Mpita Njia
JF-Expert Member
- Mar 3, 2008
- 6,997
- 1,163
That is you, the Pasco I know, mature as ever. Kudos
kumbe watu huwa hawasomi, wanatoa comments kwa kuangalia vichwa vya habari. Huyu jamaa hajaomba msamaha!
Mkuu sana Mhe. Regia Mtema,
Heshima mbele!.
Kwanza samahani kuchelewa kuomba radhi, nilikuwa nasubiri ile hansard uliyoahidi, ili nijiridhishe, nilimwelewa vibaya Mhe. Mbowe.
Baada ya kusoma michango mingi humu kuhusu hoja hii, nimeona sina sababu ya kuendelea kuisubiria hansard, hivyo ninatumia fursa hii kwa kusema yafuatayo,
Mimi Pasco wa JF, "Nawaomba Radhi CHADEMA, Nilimwelewa Vibaya Mhe. Mbowe".
Nawaomba radhi kwa dhati, wale wote waliofedheheshwa na uelewa wangu.
Kwa vile sisi ni binadamu na tumeumbwa tofauti, hivyo tofauti za uelewa kati ya mtu na mtu ni kawaida, hakuna binadamu mkamilifu, kufanya makosa ni jambo la kawaida na kuombana misamaha pale mnapotofautiana pia ni kawaida, hivyo sanahani sana.
Msamaha huu nimeufungulia thread inayojitegemea, ili niweke na chanzo cha uelewa wangu huo uliopelekea kumwelewa vibaya Mhe. Mbowe hivyo kutoa fursa kwa Chadema, kutuelewesha vizuri kusije jitokeza mikanganyiko kama hii kwa siku za usoni.
Utangulizi
Baada ya kumalizika Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani, Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema, kilitangazwa kutokuridhishwa kwake na jinsi zoezi zima la uchaguzi lilivyoendeshwa, hivyo wakakataa kuyakubali matokeo ya kura za urais na kutangaza rasmi kutomtambua mshindi.
Binafsi sikukubaliana na msimamo wa Chadema na niliandika humu jamvini kwanini sikukubaliana nao. Tangu mwanzo wa mchezo, Chadema wakijua wazi, the playing ground is not level, lakini walikubali kuingia uwanjani na kupambana hivyo hivyo, huku mmoja ameshika mpini, ungetegemea nini?.
Chadema walikubali kutia saini kanuni za mchezo, hivyo sio busara kuja kukiuka kanuni hizo kwa kukataa matokeo, ndio maana kwa maoni yangu nilisema, the right forum kwa Chadema, kuyakataa matokeo, ni kufika siku yanatangazwa, kususa kusaini na kuwaeleza Watanzania sababu, ikiwemo kutomtabua rais, unamweleza pale pale in front of his face, na jamii yote ya kimataifa.
Kwa kutomtambua rais, Chadema walitoka nje siku ile rais akilihutubia Bunge.
Kilichotokea
Ulipowadia wakati wa kuchangia hotuba ya rais, waliosusa kuisikiliza, nilitegemea Chadema, wangenyamaza kimya, kuonyesha kuendelea kumsusia rais, au wangechangia bila kumtaja ili kuonye kutomtambua.
Kitendo cha Mwenyekiti wa Chadema, kusimama, akaanza kumsifu na kumshukuru na kumpongeza rais Kikwete, mimi nilichanganyikiwa na kuhamanika kwa furaha nikiamini sasa Chadema wanamtambua rais Kikwete ndipo nikapost thread hii
https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...li-yaishe-yamtambua-rais-yampongeza-rais.html
Kwenye thread yangu hiyo, chini niliweka angalizo hili
Angalizo!.
Kuna kitu kinaitwa expressly na impliedly!
Expressly ni kwa Mbowe kutangaza kwamba sasa Chadema inamtambua Rais!
