Nauli Feri: Mnyika, Hata Wewe?

Tunazungumzia nauli kupanda kutoka shillingi mia hadi mia mbili, na katika my original post, nimeelezea kwa uwezo wangu wote binafsi naona tatizo lipo wapi. Vinginevyo hakuna anaekataa kwamba wananchi wana hali mbaya, lakini wapo wanaopinga (mimi nikiwa mmoja wapo) vitendo vya baadhi ya viongozi kutumia hali hizo mbaya za wananchi, kisiasa.

Heshima kwako Mchambuzi;
Una mawazo mazuri sana kamanda.
Pamoja na wabunge kutumia matatizo (hali mbaya) ya wananchi kujinufaisha kisiasa; Binafsi nawaunga mkono tamko la wabunge wa dsm kwa sababu moja tu ifuatayo;

  • Taifa letu limeazimisha miaka hamsini ya uhuru, ilitakiwa pale tuwe na daraja na wananchi tuvuke bure (bila kutoa hata tshs. 5), Sitaki kuangalia wala kufahamu mapato na gharama za uendeshaji wa kivuko.
 
Unnecessarily...kamanda mchambuzi huwa nakuheshimu sana. Nakumbuka ile article yako juu ya Baba wa Taifa Nyerere! Leo umechemka. Naona umeinga kwenye mradi wa spinning na propaganda wa Magufuli, kwa kujua ama kutojua. Pole! Juzi nilimsikia mtangazaji mmoja wa Clouds FM (nililazimika kusikiliza coz nilikuwa ndani ya gari ya mtu), akiweka sauti ya Pombe Magufuli, hasa pale aliposema ati anamheshimu sana Mdee kwa sababu ana-concetrate na jimbo lake (hajui kuwa Mdee yuko safarini), akasema ati Mnyika ameshindwa kushughulikia mambo kama ya mabweni UDSM na nauli ya Ubungo Terminal (pia hajui jitihada za Mnyika ndizo zilisababisha nauli isipande kwenda shilingi 300 kama ilivyokuwa imepangwa na sasa hivi kutokana na juhudi hizo, jiji linapitia sheria ndogo ndogo juu ya suala la Ubungo Terminal kucheki utaratibu huo).

Mtangazaji yule (alikuwa Redio One, somebody Ayo sijui), kama ulivyofanya wewe hapa, akamalizia kwa kusema "hiyo ni sauti juu ya Waziri Magufuli akijibu hoja za wabunge wa Dar es Salaam juu msimamo wao wa kupinga ongezeko la nauli ya shilingi 100, akiwemo Mbunge wa Ubungo, John Mnyika." Come one what a crap!

The same to u brother. Hoja yako hii ya kipuuzi kabisa isiyolingana na uwezo wako niliozoea kuuona hapa mara kwa mara! Nimeshindwa kuendelea kusoma mpaka mwisho baada ya kuona kuwa umeingia kwa kiasi kikubwa katika spinning ya Kundi la Pombe Magufuli, ambalo limeamua kuweka msisitizo kuwa kinachopingwa na wote wenye akili timamu eti ni ONGEZEKO LA SH. 100! To hell, hii si hoja kwa watu wenye akili walioona crap ya Magufuli bro. Kuna issues kadhaa za msingi, suala si sh. 100, hata kidogo, ukijadili hivyo ure missin the point at large bro! Nitakueleza baadae kidogo!

Qualify some several conclusions zako, mara unasema serikali inaweka pesa nyingi sana katika kuendesha kivuko hicho!!!!! He kiasi gani hicho bro hebu kiseme! Je kinatosha au hakitoshi kujenga daraja hapo mahali ili tuondokane na bugudha ya watu kulipia mahali ambapo haikusathili kama serikali ingetimiza tu wajibu wake wa kutoa huduma kwa watu kwa kujenga daraja! Kuna vitu kadhaa katika hoja yako nataka nikueleze ili ufikirie upya attack zako kwa Mnyika na wabunge wenzake. Ntakueleza...punde
Mkuu maelezo yako vile vile hayajibu hoja.. Sema spinning iko wapi na ukweli ni upi maana katoa mifano wewe toa yako tuitazame na sio kufanya yale yale unayoyapinga kutoka kwa mchambuzi..
Twambie kwa nini unaona Tsh 200 sio sawa ikiwa hawa wabunge walipitisha ongezeko la nauli wakiwa bungeni..Kwa nini maswali yao yote yanakuja leo hii wakati walikuwa na muda na sehemu muafaka ya kuweka upinzani ktk swala hili..Jaribu kujenga hoja na sii kumzungumzia Mchambuzi hapo nawe unafanya makosa makubwa ya kumchafua mtu.
 
