Eiyer
JF-Expert Member
- Apr 17, 2011
- 28,258
- 20,709
Ni karibu wiki tatu zimebakia ifike ile tarehe ambayo watu huambiwa waoneshane upendo(hata kama mlikua mnavurugu inabidi muache siku hiyo)Najua siku hiyo watu hujiandaa kwa mambo mengi,ila jamani siku hiyo nyumba ndogo zimekuwa zikifurahia zaidi kuliko nyumba kubwa,nawakumbusha bado mapema,jitahidini siku hiyo jitahidini mjiandae mapema mburudike na familia zenu kwa mliooa,na wale wenye wapenzi waandaeni vyema mapema msitafute watu wapya wa kutoka nao siku hiyo,Na zaidi dumisheni upendo KILA SIKU.Kwa wale ambao hamjaoa wala hamna wapenzi kama mimi,kuweni makini nyakati hizi,wengi wanatafuta kampani na kuwezeshwa kimatumizi siku hiyo!Zaidi nawatakieni mahusiano/ndoa imara na upendo kila siku,ifanyeni siku ya WAPENDANAO kama changamoto ya kupima uhusiano/ndoa yenu ili iwe bora zaidi kila panapokucha! KILA IITWAPO LEO NA MZIDI KUPENDANA ZAIDI!......