Nawashukuru na kuwapongeza wana-CCM hapa JF, wana-CHADEMA hapa JF tuige haya....

only83

JF-Expert Member
Oct 15, 2010
5,343
2,525
...Baada ya kutokea msiba wa mum Regia nilipatwa na mshituko mkubwa,na nilipoingia kwenye threads zilizokuwa zikizungumzia habari za kifo chake niliona sura ya upendo na mshikamano toka kwa wanachama wa CHADEMA na zaidi toka kwa wanachama na wapenzi wa CCM hapa JF...Kwa kweli sikutegemea mtu kama Malaria Sugu, FaizaFoxy, Mwita25 nk kutoa pole nyingi kwa kila threads iliyokuwa inahusu kifo cha mum Regia...wana-CCM hapa JF walijitahidi sana kuficha makucha yao kupitia kwenye kivuli cha upendo na mshikamano....

...Leo nimesikia kuwa Mbunge Jerimiah Sumari amefariki usiku wa jana,kilichonisikitisha ni kuona baadhi ya wana-CDM wakishukuru na kutoa threads na comments za kuanza kupanga kuchukua jimbo la Arumeru Mashariki,mbaya zaidi,narudia tena mbaya zaidi kuna watu wanatoa maneno ya kejeli na kuudhi dhidi ya marehemu,najiuliza kwanini tusiwe wavumilivu kama wana-CCM walivyokuwa wakati wa kifo cha mum Regia? Mimi ni mwanachama damu damu wa CDM na kwa kweli ukiangalia hata chembechembe za damu zangu ni CHADEMA..

Lakini trend hii ya baadhi ya wana-CHADEMA kuanzisha threads za kujipanga kuchukua jimbo wakati wenzetu wa CCM wanasikitika kupoteza mwanachama na mpendwa wao sikubaliani nayo hata chembe...

Nawasilisha!!
 
Huo si uungwana kwa kweli kwani msiba ni jambo zito sana halipaswa kufanyiwa utani.
 
Kweli wewe ni Muungwana sana. Keep it up. Ila mkuu ujue kwamba wenzetu walijua Mh. Regia hana jimbo, na hata wangefanyeje wasingepata nafasi yake. Hatupendi yatokee kwa upande wetu tukio litakalohusu jimbo lakini hapo ndiyo utawajua akina FF, MS, nk.
 
Huo si uungwana kwa kweli kwani msiba ni jambo zito sana halipaswa kufanyiwa utani.

Ni kweli msiba ni msiba habari za kejeli hazifai lkn kila mtu apate haki yake. Idd amin alivokufa hakubadili kuwa yeye alipata kuwa nduli idd amin dada. Regia sisi wana jf tumeshiriki sana kwa kuwa alikuwa member wa jamii forum ndo maana tulifika ifakara na kuvaa zile tshirt. Msiba wa Regia haujaunganisha cdm na ccm japo wengi wamejitahidi kuutumia kuosha nyota zao. Kama mtu alikuwa nduli idd amini na ataendelea kuwa nduli idd amini tu.
 
Kumbuka kwamba members walikuwa wamoja kwa Regia siyo kwasababu yeye ni Mbunge wa CDM, bali kwakuwa alikuwa Jf member. Mkuu umepigwa changa la macho!!
 
Kwenye misiba kunakuwaga na jokes, either kwenye kucheza bao ama draft. Jf inawakilisha jokes zetu kwenye msiba.
 
we mnafiki unajifanya cdm damu lakini akili yako kwa hoja hii unafikiri kama malaria sugu.
Waache watu waamue kule nyumbani kwetu kibirizi kama mtu huwa hafiki msibani lazima mumuonyeshe kuwa kukosa kufika msibani ni dhambi. Mtamuonesha kwa bakora kumi na mbili kbla ya kutoa heshima kwa marehemu wake. Regia aliijenga ile hali ya kuwa na watu. Ukijitenga hadi ahera utatengwa tu ndugu yangu utake usitake. RIP Jeremiah Sumari
...Baada ya kutokea msiba wa mum Regia nilipatwa na mshituko mkubwa,na nilipoingia kwenye threads zilizokuwa zikizungumzia habari za kifo chake niliona sura ya upendo na mshikamano toka kwa wanachama wa CHADEMA na zaidi toka kwa wanachama na wapenzi wa CCM hapa JF...Kwa kweli sikutegemea mtu kama Malaria Sugu,FaizaFoxy,Mwita25 nk kutoa pole nyingi kwa kila threads iliyokuwa inahusu kifo cha mum Regia...wana-CCM hapa JF walijitahidi sana kuficha makucha yao kupitia kwenye kivuli cha upendo na mshikamano....

