Nawaombeni tumshauri huyu mtanzania mwenzetu

UZEE MVI

JF-Expert Member
Feb 6, 2011
232
58
Salama wakuu. Habari za jioni na poleni sana na majukumu ya ujenzi wa taifa? Natumai mu wazima. Niko karibu na kijana mmoja hapa anahitaji ushauri juu ya shida iliyomkuta ndani wiki mbili zilizopita. Hebu nivae koti lake na kuwaeleza kilichomsibu.

Naitwa X naishi na kufanya kazi mkoani Mbeya. Nina mchumba wangu aitwaye Y mabaye tulianza urafiki tangu mwaka 2009 ambaye kwa sasa anaishi Dar. kutokana na sababu ambazo wote hatukuzielewa mapema tulijikuta tuna mtoto mmoja amabaye sasa ana anakaribia kufunga mwaka wa pili. Tumeendelea kushirikiana kumlea huyo mtoto hadi leo na tumeendelea kupendana na kuheshimiana kama kawaida japo kuna mambo madodo madogo ambayo yalitufanya tugombane lakini tuliyaongea yakaisha.

Kutokana na hali ya kipato kuwa duni nimechelewa kukiri mbele ya wazazi wake kuwa mtoto ni wangu na kwamba mama yake(yaani mchumba wangu) nitamwoa, Japo wazazi wake wote wananifahamu na nahusiana nao vizuri lakini nilikuwa sijafanya ile mila.

Mara chache nimejaribu kufanya hivyo lakini nilishindwa kwa sababu ya kipato.(mimi ni fundi seremala) Miezi michache iliyopita nimejikusanya na kujikaba kila kona ili niweze kutimiza mila na hatimaye niweze kukabidhiwa mke na mtoto. Wazazi wangu wote wawili na wazazi wake wanajua juu ya maandalizi haya na kwa upande wa wazazi wangu, wameshajiandaa kwenda dar kutekeleza hili jambo. Mawasiliano yameenda vizuri lakini wiki mbili zilizopita mchumba wangu Y amesema tusitishe hii safari, unless kama naenda tu kuona mtoto wake, ila kwa upande wake yeye tayaria na mtu mwingine.

Sasa nimechanganyikiwa. nadhani hii imekuwa ghafla kwangu.

Naomba ushauri wenu, nifanyeje?
 
Kaa chini na kumshukuru Mungu kwa kuliruhusu hilo likutokee, BARAKA au LAANA ni Mungu pekee ajuaye!
 
Baba gani wewe? Yani sababu ya kipato ndio inakufanya umkane mtoto wako?Umechanganyikiwa nini sasa?wacha wanaojua majukumu waoe bana,you are not a right candidate for her.
 
Baba gani wewe? Yani sababu ya kipato ndio inakufanya umkane mtoto wako?Umechanganyikiwa nini sasa?wacha wanaojua majukumu waoe bana,you are not a right candidate for her. Ndio nyie mnakimbiaga familia mambo yakienda kombo.
 
dah, pole zake sana.
Hamna cha kufanya zaidi ya kutulia kwanza au kushirikisha wazazi wake.
 
kamkomboe mwanao, kuolewa kwa huyo mwanamke hakubadilishi kuwa wewe ndo baba wa mtoto
 
Baba gani wewe? Yani sababu ya kipato ndio inakufanya umkane mtoto wako?Umechanganyikiwa nini sasa?wacha wanaojua majukumu waoe bana,you are not a right candidate for her. Ndio nyie mnakimbiaga familia mambo yakienda kombo.


Mkuu hajamkana ila amesema tuu hajakiri kwa wazazi wa mke kuwa atamuoa mtoto wao na atamchukua na mtoto
Hilo lilikuwa kosa lake
Mkuu mpe ushauri tuu kuwa mambo ndo yamekuwa hayo na amshukuru Mungu kwamba limetokea wakati bado hajakamilisha kile alichotarajia
na kwa upande wmingine huyo mwanamke al;ikuwa na huyo mtu wake mapema tuu kama ni kuzuga alikuwa anam,zuga jamaa kuwa mambo yako sawa wakati huku kashapanga mamo mengine
Amshukuru Mungu wake aendelee na masuala mengine haki ya mtoto wake iko pale pale hata kama huyo mama yake ataolewa na mwanaume mwingine
Na anaweza kuanza taratibu za kumpata mtoto wake iwapo ana uwezo wa kumlea na yeye ajipange kimaisha sasa kupata mke mwingine
 
Usijali wala usichanganyikiwe ni bora ame kwambia ukweli kuliko unge muoa alaf atoke nje!

Kubali matokeo we endelea kupeleka matumizi ya mtoto!
 
Heshimu maamuzi yake, shika hamsini zako.Lipitalo hupishwa kwani mchama ago hanyeli,huenda akauya papo na zaidi ya hapo, mtoto akililia wembe mpe.

