Ibrah
JF-Expert Member
- Mar 22, 2007
- 2,729
- 528
Mimi si mwanachama wa chama chochote cha siasa lakini ni mfuatiliaji wa masuala ya siasa na ni mwanademokrasia na ni muumini katika haki na usawa na napenda kuona wanasiasa na vyama vyotevya siasa vinatendewa haki katika masuala ya siasa.
Kifo cha Mpambanaji Wangwe aliyekuwa Mbunge wa Tarime kiligubikwa na utata mkubwa sana huku Wanasiasa wa vyama vyote wakishutumiana kuhusiana na kifo hicho kwa minajili ya kujijenga kisiasa na kukitumia kifo hicho kujijenga kisasa huko Tarime kama tunavyosikia yanayoendelea huko Tarime kwenye kampeni kwenye Jimbo hilo.
Vyombo vya Habari vimekuwa vikitoa mchango mkubwa katika kutujuza yaliyotokea wakati wa kipindi cha msiba wa Wangwe na chombo cha TBC1 hakikuwa nyuma maana walipeleka timu yao huko Kimokorere kwenye msiba na ingawa TBC Radio (pamoja na baadhi ya magazeti) ili-ripoti mambo yaliyokuwa yakitokea huko kwa namna ambayo haikukifurahisha CHADEMA maana taarifa za chombo hicho cha umma zilioneka kutokuwa fair na CHADEMA na baadhi ya wadau mimi miongoni mwao nilishangazwa na jinsi TBC Radi walivyokuwa wakiripoti mambo yaliyokuwa yakijiri huko na kupelekea CHADEMA kuwasilisha malalamiko katika Jukwaa la Wahariri wakida baadhi ya magazeti yaliripoti habari za matukio ya Tarime kwa kupotosha na kwa kuichimba CHADEMA na hatimaye JUkwaa la Wahariri kuunda tume kuchunguza tuhuma hizo za CHADEMA.
Baada ya Kampeni za Uchaguzi wa Ubunge na udiwani kuanza huko Tarime vyombo karibu vyote vya habari viliendelea kutupasha juu ya mambo yanayojiri katika kampeni hizo ambazo kwa mujibu wa habari hizo Kampeni hizo zimetawaliwa na vurugu kubwa na faulo kubwa kutoka pande zote zinazoshiriki uchaguzi huo.
Mwezi Septemba (baada ya kampeni za uchaguzi kuanza) TBC1 walimkariri Mjane mmojawapo wa Marehemu Wangwe: Mariam Wangwe akiituhumu CHADEMA kuwa imeitelekeza familia ya Marehemu Wangwe na hakikushiriki kwenye Arobaini ya Marehemu na akimtaka Spika Sitta kuunda tume ya BUNGE kuchunguza mazingira ya kifo cha Wangwe.
Siku chache baada ya taarifa hiyo, TBC1 tena wakawakariri baadhi ya viongozi wa CHADEMA Mkoa wa Dar es salaam wakikituhumu chama chao na kuhusiana na kifo cha Wangwe! TBC1 kwa makusudi au kwa kutokujua kuwa CHADEMA hawana kitu kinachoiutwa Mkoa wa Dar es Salaam katika safu yao ya Uongozi wakaipa umuhimu mkubwa taarifa hiyo, wakiiweka kando kauli mbiu yao nzuri ya TBC1 "Ukweli na Uwazi".
Nachokiona mimi ni kuwa TBC1 ama ina bifu na CHADEMA au inawapotosha kwa makusudi kabisa Watanzania kwa kujaribu kuwaambia Watanzania kuwa CHADEMA si chama makini hapa nchini; TBC 1 imekubali kutumiwa na baadhi ya wanasiasa kwa manufaa ya wanasiasa hao ili kukipaka matope CHADEMA kwa manufaa ya watu au kikundi hicho. TBC1 ni vema wakumbuke kuwa wao ni chombo cha Umma kinachoendeshwa kwa kodi za Watanzania wote wa vyama vyote vya siasa na ya kuwa wanapaswa kuvitendea haki vyama vyote vya siasa maana hakuna chama kilicho bora cha siasa vyote viko sawa. TBC1 ni kama vile hatuambii chochote kuhusu Kampeni za Uchaguzi Tarime badala yake wanatafuta na kuzipa uzito habari zinazoiumiza CHADEMA tu!
