only83
JF-Expert Member
- Oct 15, 2010
- 5,343
- 2,525
...Baada ya kutokea msiba wa mum Regia nilipatwa na mshituko mkubwa,na nilipoingia kwenye threads zilizokuwa zikizungumzia habari za kifo chake niliona sura ya upendo na mshikamano toka kwa wanachama wa CHADEMA na zaidi toka kwa wanachama na wapenzi wa CCM hapa JF...Kwa kweli sikutegemea mtu kama Malaria Sugu, FaizaFoxy, Mwita25 nk kutoa pole nyingi kwa kila threads iliyokuwa inahusu kifo cha mum Regia...wana-CCM hapa JF walijitahidi sana kuficha makucha yao kupitia kwenye kivuli cha upendo na mshikamano....
...Leo nimesikia kuwa Mbunge Jerimiah Sumari amefariki usiku wa jana,kilichonisikitisha ni kuona baadhi ya wana-CDM wakishukuru na kutoa threads na comments za kuanza kupanga kuchukua jimbo la Arumeru Mashariki,mbaya zaidi,narudia tena mbaya zaidi kuna watu wanatoa maneno ya kejeli na kuudhi dhidi ya marehemu,najiuliza kwanini tusiwe wavumilivu kama wana-CCM walivyokuwa wakati wa kifo cha mum Regia? Mimi ni mwanachama damu damu wa CDM na kwa kweli ukiangalia hata chembechembe za damu zangu ni CHADEMA..
Lakini trend hii ya baadhi ya wana-CHADEMA kuanzisha threads za kujipanga kuchukua jimbo wakati wenzetu wa CCM wanasikitika kupoteza mwanachama na mpendwa wao sikubaliani nayo hata chembe...
Nawasilisha!!
...Leo nimesikia kuwa Mbunge Jerimiah Sumari amefariki usiku wa jana,kilichonisikitisha ni kuona baadhi ya wana-CDM wakishukuru na kutoa threads na comments za kuanza kupanga kuchukua jimbo la Arumeru Mashariki,mbaya zaidi,narudia tena mbaya zaidi kuna watu wanatoa maneno ya kejeli na kuudhi dhidi ya marehemu,najiuliza kwanini tusiwe wavumilivu kama wana-CCM walivyokuwa wakati wa kifo cha mum Regia? Mimi ni mwanachama damu damu wa CDM na kwa kweli ukiangalia hata chembechembe za damu zangu ni CHADEMA..
Lakini trend hii ya baadhi ya wana-CHADEMA kuanzisha threads za kujipanga kuchukua jimbo wakati wenzetu wa CCM wanasikitika kupoteza mwanachama na mpendwa wao sikubaliani nayo hata chembe...
Nawasilisha!!