Ndugu wana jf nina tatizo la visigino, nikisimama kwa mda mrefu vinaniuma sana. Lakini nikiwa natembea hata km ni safari ndefu haviumi shida ni pale tu ninaposimama mda mrefu. Naombeni ushauri kwani ni mwaka wa 3 sasa naumwa. Asanteni.
duuh Hii nayo!Anza mazoezi ya kusimamia kucha au vidole, unatumia njia mbadala
Dawa ni nyingi kwa kweli lakini Inshallah nitaziandika hizi 4 ambazo ni common tu:
(1) Pika kuzu-bara kwa lugha ya kiingereza inaitwa (coriander) pamoja na hinna na sikikwa kiingereza inaitwa (Vinegar)pamoja na unga wa shairi ni (unga wa ngano)kisha uweke au upake pale penye maumivu.
(2) Ukipika sarjal kwa lugha ya kiingereza inaitwa (quince) pamoja na maji ya shairi (ngano) ikisha upake panopo uma hupoza maumivu.
(3) Asali safi ya nyuki ukinywa pamoja na mafuta ya habbati Sauda kwa kiingereza inaitwa (Nigella Sativa oil) huondosha maumivu ya viungo.
(4) Ukisaga kuzu-bara Kwa kiingereza inaitwa (Coariander) au maji yake pamoja na maji ya busanji kwa kiingereza inaitwa (violet) na lozi kwa kiingereza inaitwa (Almond ) kisha paka katika viungo vinavyouma. Inshallah maumivu yataondoka.
Wewe Nenda katika Maduka ya Kariakoo Mtaa wa pemba kwenye Maduka ya madawa za kiarabu,au kama una jirani yako muarabu muulize atakufahamisha wapi inapatikana mimi sipo bongo miaka mingi tena ningelikuwepo ningeweza kukusaidia wapi inapatikana.Nashukuru sana Mzizi Mkavu kwa ushauri wako mzuri. Naomba kujua hiz dawa nitazipataje? Zinauzwa dukani? Asante mkuu.