Badala yake nashauri TBC1 waige kutoka ITV ambacho kimuundo kingeweza kabisa kuwa biased kwa kufuata mapenzi ya mmliki wake ambaye ni mtu binafsi lakini kwa kutambua nafasi ya vyombo vya habari katika kuuelimisha umma kinatujuza habari za Kampeni za Tarime kwa umakini mkubwa kwa kutoa habari ambazo ziko fair kwa vyama vyote.
TBC1 kama wanashindwa kutoa habari zilizo fair kwa vyama vyote ni heri wakae kimya kabisa kuliko kucheza mchezo ambao sisi Watanzania tutakuja kuwahukumu iwapo habari wanazotoa ambazo kwa kiasi kikubwa ziko biased zitapokuja kuwa sehemu ya vurugu zinazotokea au zitazotokea kati ya Wanachama wa CHADEMA na Watawala.
Kwa kuwa habari walizotoa TBC1 kweye taarifa zao mwezi Septemba zililenga kuikandamiza CHADEMA kwa faida ya Vyama vingine vya Siasa vinavyoshiriki Uchaguzi wa Tarime kwa makusudi au kwa bahati mbaya (isingekuwa bahati mbaya kama TBC1 wangefanya utafiti wa tuhuma hizo kabla ya kuzirusha na kujua malengo ya wanaoituhumu CHADEMA kwa kuzingatia kuwa hiki ni kipindi cha kampeni za Uchaguzi TaRIME).
TBC1 wangeweza kukaa kimya kabisa kama walivyfanya Jukwaa la Wahariri walioamua kuikalia ripoti yao kuhusu madai ya CHADEMA kwa kuhofia kuwa ripoti hiyo inaweza kutumika na baadhi ya vyama kujipatia umaarufu dhidi ya vyama vingine.
TBC1 Jirekebisheni.
Kifo cha Mpambanaji Wangwe aliyekuwa Mbunge wa Tarime kiligubikwa na utata mkubwa sana huku Wanasiasa wa vyama vyote wakishutumiana kuhusiana na kifo hicho kwa minajili ya kujijenga kisiasa na kukitumia kifo hicho kujijenga kisasa huko Tarime kama tunavyosikia yanayoendelea huko Tarime kwenye kampeni kwenye Jimbo hilo.
Vyombo vya Habari vimekuwa vikitoa mchango mkubwa katika kutujuza yaliyotokea wakati wa kipindi cha msiba wa Wangwe na chombo cha TBC1 hakikuwa nyuma maana walipeleka timu yao huko Kimokorere kwenye msiba na ingawa TBC Radio (pamoja na baadhi ya magazeti) ili-ripoti mambo yaliyokuwa yakitokea huko kwa namna ambayo haikukifurahisha CHADEMA maana taarifa za chombo hicho cha umma zilioneka kutokuwa fair na CHADEMA na baadhi ya wadau mimi miongoni mwao nilishangazwa na jinsi TBC Radi walivyokuwa wakiripoti mambo yaliyokuwa yakijiri huko na kupelekea CHADEMA kuwasilisha malalamiko katika Jukwaa la Wahariri wakida baadhi ya magazeti yaliripoti habari za matukio ya Tarime kwa kupotosha na kwa kuichimba CHADEMA na hatimaye JUkwaa la Wahariri kuunda tume kuchunguza tuhuma hizo za CHADEMA.
Baada ya Kampeni za Uchaguzi wa Ubunge na udiwani kuanza huko Tarime vyombo karibu vyote vya habari viliendelea kutupasha juu ya mambo yanayojiri katika kampeni hizo ambazo kwa mujibu wa habari hizo Kampeni hizo zimetawaliwa na vurugu kubwa na faulo kubwa kutoka pande zote zinazoshiriki uchaguzi huo.
