Habari zenu waheshimiwa mabibi na mabwana
Naomba ushauri wa jinsi ya kutatua tatizo langu la mapenzi ambalo mwenyewe linanikera na nahisi mwenzangu anakuwa mnyonge.
Ninahisi nawapenda zaidi watoto kuliko ninavyompenda baba yao. Muda wangu mwingi nautumia na watoto, kuanzia asubuhi kuwatayarisha kiusafi, kuwapa kifungua kinywa, na kuhakikisha wamekwenda shule kwa wakati stahiki. Baada ya hapo ni zamu yangu kujiandaa na kutoka nyumbani. Wakati mwingine nasahau hata kumwamsha baba watoto, kumwandalia nguo za kuvaa etc.
Nikirudi kutoka kazini jioni, nakuwa busy kutayarisha chakula cha jioni na baada ya hapo kuwasimamia na kuwasaidia watoto kufanya homework, na kuhakikisha kuwa wamelala wakati muafaka. Baada ya watoto kuwa wamelala naanza kufanya usafi wa nyumba, na kufanya maandalizi ya shule kwa watoto siku inayofuata, kunyoosha nguo zao, kuhakikisha kila mtu kaweka sawa vifaa vyake vya shule kwenye begi, na kuandaa snacks zao. Baada ya hapo huwa nahisi kuchoka mno na ninapoingia kitandani nalala fofofo.
Weekends niko busy na watoto kufanya shopping ya groceries, kutengeneza bustani, kufua, kucheza nao, kufanya homework na wakati mwingine kutembelea ndugu,jamaa na marafiki . Sina muda ambao naspendi na mume huyu na sijisikii kumpa attention ya kutosha. Mara nyingi huna naona ni wajibu wake kujimudu kwani ninahisi majukumu ya kuwalea na kuwasaidia watoto ndio ya kupewa kipaumbele, na wakati mwingine yananizidi.
Huwa nahisi anakuwa mnyonge. Hata nikijilazimisha, najikuta niko nae lakini mawazo yangu yote yako kwa watoto, huyu nahitaji kile, huyu kakosea hivi, huyu kafanya utundu huu na mawazo kama hayo. Wiki yangu huwa imekwisha na wiki inayoanza mchakamchaka wake ni hivyo hivyo.
Je kuna ambao hali hii inawatokea? Je mnakabiliana nayo vipi au ni mambo ya kawaida?
Naomba ushauri wa kukabiliana na hii hali kama sio ya kawaida, ili ni balance mapenzi.
Naomba ushauri wa jinsi ya kutatua tatizo langu la mapenzi ambalo mwenyewe linanikera na nahisi mwenzangu anakuwa mnyonge.
Ninahisi nawapenda zaidi watoto kuliko ninavyompenda baba yao. Muda wangu mwingi nautumia na watoto, kuanzia asubuhi kuwatayarisha kiusafi, kuwapa kifungua kinywa, na kuhakikisha wamekwenda shule kwa wakati stahiki. Baada ya hapo ni zamu yangu kujiandaa na kutoka nyumbani. Wakati mwingine nasahau hata kumwamsha baba watoto, kumwandalia nguo za kuvaa etc.
Nikirudi kutoka kazini jioni, nakuwa busy kutayarisha chakula cha jioni na baada ya hapo kuwasimamia na kuwasaidia watoto kufanya homework, na kuhakikisha kuwa wamelala wakati muafaka. Baada ya watoto kuwa wamelala naanza kufanya usafi wa nyumba, na kufanya maandalizi ya shule kwa watoto siku inayofuata, kunyoosha nguo zao, kuhakikisha kila mtu kaweka sawa vifaa vyake vya shule kwenye begi, na kuandaa snacks zao. Baada ya hapo huwa nahisi kuchoka mno na ninapoingia kitandani nalala fofofo.
Weekends niko busy na watoto kufanya shopping ya groceries, kutengeneza bustani, kufua, kucheza nao, kufanya homework na wakati mwingine kutembelea ndugu,jamaa na marafiki . Sina muda ambao naspendi na mume huyu na sijisikii kumpa attention ya kutosha. Mara nyingi huna naona ni wajibu wake kujimudu kwani ninahisi majukumu ya kuwalea na kuwasaidia watoto ndio ya kupewa kipaumbele, na wakati mwingine yananizidi.
Huwa nahisi anakuwa mnyonge. Hata nikijilazimisha, najikuta niko nae lakini mawazo yangu yote yako kwa watoto, huyu nahitaji kile, huyu kakosea hivi, huyu kafanya utundu huu na mawazo kama hayo. Wiki yangu huwa imekwisha na wiki inayoanza mchakamchaka wake ni hivyo hivyo.
Je kuna ambao hali hii inawatokea? Je mnakabiliana nayo vipi au ni mambo ya kawaida?
Naomba ushauri wa kukabiliana na hii hali kama sio ya kawaida, ili ni balance mapenzi.