Nauliza kwa nini Agakhan Foundation wanapewa misamaha ya kodi

anney

Senior Member
Jul 9, 2010
155
45
Ndugu wanaJF napenda kufahamu kwa nini taasisi ya Agakhan inapewa misamaha ya kodi hapa nchini kwetu. Nina uliza kwa sababu huduma za Agakhan mfano hospital za Agakhan ni ghali kuliko hospitali zote hapa nchini. Mfano mtoto mdogo wa wiki moja ukimpeleka Agakhan ili alazawe lazima uweke deposit ya laki tano za Tanzania ndiyo apewe huduma ya matibabu. Kumwona daktari ni elfu Ths 40,000-70,000. Shule za Agakhan ada zake nazo zipo juu kulinginishwa shule zingine za binafsi. Je kwanini wapate misamaha ya kodi? Je wanastahili kupewa misamaha ya kodi?
 
Unatafuta ugomvi na akina Pengo wewe! ukianzia huko utakuja kuishia kwa nini Serikali inalipa Kanisa mabilioni ya pesa kwa mwaka halafu bado gharama zao ni za juu sana huku wakipewa misamaha ya kodi, na mwisho wa siku faida inayopatikana katika hizo Hospitali inakwenda Kanisani.
Unafikiri akina Pengo watakuachia hivihivi uwatilie kitumbua chao mchanga?
 
Unatafuta ugomvi na akina Pengo wewe! ukianzia huko utakuja kuishia kwa nini Serikali inalipa Kanisa mabilioni ya pesa kwa mwaka halafu bado gharama zao ni za juu sana huku wakipewa misamaha ya kodi, na mwisho wa siku faida inayopatikana katika hizo Hospitali inakwenda Kanisani.
Unafikiri akina Pengo watakuachia hivihivi uwatilie kitumbua chao mchanga?

Mkuu nahisi unakimbia mada. Alichouliza ni uhalali wa kupewa msamaha halafu gharama zao zikawa juu. Nadhani ulipaswa kutaja hospitali gani za hao akina Pengo zenye garama kama au kuliko agakhani ili nazo tuzijadili.
 
Unatafuta ugomvi na akina Pengo wewe! ukianzia huko utakuja kuishia kwa nini Serikali inalipa Kanisa mabilioni ya pesa kwa mwaka halafu bado gharama zao ni za juu sana huku wakipewa misamaha ya kodi, na mwisho wa siku faida inayopatikana katika hizo Hospitali inakwenda Kanisani.
Unafikiri akina Pengo watakuachia hivihivi uwatilie kitumbua chao mchanga?

Ni mjadala mzuri tu,kama umeona hata kanisa lina misamaha lakini gharama ziko juu ni bora ungeongeza idadi ya taasisi za kuhoji uhalali wa misamaha ya kodi wakati zaniajiendesha kibiashara zaidi...
Ni hoja nzuri ijadiliwe kwa uwazi pasipo kuleta jazba za kidini.
Binafsi nashindwa kuelewa un NON-PROFIT ORG wa taasisi za AGHA KHAN,kwa kweli wanachuma sana zaidi ya taasisi zingine za kibiashara,ni wakati kuafaka wa serikali kuweka utaratibu wa namna ya kuhakikisha misamaha ya kodi inawanufaisha watanzania kupitia taasisi zinazopata hiyo misamaha.
 
Side naona unataka kutupotezea
Ili suala ata Mbatia aliuliza kwa bunge last time,regence hawana exemption but wanalipa kodi kubwa tuu na gharama zao ni sawa na agha khan
Ila kwa serikali hii sishangai bse kuna viwanda vinatumia gesi but hawajashusha bei ya bidhaa zao na serikali haifanayi follow up
So the same to this watu wana exemption but hakuna unafuu wa huduma which make the exemption usesless kwa mwananchi wa kawaida
 
Unatafuta ugomvi na akina Pengo wewe! ukianzia huko utakuja kuishia kwa nini Serikali inalipa Kanisa mabilioni ya pesa kwa mwaka halafu bado gharama zao ni za juu sana huku wakipewa misamaha ya kodi, na mwisho wa siku faida inayopatikana katika hizo Hospitali inakwenda Kanisani.
Unafikiri akina Pengo watakuachia hivihivi uwatilie kitumbua chao mchanga?

Hujui unachokisema, Pengo ndo AF, fungua akili yako mkuu. Nachojua RC (na mashirika yao inc. Benedectine) wanamiliki baadhi ya hospital kubwa ikiwemo BMH, Ndanda Mission, Ligula, Peramiho na hizi zote zinatoa huduma kwa bei ya kawaida kabisa na tena zinahudumia jamii kubwa na si matajiri mfano wa AF.

