Nawajua wanaosaidia kukwepa kodi TRA - Kikwete

Mnataka iweje? ukikosowa utoe na ushauri kifanyike nini?

Tuwe waa kweli kidogo. ni Raisi gani aliyeshughulikia ufisadi Tanzania zaidi ya Kikwete? na bado anaendelea kazi yake haijesha, lakini tukubali kuwa Kikwete sio Dikteta na anafanya kazi zake kufata sheria, sasa nyinyi mlitaka akamate hovyo, aweke ndani hovyo, kama alivyofanya yule mmasai? enzi za Nyerere? au ule ndio mnaona utawala bora? wa kusweka watu ndani hovyo?

Yapo mambo ya kushabikia hili la kumshabikia Rais aliyeshindwa siyo jambo la kuchekelea kabisa ,haina tofauti na Shujaa aliyejisifia hadharani huku adui akimkaribia anatimua mbio na kudai ameshinda kwa makelele mengi bila mpango. Hebu mkumbuke Kemikali Ali wa Iraq.Huku tunaita kutapatapa.

Rais hapaswi kutoa habari zisizochujwa, kwani yeye kama kiongozi wa watu kauli yake ni ya mwisho, siyo ya kupapasapapasa umbeya umbeya. Alipaswa kumwita Mkuu wa TRA na kumwambia orodha hii hapa TIMUA WATU HAWA! Kama uchunguzi haujakamilika Kiongozi kaa yeye hapaswi kuzungumzia habari za kijiweni kwa wananchi.

Kwanza kajulishwa na washikaji tuu, not official statement. Sasa utawala wa sheria ni kuongoza nchi kwa majungu tuu na kuvizia vizia ofisi za watu? Atavizia ofisi ngapi kwa mtindo huo? Basi hata kule mipakani kuna matatizo aende basi,Kasumulu, Nandonde, Kyaka, Rongai na Namanga kwa staili hiyo hiyo.

Nchi ina sheria na taatibu za kaz kuna mfumo wa ufuatiliaji utendaji na kutoa taarifa. Iweje leo President ni M&E Officer wa serikali?
 

Rais Jakaya Kikwete amesema ana orodha ya wafanyakazi wa Mamlaka ya Mapato Nchini (TRA) wasio waaminifu ambao wanashirikiana na wafanyabiashara kukwepa kodi kwenye Bandari ya Dar es Salaam.

Alisema anaifanyia kazi orodha hiyo na akishamalizana nayo atamkabidhi Kamishna Mkuu wa TRA, Harry Kitilya, ili achunguze na kuwafukuza kazi wafanyakazi watakaothibitika kujihusisha na vitendo hivyo.

...'delegation' nyingine bana, halafu sio wakabidhiwe kwa TAKUKURU, au kupelekwa mahakamani?
 
Duniani ni tanzania pekee ambapo mwizi ,mlarushwa ,muuja Raisi wa nchi aliyeaapa kuongoza kuulinda katiba na kuwa mfano wa jamii anaweza akawa anawajua wezi,wauaji na bado ukakutana nao mtaani.
Kama raisi anawajua wahalifu asiwachukulie hatua wala kuwataka waandamizi wao wafanye kazi zao unategemea nini kitatokea kwa wale wa ngazi za chini.

Swala la raisi kusema anawajua wala rushwa pale bandari na kusema atamwomba mkurugezi wao awafukuze kazi mda utakapowadia kweli inashtusha.

Raisi wa nchi mwenye kujua wala rushwa halafu bado wanapata mshahara wa wanyonge. hii inasikitisha.

Ndio maana pamoja nakuambiwa na sfo kuwa chenge ni mwizi na dr idrisa bado wanakula fedha zetu kwa utumishi wa umma.

wananchi sasa wakati umefika kumchukulia raisi wetu hatua za makusudi kumwajibisha na kumfungulia mashtaka ya uzembe kazini na kulisababishia taifa hasara kubwa kuanzia ya wizi wa kodi za bandari na ule wa rada na wowote unaohusiana na majalada aliyoyakalia na kulinda wahusika.
jadili
 
Duniani ni tanzania pekee ambapo mwizi ,mlarushwa ,muuja Raisi wa nchi aliyeaapa kuongoza kuulinda katiba na kuwa mfano wa jamii anaweza akawa anawajua wezi,wauaji na bado ukakutana nao mtaani.
Kama raisi anawajua wahalifu asiwachukulie hatua wala kuwataka waandamizi wao wafanye kazi zao unategemea nini kitatokea kwa wale wa ngazi za chini.