Mwezi Septemba (baada ya kampeni za uchaguzi kuanza) TBC1 walimkariri Mjane mmojawapo wa Marehemu Wangwe: Mariam Wangwe akiituhumu CHADEMA kuwa imeitelekeza familia ya Marehemu Wangwe na hakikushiriki kwenye Arobaini ya Marehemu na akimtaka Spika Sitta kuunda tume ya BUNGE kuchunguza mazingira ya kifo cha Wangwe.
Siku chache baada ya taarifa hiyo, TBC1 tena wakawakariri baadhi ya viongozi wa CHADEMA Mkoa wa Dar es salaam wakikituhumu chama chao na kuhusiana na kifo cha Wangwe! TBC1 kwa makusudi au kwa kutokujua kuwa CHADEMA hawana kitu kinachoiutwa Mkoa wa Dar es Salaam katika safu yao ya Uongozi wakaipa umuhimu mkubwa taarifa hiyo, wakiiweka kando kauli mbiu yao nzuri ya TBC1 "Ukweli na Uwazi".
Nachokiona mimi ni kuwa TBC1 ama ina bifu na CHADEMA au inawapotosha kwa makusudi kabisa Watanzania kwa kujaribu kuwaambia Watanzania kuwa CHADEMA si chama makini hapa nchini; TBC 1 imekubali kutumiwa na baadhi ya wanasiasa kwa manufaa ya wanasiasa hao ili kukipaka matope CHADEMA kwa manufaa ya watu au kikundi hicho. TBC1 ni vema wakumbuke kuwa wao ni chombo cha Umma kinachoendeshwa kwa kodi za Watanzania wote wa vyama vyote vya siasa na ya kuwa wanapaswa kuvitendea haki vyama vyote vya siasa maana hakuna chama kilicho bora cha siasa vyote viko sawa. TBC1 ni kama vile hatuambii chochote kuhusu Kampeni za Uchaguzi Tarime badala yake wanatafuta na kuzipa uzito habari zinazoiumiza CHADEMA tu!
Badala yake nashauri TBC1 waige kutoka ITV ambacho kimuundo kingeweza kabisa kuwa biased kwa kufuata mapenzi ya mmliki wake ambaye ni mtu binafsi lakini kwa kutambua nafasi ya vyombo vya habari katika kuuelimisha umma kinatujuza habari za Kampeni za Tarime kwa umakini mkubwa kwa kutoa habari ambazo ziko fair kwa vyama vyote.
TBC1 kama wanashindwa kutoa habari zilizo fair kwa vyama vyote ni heri wakae kimya kabisa kuliko kucheza mchezo ambao sisi Watanzania tutakuja kuwahukumu iwapo habari wanazotoa ambazo kwa kiasi kikubwa ziko biased zitapokuja kuwa sehemu ya vurugu zinazotokea au zitazotokea kati ya Wanachama wa CHADEMA na Watawala.
Kwa kuwa habari walizotoa TBC1 kweye taarifa zao mwezi Septemba zililenga kuikandamiza CHADEMA kwa faida ya Vyama vingine vya Siasa vinavyoshiriki Uchaguzi wa Tarime kwa makusudi au kwa bahati mbaya (isingekuwa bahati mbaya kama TBC1 wangefanya utafiti wa tuhuma hizo kabla ya kuzirusha na kujua malengo ya wanaoituhumu CHADEMA kwa kuzingatia kuwa hiki ni kipindi cha kampeni za Uchaguzi TaRIME).
TBC1 wangeweza kukaa kimya kabisa kama walivyfanya Jukwaa la Wahariri walioamua kuikalia ripoti yao kuhusu madai ya CHADEMA kwa kuhofia kuwa ripoti hiyo inaweza kutumika na baadhi ya vyama kujipatia umaarufu dhidi ya vyama vingine.
TBC1 Jirekebisheni.