Makanisa mengine yenye hizi Hospital na bado zinatoza huduma za 'kawaida' ni pamoja na AIC Makongoro, na Kolandoto, KCMC, kutaja machache.
Na pia hospital za BAKWATA zinatoa huduma kwa bei ya kawaida na ndiyo maana mtoa mada anahoji inakuwaje AghaKhan hospitals zinatoza gharama kubwa wakati anahisi zinapata msamaha kama hospitali nilizojaribu kuainisha hapo juu.

EID MUBARAK
 
Mkuu nahisi unakimbia mada. Alichouliza ni uhalali wa kupewa msamaha halafu gharama zao zikawa juu. Nadhani ulipaswa kutaja hospitali gani za hao akina Pengo zenye garama kama au kuliko agakhani ili nazo tuzijadili.

Sio mpaka gharama ziwazidi Agakhan hata hospital zingine wanapewa misamaha ya kodi lakini gharama zao zipo juu mfano Bugando Hospital, KCMC Hospital.
 
kuna haja ya kuangalia upya misamaha ya kodi hasa kwa taasisi za kidini, wengi hawaitumii ipasavyo.
Wanafanya biashara badal ya kuhudumia jamii.
 
ni kweli Mbatia aliuliza bungeni lakini hoja yake haikujibiwa.Huduma za Agakhani zimelenga daraja la juu la watanzania hivyo kuwepo kwao hakuwasaidii wananchi wa kawaida ambao ni wengi Tanzania.Hindu mandal wanalipa kodi hizo hospital nyingine unazozungumzia za makanisa huduma zake ni za kawaida na hazibagui watu kwa vigezo vya kipato au dini tuna haki ya kujua nini kinaendelea kuhusu kodi zetu na wapi wanapata kiburi cha kupandisha gharama wakati wana msamaha wa kodi
 
Hujui unachokisema, Pengo ndo AF, fungua akili yako mkuu. Nachojua RC (na mashirika yao inc. Benedectine) wanamiliki baadhi ya hospital kubwa ikiwemo BMH, Ndanda Mission, Ligula, Peramiho na hizi zote zinatoa huduma kwa bei ya kawaida kabisa na tena zinahudumia jamii kubwa na si matajiri mfano wa AF.
Nilikuwa nikifikiria kuwa Kanisa la Pengo lilikuwana mwakilishi wakati wa kusaini ile "MoH" na kwa vile yeye ndiye kinara ndio maana nikamtaja.
Obe said:
Makanisa mengine yenye hizi Hospital na bado zinatoza huduma za 'kawaida' ni pamoja na AIC Makongoro, na Kolandoto, KCMC, kutaja machache.
Na pia hospital za BAKWATA zinatoa huduma kwa bei ya kawaida na ndiyo maana mtoa mada anahoji inakuwaje AghaKhan hospitals zinatoza gharama kubwa wakati anahisi zinapata msamaha kama hospitali nilizojaribu kuainisha hapo juu.
Mkuu! ili kuurahisisha huu mjadala tungeangalia ni kiasi gani cha ruzuku inayopata mahospitali yote ya Kanisa kisha tuioanishe na ruzuku inayopata AghaKhan. Tuangalie pia ruzuku za gharama za ukarabati, elimu kwa wafanyakazi tuoanishe.
Halafu tuangalie gharama za matibabu kati ya hospitali moja ya Aghakhan na KCMC au Bugando tuoanishe, hii nafikiri itakuwa njia rahisi ya kuwa na munakasha wenye tija au unafikiri kuna njia nyingine rahisi zaidi ya hii kuuendesha huu mjadala?
Nakumbuka kuna mchangiaji hapa aliye oanisha gharama za kumtibu mgonjwa wake KCMC na India jibu ikawa India ni rahisi zaidi kuliko KCMC, hii ilimlazimu kumpeleka mgonjwa wake India! huyu ni mlipa kodi ambaye kiasi cha kodi yake kinakwenda kama "ruzuku" KCMC na ameshindwa kumtibu mgonjwa wake pale! Serikali pia inapoteza pale pesa ya huyu mlipa kodi inapokwenda kutumika nje ya nchi badala ya kuuingiza katika mzunguko wa pesa nchini.
Miaka kadhaa iliyopita gharama tu za kujiandikisha Bugando Hospital ilikuwa ni elfu Ishirini!
MoH inabidi ifutwe pesa za ruzuku zirudishwe (mkataba hauna ridhaa ya walipa kodi) wasioweza kurudisha Hospitali zao ziuzwe ili kufidia na Serikali ichukuwe its own responsibility.
 
Alie toa mfano Wa aghakan kidogo ametoa walau pa kuanzia na kusherehesha hoja yake kwa data, anasema kulaza mtoto mdogo walau uanze na deposit tsh. 500,000/=, kumuoana dkr at least uwe na tsh. 40,000 - 70,000.

Na nyie mnaomension kcmc na .... Tupen data msilete majibu ya kisiasa, lengo tujue nan anadanganya nan anasema ukweli, na taasis zipi zinatuibia misamaha ya kod zetu kwa kututoza zaid.

Tuache majibu ya jujuu, kisiasa na yenye mtazamo wa kidin.
 
Sio mpaka gharama ziwazidi Agakhan hata hospital zingine wanapewa misamaha ya kodi lakini gharama zao zipo juu mfano Bugando Hospital, KCMC Hospital.

hivi na wewe kumbe uelewa wako bado ni mdogo. Unaweza ukalinganisha gharama ya huduma zitolewazo na bungano na zile za aghakhan.
 
Alie toa mfano Wa aghakan kidogo ametoa walau pa kuanzia na kusherehesha hoja yake kwa data, anasema kulaza mtoto mdogo walau uanze na deposit tsh. 500,000/=, kumuoana dkr at least uwe na tsh. 40,000 - 70,000.

Na nyie mnaomension kcmc na .... Tupen data msilete majibu ya kisiasa, lengo tujue nan anadanganya nan anasema ukweli, na taasis zipi zinatuibia misamaha ya kod zetu kwa kututoza zaid.

Tuache majibu ya jujuu, kisiasa na yenye mtazamo wa kidin.
Ameshindwa kutuonyesha KCMC au Bugando gharama zao ni kiasi gani!
Tukipata tuangalie idadi ya pesa ambazo KCMC inaingiza kutoka Serikalini (Ruzuku,ukarabati, msamaha wa kodi n.k)na Aghakhan nayo inaingiza kiasi gani ili tujumlishe. simple
 
Dawa ni taasisi za kidini zote zinzofanya biashara zilipe kodi kama ilivyo msumbiji!!Agha Khan wa Bank Diamond Trust,Wana magazeti mwananchi,citizen,wana shule mzizima pia mwingira ana ban efatha,mashamba ya mazao ya biashara!Nadhani mwaka ujao wa fedha waziri atamke juu ya hizi taasisi kulipa kodi
 
kuna watu msipomtaja pengo au katoliki hamwezi kupumua eeeh?


Unatafuta ugomvi na akina Pengo wewe! ukianzia huko utakuja kuishia kwa nini Serikali inalipa Kanisa mabilioni ya pesa kwa mwaka halafu bado gharama zao ni za juu sana huku wakipewa misamaha ya kodi, na mwisho wa siku faida inayopatikana katika hizo Hospitali inakwenda Kanisani.
Unafikiri akina Pengo watakuachia hivihivi uwatilie kitumbua chao mchanga?
 
Sio mpaka gharama ziwazidi Agakhan hata hospital zingine wanapewa misamaha ya kodi lakini gharama zao zipo juu mfano Bugando Hospital, KCMC Hospital.

Sawa...sasa tuseme eg 1- ECG Bugando ni Tsh..... na Aga Khan ni Tsh......, 2-CT SCAN Bugando ni Tsh.... na Aga Khan ni Tsh...., tulinganishe na kupata jibu zuri
 
Nimeupenda huu mjadala wanaJF. Badala ya kuangalia Agakhan, ni vizuri tukaangalia mbali zaidi. Hata katika huduma ya elimu, kwamfano, ada anayolipa mwanafunzi wa Tumaini Dar kwa kozi za kawaida za Arts mwaka mmoja inakaribia ada anayolipa mwanafunzi wa UDSM kwa miaka miwili na nusu. Pia ni zaidi ya ada ya SAUT kwa tabribani 1mn kwa mwaka. Hivi, misamaha hii inafanya kazi gani?
 
Sawa...sasa tuseme eg 1- ECG Bugando ni Tsh..... na Aga Khan ni Tsh......, 2-CT SCAN Bugando ni Tsh.... na Aga Khan ni Tsh...., tulinganishe na kupata jibu zuri
Mkuu lengo ni kupata suluhisho la maana hivyo sioni tabu yoyote ile ikiwa kila kitu kitawekwa mezani ili kitusaidie katika mjadala wetu huu!
 
Unatafuta ugomvi na akina Pengo wewe! ukianzia huko utakuja kuishia kwa nini Serikali inalipa Kanisa mabilioni ya pesa kwa mwaka halafu bado gharama zao ni za juu sana huku wakipewa misamaha ya kodi, na mwisho wa siku faida inayopatikana katika hizo Hospitali inakwenda Kanisani.
Unafikiri akina Pengo watakuachia hivihivi uwatilie kitumbua chao mchanga?
Nyie ndo mnalichafua jamvi nakuonekana kuwa ni la vilaza. Mada umeielewa au umeamua kutumia moyo wako kuchangia badala ya kutumia kichwa?

gharama zao zipo juu mfano Bugando Hospital, KCMC Hospital.

Tupe mchanganuo wa ughari wa huduma zao basi mkuu. Kuongea tuuuu kila mtu anaweza kuongea. Kuthibitisha anachokiongea mtu ndo kutafanya hoja yake kuwa na nguvu!
 
Back
Top Bottom