uanachama ninayo.

Ubinadamu kwanza vyama baadae!!
 
Kwa akili yako timamu unadhani hata jambazi akifa unataka tuseme R.I.P.? Be matured mazee!

Mkuu Mungi naomba akili yangu isiwe timamu kwa hili na naomba akili yangu isiwe matured kwa hili...maneno yako ya kejeli hayawezi kufuta ukweli kuwa kifo cha mwenzako si cha kushangilia hata kidogo...mimi sijui kama Sumari alikuwa jambazi au la,ila nachosema tuweni wavumilivu kwenye misiba...mapambano yetu yasiwe ni ushetani bali yawe ni vita ya kudai haki na usawa...
 
Kimsingi si busara na ni ukame mkubwa wa hekima kuanza kumbeza marehemu kwasababu ati alikuwa wa kundi fulani na hivyo hakuwa mwenzetu.Kama kweli kuna mwana- cdm au hata mtu baki katuma hizo threads basi atambue kuwa hajamtendea haki marehemu.Na hiyo ni sawa na wanafamilia kuanza kujadili suala la mirathi hata kabla marehemu hajazikwa.
 
ungeweka mfano wa mwanachadema aliyeanzisha thread ya kusaka ubunge kipindi cha msiba ungeeleweka zaidi,
niliona thread 1 tu ilianzishwa na KIM KARDASH kutaka Dr. Slaa akagombee, na ile alianzisha makusudi ili propaganda km hii thread ziwepo. KIM KADARSH sio CDM, ni gamba,
 
Sijui kama mtoa mada anaweza kututhibitishia kuwa waliotoa threads za hivyo ni Chadema kweli... Halafu kumbukumbu yake itakuwa haiko sawa, anatoa sifa kwa kutaja ID ambazo comments zao wakati wa vifo vya Nyamongo au Arusha zikiwekwa hapa ataficha uso wake!!! Kama ulikuwa hujui hakuna watu makatili na wasio na utu kama wanaoiunga mkono ccm huku wakijua mateso yote ya raia wa nchi hii.
 
Mwajua dada yule kwa harakaharaka aligain sympathy ya watu kutokana na juhudi zake binafsi..
Yaani yule hata angekuwa ni mbunge wa CCM,angegain sympathy ya wana JF wengi likewise..

Kwanza ni binti mdogo,mwenye nafasi kubwa ya kuwakilisha jamii katika chombo kikubwa cha kutunga sheria..

Pili,alikuwa mlemavu wa kiungo cha mwili. Kwa hili,sympathy inajengeka automatically kutokana na maumbile yake,lakini zaidi ni kwa kumuangalia jinsi yeye binafsi asivyoona hilo kama handicap kwake..

Tatu,jinsia yake.. Binadamu wengi hutend kuwa na huruma kwa akina mama,wanaokutwa na matatizo makubwa..

Nne,alikuwa mwana JF.. Hili halina haja ya kulielezea, maana mara nyingi tunaguswa nyoyo zetu tunapompoteza mtu tunayemfahamu kuliko tusiyemfahamu..
 
Kumbuka kuwa siasa ni vitu vya kusadikika, hakuna dunia hii kiongozi hata mmoja ambae hana mpinzani, lakini upinzani wetu wa kisiasa usihusishe vitu ambavyo mimi na wewe havipo katika uwezo wetu, kama kifo. "Kifo Hakina Huruma" si kwa CCM wala CHADEMA.

Kila mmoja wetu ambae sisi tunapingana nae kuna wengine wanaomshangilia, mshabikia, mtegemea, mfatilia na wanao mpenda kiasi cha kwamba hata akifanya kosa wako tayari kumkingia kifua.

Sisi hatuna ugomvi na yoyote anaetutangulia mbele ya haki, ikiwa kaacha mema tutayataja, ikiwa kaacha uovu tutautaja, mradi isije jamii ikajifunza mabaya na kuacha mema.

Kumbuka kuwa "siasa" ni neno linaloashiria amani na kutumia njia za kufikia malengo kwa kukinaishana kwa mema zaidi, ikiwa leo tutaanza kususiana hata wafu, sasa inakuwa siasa au vita? Hata kanuni za kivita zinatoa mwanya kwa wafu kuheshimiwa.

Wana Chadema wanao mbeza marehemu kwa kuwa tu alikuwa Mbunge wa CCM hao si watu wa kawaida na sidhani kama wanaiwakilisha CHADEMA, hao ni wanazi na washabiki wasio kuwa na fikra hata kidogo na siwezi kuilaumu CHADEMA nzima kwa mapungufu ya wajivuni wachache.

sina shaka kuwa una akili timamu, lakini katika hili umechemka na unataka kulazimisha kuhurumiwa kwa kuondokewa na mtu anayekuhusu. Nakumbuka sana maneno yako uliyoyatoa tena ya kejeli na kashfa kuhusu MAUAJI YA ARUSHA, ukadai kuwa wale watu waliuawa kwa kiherehere chao, ukayarudia maneno kama hayo kuhusu MAUAJI YA NYAMONGO, sasa iweje leo utake kuwapumbaza kana kwamba wana mageuzi hawaweki kumbukumbu. Mapambano yataendelea, iwe msikitini, kanisani, mikusanyiko ya aina yoyote, ikiwa pamoja na kwenye misiba. Simkejeli mzee wangu Sumari, lakini lazima nikiri kuwa urithi aliotuachia ni jimbo letu la Arumeru Mashariki. R.I.P. Mzee Sumari.
 
Kijana we2 alikuwa bado mbichi, mzee sumari alikuwa mzee ni haki yake mzee kufa!
 
Back
Top Bottom