mkomatembo
JF-Expert Member
- Dec 17, 2011
- 1,477
- 815
Salaam wana Jamvi,
Leo kwenye gazeti la Uhuru na Jambo Leo kuna habari inayosema "Mbunge afichua UFISADI Kivukoni. Katika kupitia habari ndani nikaona kuwa kuna bei mpya za kivuko zimeelezwa katika habari hiyo ambayo kwa kweli ni mzigo mkubwa kwa mwananchi wa kawaida na hata yule ambae anamiliki ama gari ya kawaida au gari ya biashara. Bei hizo zilisomeka kama ifuatavyo ukilinganisha kuwa zimepanda kwa asilimia 100 katika kila upande.
Watu wazima Tsh 200
Baiskeli Tsh 300
Bajaj Tsh 1,300
Pikipiki Tsh 500
Gari ndogo ya kawaida Tsh 1,500
Pick up (pia huwekwa katika kundi hili station wagon, gari aina ya LAnd cruiser , n.k) Tsh 2,000
Basi Dogo Tsh 3,500
Magari ta tani mbili na trekta tsh 7,500
Ndugulile ameiambia Uhuru kuwa, kuna ufisadi mkubwa upo pale ikiwemo wafanyakazi wa plae ambao ni wanaokata ticket huchapisha vitabu aina mbili tofauti. Hutumia vitabu vyao hivo feki kukatia ticket watu na matokeo yake pesa nyingi kuishia katika matumbo yao!
Kwa siku wanadai inakusanywa Tsh million 4. tofauti na ilipokusanywa siku alipoingilia katika waziri magufuli na kuweka watu kutoka wizarani ambapo ilikusanywa Tsh Million 13.
Aidha amedai kuwa kuna mchezo mchafu wa kuuza mafuta unaofanywa na wafanyakazi wa kivuko hicho cha kuuza mafuta kwa wenye maboti.
Mbunge amekemea vikali ongezeko hilo na kudai kuwa kwanza serikali idhibiti wizi huu na baadae ifikirie kupandisha nauli huku ikiwashirikisha wakaazi wa Kigamboni.
Source : Uhuru.
Maoni yangu,
Kama serikali iliwahi kuweka watu wake wa wizara na kukusanywa Tsh Mil 13. iweje serikali iwatoe watu hao? ina maana serikali inajua fika kuwa kuna wizi pale kwa sababu wanajua fika habari hizi.
Kuna wakati wakuu hawa wa kivuko walitaka ruzuku kutoka serikalini wakidai kuwa kivuko kimeshindwa kujiendesha kumbe wanajua fika kuwa pesa yote inaishia katika matumbo yao!
NAsikitika kusema haya ni ya kuwatwsha mizigo wananchi kama tunavotaka kutwisha msigo wa kulipa DOWANS kwa Tanesco kupandiha gharama kwa asilimia 155.
KIla mwananchi anawajibika kulipia deni la dowans na ndio maana leo Tanesco imeamua kupandisha gharama zake kwa asilimia 155 ili tukamuliwe wananchi kulipa deni hilo.
Kwa mtindo huo huo wananchi wa Kigamboni wakamuliwe kulipa gharama mara mbili ya sasa hivi, ilhali pesa ile hainedi katika mfuko wa serikali bali inaingia katika matumbo ya watu binafsi NA SERIKALI INAJUA FIKA !
Serikali amkeni msimamie watu wenu !
Leo kwenye gazeti la Uhuru na Jambo Leo kuna habari inayosema "Mbunge afichua UFISADI Kivukoni. Katika kupitia habari ndani nikaona kuwa kuna bei mpya za kivuko zimeelezwa katika habari hiyo ambayo kwa kweli ni mzigo mkubwa kwa mwananchi wa kawaida na hata yule ambae anamiliki ama gari ya kawaida au gari ya biashara. Bei hizo zilisomeka kama ifuatavyo ukilinganisha kuwa zimepanda kwa asilimia 100 katika kila upande.
Watu wazima Tsh 200
Baiskeli Tsh 300
Bajaj Tsh 1,300
Pikipiki Tsh 500
Gari ndogo ya kawaida Tsh 1,500
Pick up (pia huwekwa katika kundi hili station wagon, gari aina ya LAnd cruiser , n.k) Tsh 2,000
Basi Dogo Tsh 3,500
Magari ta tani mbili na trekta tsh 7,500
Ndugulile ameiambia Uhuru kuwa, kuna ufisadi mkubwa upo pale ikiwemo wafanyakazi wa plae ambao ni wanaokata ticket huchapisha vitabu aina mbili tofauti. Hutumia vitabu vyao hivo feki kukatia ticket watu na matokeo yake pesa nyingi kuishia katika matumbo yao!
Kwa siku wanadai inakusanywa Tsh million 4. tofauti na ilipokusanywa siku alipoingilia katika waziri magufuli na kuweka watu kutoka wizarani ambapo ilikusanywa Tsh Million 13.
Aidha amedai kuwa kuna mchezo mchafu wa kuuza mafuta unaofanywa na wafanyakazi wa kivuko hicho cha kuuza mafuta kwa wenye maboti.
Mbunge amekemea vikali ongezeko hilo na kudai kuwa kwanza serikali idhibiti wizi huu na baadae ifikirie kupandisha nauli huku ikiwashirikisha wakaazi wa Kigamboni.
Source : Uhuru.
Maoni yangu,
Kama serikali iliwahi kuweka watu wake wa wizara na kukusanywa Tsh Mil 13. iweje serikali iwatoe watu hao? ina maana serikali inajua fika kuwa kuna wizi pale kwa sababu wanajua fika habari hizi.
Kuna wakati wakuu hawa wa kivuko walitaka ruzuku kutoka serikalini wakidai kuwa kivuko kimeshindwa kujiendesha kumbe wanajua fika kuwa pesa yote inaishia katika matumbo yao!
NAsikitika kusema haya ni ya kuwatwsha mizigo wananchi kama tunavotaka kutwisha msigo wa kulipa DOWANS kwa Tanesco kupandiha gharama kwa asilimia 155.
KIla mwananchi anawajibika kulipia deni la dowans na ndio maana leo Tanesco imeamua kupandisha gharama zake kwa asilimia 155 ili tukamuliwe wananchi kulipa deni hilo.
Kwa mtindo huo huo wananchi wa Kigamboni wakamuliwe kulipa gharama mara mbili ya sasa hivi, ilhali pesa ile hainedi katika mfuko wa serikali bali inaingia katika matumbo ya watu binafsi NA SERIKALI INAJUA FIKA !
Serikali amkeni msimamie watu wenu !