Swala la raisi kusema anawajua wala rushwa pale bandari na kusema atamwomba mkurugezi wao awafukuze kazi mda utakapowadia kweli inashtusha.

Raisi wa nchi mwenye kujua wala rushwa halafu bado wanapata mshahara wa wanyonge. hii inasikitisha.

Ndio maana pamoja nakuambiwa na sfo kuwa chenge ni mwizi na dr idrisa bado wanakula fedha zetu kwa utumishi wa umma.

wananchi sasa wakati umefika kumchukulia raisi wetu hatua za makusudi kumwajibisha na kumfungulia mashtaka ya uzembe kazini na kulisababishia taifa hasara kubwa kuanzia ya wizi wa kodi za bandari na ule wa rada na wowote unaohusiana na majalada aliyoyakalia na kulinda wahusika.
jadili


Ni kweli hatuna RAISI, Maneno yake ukiyasikia wakati mwingine, ama unahisi kichefuchefu, ama unatapika kabisa(Huo ndio ukweli wenyewe).
 
You are correct... Kikwete should be charged with withholding evidence :)

Seriously though i agree this is completely ridiculous.
 
Matatizo Bandarini, ATCL, TANESCO, Kiwira, Vitambulisho vya uraia, TRL. Hao waliofunguliwa kesi kama angeona kuna umuhimu wa kuzishughulikia kesi hizo haraka basi angeweza kabisa kuamuru kesi hizo ziendeshwe kwa siku tano kwa wiki au hata zaidi ili zimalizike mapema lakini zinapigwa kalenda tu na mwishotutaanbiwa hakuna ushahidi wa kutosha watuhumiwa wote wako huru.

Nahapo ndio kodi zetu wadanganyika zitakuwa zimetumika bure.Na itakuwa dili kwa hao jamaa watafungua kesi za madai tutakamuliwa kodi zetu mpaka.Sometimes huwa nashawishika kwamba labda hawa jamaa(Mafisadi wote) si raia wa Tanzania ni wageni toka nji jirani za Congo,Rwanda etc.kwa sabubu jamaa hawana uchungu wala uzalendo,wanakamua tu.
 
Grrrrrrr.. wakati mwingine hujisikia kama napasuka vile

Hivi mkuu wangu JK huko kuwajua kwako hao wanao kwepesha kodi na si hao tu kuanzia wauza madawa, mafisadi, viongozi wazembe na hata wale wanao ambukiza wenzao virusi kwa makusudi kuna isaidia nini jamii inayo lala gizani kwa kukosa 200 ya kununua kibaba cha mafuta ya taa??

JK, kama hizo orodha unazijua, na huna ubavu wa kuzifanyia kazi bora unyamaze milele na ufe na siri zako moyoni zamu yako ikifika, kuliko kuja kututambishia unawajua, unawajua, unawajua ili hali huna ubavu wa kuwagusa! Tumechoka na nawajua zako...
 
hii kweli ni porojo, sasa mkuu wa TRA ndio atachagua nani afukuzwe nani ajiteteee nani asaidiwe na ma supervisor kujitetea kabla ya kuchukuliwa hatua, na watakaofukuzwa ni ma whistlblower watakaoshughulikiwa. natoa pole kwa wale wa sio na connection za kusaidiwa

nimefikiria kitu....

JE TRA INAREKODI MAONGEZI YA SIMU? MAANA HII INAWEZA KUWA MOJA YA JK KUJIAMINI KUSEMA MANENO HAYO

Wafanyakazi tafuteni na lawyer
 
Nchi haiongozi na Kangoroo court. Hata kama rais anajua watu itabidi vyombo vya mamlaka husika zichukue sheria.
 
`Ninayo orodha ndefu na nitaikabidhi kwa Kamishna Mkuu wa TRA, Kitilya ili awafuatilie na ahakikishe anawatimua kazi mara moja wale watakaobainika wanahusika na mchezo huo ili tuanze upya,`` alisema.

Naona JK amekumbuka mtizamo wake 1995. Hata hivyo tunapaswa kuanza upya katika ngazi ya siasa na uongozi kitaifa ili hawa wengine walazimike kufuata mkondo chanya.

