Navumilia kuwa Mtanzania

BIN BOR

JF-Expert Member
Nov 23, 2010
1,013
407
Zamani nilijivunia kuwa Mtanzania, lakini sasa navumilia kuwa Mtanzania. Kila kukicha, aheri ya jana. Mkombozi wa taifa hili atatoka wapi? Yuko wapi mkombozi.....aliye tayari kusulubiwa kwa ajili ya ukombozi wa watu wake? Wadhalimu wanatamalaki kuanzia ikulu hadi Nangulukulu. Hadi lini tutashindwa kupumua kutokana na kubanwa na viongozi waovu wa taifa hili? Kitabu kitukufu cha nchi hii (katiba) badala ya kuwa safi sasa ni fifi. Ile nyumba takatifu (ikulu) imegeuzwa danguro. Watu matajiri huenda huko kujiburudisha. Mitume (mawaziri) pamoja na bwana wao (mkuu) wamedhamiria kuwa wezi na wanyang'anyi. Nchi imegeuka kama pori la wanyama. Tunaokula nyasi tunaliwa na walao nyama. Hadi lini? Nitashika silaha na kuukabiri uovu huu. Udogo wangu si hoja. Daudi alimuua Goliath kwa kombeo tu. Kila mtu basi na ashike kombeo lake, tupambane na udhalimu huu. Hadi tutakapofanikiwa, nitaendelea kuvumilia kuwa Mtanzania.
 
Back
Top Bottom