Impliedly ni pale Mbowe alipompongeza rais, akamsifu na kumshukuru na kuonyesha spirit ya reconciliation.
mkubali msikubali, Chadema imemtambua Rais JK impliedly na wamekubali yaishe zaidi ya hapo ni ubishi tuu, vinginevyo Mhe. Mbowe afanye Press Conference afafanue na kukazia kutomtambua JK!
Pamoja na angalizo hilo, haikusaidia watu kunielewa ni mpaka Mbunge wa Chadema, Mhe. Regia Mtema aliponitaka kuomba msamaha kupitia thread hii
https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...i-chadema-umemwelewa-vibaya-hon-mbowe-14.html
Hitimisho
Mwanzo niliamini kwa vile Chadema, walitamka expressly kuwa hawamtambua JK, kubadilika na kutamkata tena expressly kuwa sasa wanamtambua itakuwa ni kugeuka nyuma na kugeuka jiwe la chumvi, hivyo niliamini wamechukua njia ya ustaarabu zaidi kwa kutosema expressly wamemtambua, bali impliedly kuonyesha kumtambua kwa kauli na matendo na hili ndilo kosa langu, nakubali kosa na naomba msamaha wa dhati.
Natumaini msamaha wangu emeeleweka japo sio lazima ukubalike, tuendelee kuchambua hoja mbalimbali humu jamvini kwa maslahi ya taifa.
Natanguliza shukrani.
Wenu
Pasco.
Angalizo: Pasco wa JF siyo mwanachama wala mshabiki wa chama chochote cha siasa, ila ni mkereketwa wa demokrasia ya kweli ndani ya Bunge. Principle ya uchangiaji wangu ni kuongea nothing but the truth kwa kuzingatia truthfulness, accuracy, objectivity, impartiality, fairness, na balance nikiweka mbele maslahi ya taifa.
mbowe anamtambua jk kama rais wa jmt, ila dr.slaa yeye hamtambui jk kama rais wa jmt. Matendo na kauli za hawa viongozi 2 wakuu wa cdm yanadhihirisha wazi kukinzana kwao, mkubali au mkatae ukweli unauma japo mambo yako wazi tena sana, peupe hadharani! Natoa changamoto kwa mbowe na dr.slaa, kama wanabisha jambo hili basi waitishe pc kwa pamoja, na watoe kauli yao kuthibitishia umma wa tz msimamo wao wa kutomtambua jk kama rais wa jmt.
Hahaha .....Pasco wenye kuelewa wameelewa. Kwa hii post yako huna ulipoomba radhi.
Sijui watu tunabishana kitu gani hapa jamvini.
Maana ya alama za kufungua na kufunga usemi kwenye kichwa cha habari cha mwerevu Pasco zinaonesha kuwa Pasco ameomba radhi ila hiyo ni kama taarifa amabyo jamvi hili linafahamishwa na mtu mwingine ambaye siye Pasco kuhusu kuomba radhi huko kwa Pasco. Ili kujua kama hajaomba radhi Pasco anatakiwa akanushe taarifa hizo hapo juu, kwani kwa jinsi ilivyoandikwa hapo inamaanisha kuwa mtu mwingine ameomba msamaha kwa niaba ya Pasco. Ikibaki hivyo hivyo ni kuwa PASCO AMEOMBA RADHI kwisha.
Yani rais aliyewekwa kisheria lakini si halali?Byendagwero said:Chadema imetamka mara nyingi ya kwamba wanamtambua JK kama rais aliyewekwa kwa mujibu wa sheria, ingawaje wanaamini hakuwekwa kiharari
content ya hii sredi haioneshi kuwa unaomba msamaha bali unazidi kung'ang'aniza lilelile. Naona umeanzisha hii sredi kujaribu kutushawishi kivingine tuamin jambo ambalo halikufanywa na mbowe. Hulazimishwi kuomba bali tulijaribu kukuelekeza umeelewa ila unagoma kuridhia.