Vilevile tutaanza upya pale tu rais wa nchia atakapoamua kuchagua kati ya Tanzania na CCM na sio vyote viwili..

omarilyas
 
Msihofu, kamishna mkuu bado anashughulikia ile orodha aliyokabidhiwa, final touches, watafukuzwa mwezi ujao!! :tape:
 
Tusikate tamaa.tumpe nafasi ila ajue,porojo zake zitamponza.
Alisema ana orodha ya majina ya wanaohusika na madawa ya kulevya na kuahidi kuitoa hadharani,mpaka leo kimya.
Leo anayo majina ya bandarini!alienda kufuata nini kama anajua kwamba hao wakwepa ushuru na wababaisha bado wapo hapo?Si angeagiza waondolewe halafu akaangalie ufanisi baada ya wazembe na wakwepa ushuru kuondoka.au
ame watahadharisha kama alivyo fanya kwa wala rushwa wakati akiandaa 'script' Igizo linaloendelea sasa?

Umeangalia tarehe ya kauli yake hii? Ni miaka miwili sasa. Tumpe nafasi gani na ya nini?
 
Duniani ni tanzania pekee ambapo mwizi ,mlarushwa ,muuja Raisi wa nchi aliyeaapa kuongoza kuulinda katiba na kuwa mfano wa jamii anaweza akawa anawajua wezi,wauaji na bado ukakutana nao mtaani.
Kama raisi anawajua wahalifu asiwachukulie hatua wala kuwataka waandamizi wao wafanye kazi zao unategemea nini kitatokea kwa wale wa ngazi za chini.

Swala la raisi kusema anawajua wala rushwa pale bandari na kusema atamwomba mkurugezi wao awafukuze kazi mda utakapowadia kweli inashtusha.

Raisi wa nchi mwenye kujua wala rushwa halafu bado wanapata mshahara wa wanyonge. hii inasikitisha.

Ndio maana pamoja nakuambiwa na sfo kuwa chenge ni mwizi na dr idrisa bado wanakula fedha zetu kwa utumishi wa umma.

wananchi sasa wakati umefika kumchukulia raisi wetu hatua za makusudi kumwajibisha na kumfungulia mashtaka ya uzembe kazini na kulisababishia taifa hasara kubwa kuanzia ya wizi wa kodi za bandari na ule wa rada na wowote unaohusiana na majalada aliyoyakalia na kulinda wahusika.
jadili

Usishangae kwa sababu aliapa kutetea kariba feki, kwa hivyo kila anachokifanya ni feki feki tu.
 
Zakumi unazungumzia kangaroo court na utawala wa sheria? Labda ungeongezea na haki za binadamu! NIONAVYO mimi utetezi wa style hii kwa mambo nyeti kama RUSHWA, UHUJUMU UCHUMI na kuwafanya watoto wetu ndondocha kwa MADAWA YA KULEVYA ni kukosa uzalendo na political will ya kuchukua hatua. Ukiona kiongozi mkuu wa nchi anampa amnesty mwizi wa mali ya umma - kuwa 'rudisha basi yaishe, sitakutaja wala sitakushitaki' hii ni laana na kejeli kwa wadhifa wa mkuu wa nchi. Napenda anavyojinasibu Rais Kagame kwa kusema " I am proud to be a President that has Zero tolerance on Corruption" haya ni maneno yanayoonesha political will kupambana na rushwa.
 
Tuna Rais wa ajabu aneyejua waarifu wote lakini hachukui hatua hii inamaana gani?INATUFANYA TUAMINI YA KUA KATIKA MAJINA HAYO NAE NI MIONGONI MUNGU IBARIKI TANZANIA.
....majina, majina, majina, orodha, orodha, orodha, ahadi ya kuwashughulikia, ahadi ya kuwashughulikia....Surely we have heard all this before?? Time someone ACTED!!!!!
 
mheshimiwa bado hajapata kikombe cha babu? Msaidieni labda anachokisema hakijui ama hajui kutekeleza mamlaka yake kama mkuu wa nchi, inanishangaza sana anaposema orodha anayo atamkabidhi Kitilya aifanyie kazi, yeye kama mkuu wa nchi kwa nini asiwawajibishe mara moja? ama ndio tuseme anawapa nafasi ya mwisho kulitia Taifa hasara kabla hatua hazijachukuliwa?
 
Back
Top Bottom