...Leo nimesikia kuwa Mbunge Jerimiah Sumari amefariki usiku wa jana,kilichonisikitisha ni kuona baadhi ya wana-CDM wakishukuru na kutoa threads na comments za kuanza kupanga kuchukua jimbo la Arumeru Mashariki,mbaya zaidi,narudia tena mbaya zaidi kuna watu wanatoa maneno ya kejeli na kuudhi dhidi ya marehemu,najiuliza kwanini tusiwe wavumilivu kama wana-CCM walivyokuwa wakati wa kifo cha mum Regia? Mimi ni mwanachama damu damu wa CDM na kwa kweli ukiangalia hata chembechembe za damu zangu ni CHADEMA..Lakini trend hii ya baadhi ya wana-CHADEMA kuanzisha threads za kujipanga kuchukua jimbo wakati wenzetu wa CCM wanasikitika kupoteza mwanachama na mpendwa wao sikubaliani nayo hata chembe...

Nawasilisha!!
 
we mnafiki unajifanya cdm damu lakini akili yako kwa hoja hii unafikiri kama malaria sugu.
Waache watu waamue kule nyumbani kwetu kibirizi kama mtu huwa hafiki msibani lazima mumuonyeshe kuwa kukosa kufika msibani ni dhambi. Mtamuonesha kwa bakora kumi na mbili kbla ya kutoa heshima kwa marehemu wake. Regia aliijenga ile hali ya kuwa na watu. Ukijitenga hadi ahera utatengwa tu ndugu yangu utake usitake. RIP Jeremiah Sumari

Congrats Mkuu
 
Kumbuka kwamba members walikuwa wamoja kwa Regia siyo kwasababu yeye ni Mbunge wa CDM, bali kwakuwa alikuwa Jf member. Mkuu umepigwa changa la macho!!

Vyovyote vile itakavyokuwa,inapaswa kufahamika kuwa kifo ni kitu kingine kabisa,ni bora tupigane kejeli na matusi kwenye mambo mengine..inapotokea kuwa umefiwa au mtu kafariki lol!! ni hali ngumu..mimi nina uzoefu wa kufiwa na baba yangu,real inauma siku unapoambiwa kuwa ndugu yako kalala mauti...maumivu haya ndio yanasababisha nijisikie vibaya mtu anapocheza na kifo cha mtu...Hivi ndugu zake wakiingia hapa JF na kuona hizi threads watasemaje kuhusu CDM?
 
pamoja na Msiba wa Regia kuwa na mguso tofauti kutokana na tulivyomzoea,sikubaliani na baadhi ya wanacdm kutuma message za ovyo! Kuzungumzia uchaguzi haikwepeki!pamoja na kuwa viti maalum pia Watu walijadili wa kumrithi Regia!
 
...Baada ya kutokea msiba wa mum Regia nilipatwa na mshituko mkubwa,na nilipoingia kwenye threads zilizokuwa zikizungumzia habari za kifo chake niliona sura ya upendo na mshikamano toka kwa wanachama wa CHADEMA na zaidi toka kwa wanachama na wapenzi wa CCM hapa JF...Kwa kweli sikutegemea mtu kama Malaria Sugu, FaizaFoxy, Mwita25 nk kutoa pole nyingi kwa kila threads iliyokuwa inahusu kifo cha mum Regia...wana-CCM hapa JF walijitahidi sana kuficha makucha yao kupitia kwenye kivuli cha upendo na mshikamano....

...Leo nimesikia kuwa Mbunge Jerimiah Sumari amefariki usiku wa jana,kilichonisikitisha ni kuona baadhi ya wana-CDM wakishukuru na kutoa threads na comments za kuanza kupanga kuchukua jimbo la Arumeru Mashariki,mbaya zaidi,narudia tena mbaya zaidi kuna watu wanatoa maneno ya kejeli na kuudhi dhidi ya marehemu,najiuliza kwanini tusiwe wavumilivu kama wana-CCM walivyokuwa wakati wa kifo cha mum Regia? Mimi ni mwanachama damu damu wa CDM na kwa kweli ukiangalia hata chembechembe za damu zangu ni CHADEMA..