Ukilazimisha unaweza kukutana na makubwa, madogo yana nafuu.

Heri nusu shari kuliko shari kamili, na asiyekubali kushindwa si mshindani. Vile vile tafuta mwingine wako kwani kila chombo kwa wimbile, ibilisi wa mtu ni mtu, pia dawa ya moto ni moto na avumaye baharini papa kumbe wengine wapo.Usihofie mwanako kwani kuku havunji yai lake, wala usimtelekeze kwani damu nzito kuliko maji, na juu ya yote mshale kwenda msituni haukupotea.Kumbuka mtupa jongoo hatupi na mti wake na mwana mpe mwanga kulea.

Usiwe na kisebusebu wala kiroho papo kwani kwa kila asemaye mla mla leo mla jana kala nini kuna jeshi la kusema ganda la muwa la jana chungu kaona kivuno.

Mwapiza la nje, hupata la ndani ilhali usije kushangaa mwenda tezi na omo kurejea ngamani na ng'ombe avunjikapo guu hurejea zizini.

Kwa sasa ni hayo tu
 
waeleze wazazi wako na muwaziliane na wazazi wake juu ya mtoto wako maana tayari ameshapata mtu mwingine na tulia utampata aliye chaguo lako maana mke ni mipango ya mola
 
kubali yaishe...ubadhani dar ndio mbeya...wanaume walishakamatia bby huyo na wanampiga raha za mujini bana....mapenzi ya mbali hayapo ndungu zanguni...watu wanapitiwa mbavuni wakiwa wanaishi ndani ya nyumba moja ndio iwe mikoa tofauti.
 
Kwa niaba ya X nashukuru sana kwa ushauri wenu. Mungu awabariki sana. samahani kwa kukaa mbalia na jukwaa tangu jana. Hii ni changamoto tu ya shughuli za maisha.

Namfikishia ushauri huu wa awali ili achanganye na zake kabla ya kuamua nini cha kufanya.

Thanks all. Thanks JF.
 
Salama wakuu. Habari za jioni na poleni sana na majukumu ya ujenzi wa taifa? Natumai mu wazima. Niko karibu na kijana mmoja hapa anahitaji ushauri juu ya shida iliyomkuta ndani wiki mbili zilizopita. Hebu nivae koti lake na kuwaeleza kilichomsibu.

Naitwa X naishi na kufanya kazi mkoani Mbeya. Nina mchumba wangu aitwaye Y mabaye tulianza urafiki tangu mwaka 2009 ambaye kwa sasa anaishi Dar. kutokana na sababu ambazo wote hatukuzielewa mapema tulijikuta tuna mtoto mmoja amabaye sasa ana anakaribia kufunga mwaka wa pili. Tumeendelea kushirikiana kumlea huyo mtoto hadi leo na tumeendelea kupendana na kuheshimiana kama kawaida japo kuna mambo madodo madogo ambayo yalitufanya tugombane lakini tuliyaongea yakaisha.

Kutokana na hali ya kipato kuwa duni nimechelewa kukiri mbele ya wazazi wake kuwa mtoto ni wangu na kwamba mama yake(yaani mchumba wangu) nitamwoa, Japo wazazi wake wote wananifahamu na nahusiana nao vizuri lakini nilikuwa sijafanya ile mila.

Mara chache nimejaribu kufanya hivyo lakini nilishindwa kwa sababu ya kipato.(mimi ni fundi seremala) Miezi michache iliyopita nimejikusanya na kujikaba kila kona ili niweze kutimiza mila na hatimaye niweze kukabidhiwa mke na mtoto. Wazazi wangu wote wawili na wazazi wake wanajua juu ya maandalizi haya na kwa upande wa wazazi wangu, wameshajiandaa kwenda dar kutekeleza hili jambo. Mawasiliano yameenda vizuri lakini wiki mbili zilizopita mchumba wangu Y amesema tusitishe hii safari, unless kama naenda tu kuona mtoto wake, ila kwa upande wake yeye tayaria na mtu mwingine.

Sasa nimechanganyikiwa. nadhani hii imekuwa ghafla kwangu.

Naomba ushauri wenu, nifanyeje?
Hela ya kumuoa unadunduliza .nani Anataka kuolewa na mdunduliza.Get rich fast trust me money matters.mimi nilikuwa sidate mwanaume maskini.na nimeolewa na very wealth men.
 
baba gani wewe? Yani sababu ya kipato ndio inakufanya umkane mtoto wako?umechanganyikiwa nini sasa?wacha wanaojua majukumu waoe bana,you are not a right candidate for her.



kabisa
dada kampata muungwana anaekutunzia had mwanao unaleta tambo??
Punguza basi hashuo,,omba mungu utapata chaguo lako
ila ndio ujifunze sasa,kumjali mtoto sio lazma uwe na kipato,wangapi wanaish maisha ya labda vijijin lakini wana familia zao?
Tulia endelea kuranda mbao mkono uende kinywani nduguu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom