Nauliza: Hivi ile ban ya Mikusanyiko wakati wa SENSA imeisha saa ngapi?

S2dak_Jr

Senior Member
Jul 15, 2012
198
45
Wanajamvi,


Kumbukumbu yangu ni kuwa mikusanyiko ya watu, ikiwa na ya siasa ilikatazwa kwa sababu ya Sensa.

Hii ikiwa ni pamoja na kukatazwa/kusitishwa kwa kazi zote zilizokuwa zikifanywa na chama cha siasa cha CHADEMA.

Kwa taarifa tu ni kwamba juzi mkusanyiko mkubwa ulifanyika mkoani Tabora kwenye kile kinachoitwa tamasha la Fiesta linaloendeeshwa na Clouds Media.

Pia kuna tetesi kuwa Mh. Mwigulu Nchemba akishirikiana na Nape Nnauye wamefanya Mkutano wa kisiasa Mjini Igunga.

Na pia Mh. Mwigulu alikuwa kwenye mkusanyiko wa kisiasa Kiomboi Iramba ikiambatana na zoezi la uchaguzi wa UVCCM wa wiilaya ya Iramba.

Kama hiyo haitoshi, mpaka muda huu kuna mkusanyiko wa watu unaoendelea mpaka muda huu Mjini Singida kwenye tamasha la Fiesta la Clouds Media na linarushwa moja kwa moja kupitia Clouds Fm tangu mchana wa jana. Na sijajua kibali cha tamasha hili kinaisha muda wake saa ngapi. Kwani mpaka saa saba ya usiku huu tamasha hilo linaendelea Mjini Singida.

Swali: Je katazo la mikusanyiko ni kwa ajili ya watu fulani au CCM na Clouds Media hao wana exemption kwenye hili katazo?

Naomba kuwasilisha.
 
Hili Tangazo/katazo lilikuwa maalum tu kwa CHADEMA kwa vile wao ndo wana historia ya kuvuta watu wengi zaidi kwenye mikutano yao, na uchunguzi wa kipolisi unaonesha wapenzi na wanachama wa CHADEMA huwa wanasafiri kwa pesa zao kwenda umbali mrefu sana tu ili wakasikilize hotuba za makamanda, kwasababu hiyo ilibidi sirikali iwapige ban kwa muda CDM.
 
Wanajamvi,


Kumbukumbu yangu ni kuwa mikusanyiko ya watu, ikiwa na ya siasa ilikatazwa kwa sababu ya Sensa.

Hii ikiwa ni pamoja na kukatazwa/kusitishwa kwa kazi zote zilizokuwa zikifanywa na chama cha siasa cha CHADEMA.

Kwa taarifa tu ni kwamba juzi mkusanyiko mkubwa ulifanyika mkoani Tabora kwenye kile kinachoitwa tamasha la Fiesta linaloendeeshwa na Clouds Media.

Pia kuna tetesi kuwa Mh. Mwigulu Nchemba akishirikiana na Nape Nnauye wamefanya Mkutano wa kisiasa Mjini Igunga.

Na pia Mh. Mwigulu alikuwa kwenye mkusanyiko wa kisiasa Kiomboi Iramba ikiambatana na zoezi la uchaguzi wa UVCCM wa wiilaya ya Iramba.

Kama hiyo haitoshi, mpaka muda huu kuna mkusanyiko wa watu unaoendelea mpaka muda huu Mjini Singida kwenye tamasha la Fiesta la Clouds Media na linarushwa moja kwa moja kupitia Clouds Fm tangu mchana wa jana. Na sijajua kibali cha tamasha hili kinaisha muda wake saa ngapi. Kwani mpaka saa saba ya usiku huu tamasha hilo linaendelea Mjini Singida.

Swali: Je katazo la mikusanyiko ni kwa ajili ya watu fulani au CCM na Clouds Media hao wana exemption kwenye hili katazo?

Naomba kuwasilisha.
mkuu sensa imeisha, au umelewa mbege ndo ukapost huu uzi?
 
Back
Top Bottom