Lakini trend hii ya baadhi ya wana-CHADEMA kuanzisha threads za kujipanga kuchukua jimbo wakati wenzetu wa CCM wanasikitika kupoteza mwanachama na mpendwa wao sikubaliani nayo hata chembe...

Nawasilisha!!

Kwa akili yako timamu unadhani hata jambazi akifa unataka tuseme R.I.P.? Be matured mazee!
 
Duh,
Yaani umeamua kuianzishia thread kabisa.
Ujue tu kwamba mazingira ya hivi vifo Na ubunge wao havifanani kabisa.
Huyu mkuu wa jana ilishajulikana kitambo tu kua soon mambo yatakua si mambo, so hata huzuni yake sio kiviile sana kulinganisha na kipenzi cha wengi RM (Rip).
Pili kwenye ubunge wa RM, kinyang'anyiro kinabaki CDM tu, Magamba hawahusiki hapa, so hawawezi kunyemelea kitu ambacho wanajua hakiwahusu. Compare to ubunge wa Sumari (Rip) ambapo ni gombania goli a.k.a sandakalawe.
Tatu usiweke sana utu kwenye siasa ambazo zenyewe hazina utu Na Wewe mkuu.
Wacha watu wapashe kuchukua jimbo safari hii
 
Vyovyote vile itakavyokuwa,inapaswa kufahamika kuwa kifo ni kitu kingine kabisa,ni bora tupigane kejeli na matusi kwenye mambo mengine..inapotokea kuwa umefiwa au mtu kafariki lol!! ni hali ngumu..mimi nina uzoefu wa kufiwa na baba yangu,real inauma siku unapoambiwa kuwa ndugu yako kalala mauti...maumivu haya ndio yanasababisha nijisikie vibaya mtu anapocheza na kifo cha mtu...Hivi ndugu zake wakiingia hapa JF na kuona hizi threads watasemaje kuhusu CDM?

Kwa taarifa yako mimi nilifiwa na wazazi wote wawili kwa mara moja, kwahiyo najua maumivu ya kufiwa. Tatizo njia unayotumia kutaka kuwaaminisha watu unachokiamini siyo kabisa.
 
we mnafiki unajifanya cdm damu lakini akili yako kwa hoja hii unafikiri kama malaria sugu.
Waache watu waamue kule nyumbani kwetu kibirizi kama mtu huwa hafiki msibani lazima mumuonyeshe kuwa kukosa kufika msibani ni dhambi. Mtamuonesha kwa bakora kumi na mbili kbla ya kutoa heshima kwa marehemu wake. Regia aliijenga ile hali ya kuwa na watu. Ukijitenga hadi ahera utatengwa tu ndugu yangu utake usitake. RIP Jeremiah Sumari

Mkuu mimi nashukuru sana kwa kunigundua kuwa mimi ni mnafiki,lakini naomba niwe mnafiki kwa hili,siwezi kubadilika na kuungana na baadhi ya watu kushangilia kifo cha mtu wakati na mie sijui ni dk ipi nitalala mauti....nashukuru!!
 
Hivi unaweza kuzuia members, hata wangekuwa 50 tu kuwa wasiongelee kitu usichotaka wewe?...utawadhibiti vipi wakati hujui wako wapi na wanafanya vitu gani, na hujui walikuwa na mahusiano gani na marehemu, au familia yake?
Wanaoelewa wanaelewa, lakini kama unaendelea kuona kejeli na kauli za kugombea jimbo ujue kuwa ndio basi tena huwezi kudhibiti hali hiyo, na kwa maana hiyo hakuna sababu ya kupandisha thread, maana kwao utakuwa una'insinuate reaction yao kwa kasi zaidi!
 
Vyovyote vile itakavyokuwa,inapaswa kufahamika kuwa kifo ni kitu kingine kabisa,ni bora tupigane kejeli na matusi kwenye mambo mengine..inapotokea kuwa umefiwa au mtu kafariki lol!! ni hali ngumu..mimi nina uzoefu wa kufiwa na baba yangu,real inauma siku unapoambiwa kuwa ndugu yako kalala mauti...maumivu haya ndio yanasababisha nijisikie vibaya mtu anapocheza na kifo cha mtu...Hivi ndugu zake wakiingia hapa JF na kuona hizi threads watasemaje kuhusu CDM?

Pole sana kamanda feki kwa kufiwa na mbunge wako,ni kweli inauma bana.
 
Back
Top Bottom