Ingekuwa ni wabunge wa CCM peke yake, pengine nisinge hoji kwani tumewazoea wabunge wengi wa CCM (sio wote), kuja na matamshi ya ajabu ajabu. Mnyika ni mtu makini sana kutumbukia katika sakata lillojaa mantiki kuliko siasa, na hilo ndilo limenigusa zaidi.
Mkuu usizungumzie badiliko la nauli ya binadamu tu, hebu jaribu kuzungumzia nauli ya kuvusha Guta
 
Si kweli kwamba mtu anayetoka kigamboni kuja upande wa pili wa Dar kwa kutumia pantoni analipa shilingi 200 tu. Tukumbuke kwamba wakazi wa kigamboni wanatumia nauli kutoka majumbani mwao ili kufika eneo la feri na wanatumia tena shilingi 200 kuvuka. Hivyo ongezeko hilo la 100 sio tu limeongeza nauli ya msafiri wa kigamboni kuwa 200 bali tunatakiwa kujumlisha pia nauli wanazotumia kutoka majumbani mwao kufika hapo feri kwa ajili ya kuvuka. Hivyo basi kuna ambao walikua wanatumia shilingi 300 kwa siku sasa watalipa 400 na ambao walikuwa wanatumia 400 sasa wanalipa 500. Tusiupotoshe umma kwamba nauli imeongeza kutoka 100 kwenda 200 bali tuangalie nauli kutoka kule wakazi hawa wa kigamboni wanapoishi mpaka kuvuka kwa kutumia hilo pantoni.
 
Heshima kwako Mchambuzi;
Una mawazo mazuri sana kamanda.
Pamoja na wabunge kutumia matatizo (hali mbaya) ya wananchi kujinufaisha kisiasa; Binafsi nawaunga mkono tamko la wabunge wa dsm kwa sababu moja tu ifuatayo;

  • Taifa letu limeazimisha miaka hamsini ya uhuru, ilitakiwa pale tuwe na daraja na wananchi tuvuke bure (bila kutoa hata tshs. 5), Sitaki kuangalia wala kufahamu mapato na gharama za uendeshaji wa kivuko.

Kimsingi nipo na wewe katika hilo. Lakini, iwapo wananchi hawatembei bali kuchukua daladala kutokea feri hadi posta - umbali wa kilomita sio zaidi ya tatu, je unadhani daraja likijengwa, wananchi watatembea kweli kwa kilometa 7 (kama sio zaidi) kutokea kurasini daraja litakapoanzia hadi kibada daraja litakapoteremkia, kisha watembee kwa kilometa nyingine 18 kutokea kibada hadi feri ya upande wa kigamboni? Ni dhahiri watapanda daladala na nauli itaweza karibia sh. 1,000, kwani kilometa 25 ni nyingi sana kwa wenye madala dala.
 
Mkuu Mchambuzi heshima mbele kwa uchambuzi mzuri,

Binafsi naomba niseme nimesikitishwa zaidi na Dr. Ndugulile, kwa vile ni kati ya true Phd (za kuzisotea), tulizonazo kwenye taifa, halafu akajitumbukiza kwenye malumbano yasiyo na tija kabisa bila kuwa na data kamili.

Nashangaa kuna watu wanaargue kuwa ukienda ubungo bus terminal, sanasana utaingia mara moja kwa siku, ilihali watu wa kigamboni wana"vukavuka" mara kadhaa kwa siku katika kutafuta maisha. Kwa nini wana"vukavuka"? bila shaka ni sababu ya nauli sawa na bure. Hivi sijui hii haki ya ziada inatoka wapi, kwa mwananchi wa Dar es salaam hii hii, just because "amechagua" kuishi kigamboni.

Hivi mbona hao watu wanaopinga kupandisha nauli ya ferry, hawajiulizi wananchi wa Dar es Salaam, wanaoishi maeneo ya Bunju, au Madale, au Kongowe, au Chamazi au Majohe wanasurvive vipi wakati na wao wanatakiwa kufika katikati ya jiji kwa shughuli zao za kujitafutia maisha? Hawa wananchi wote kwa safari moja tu ni kati ya Tsh.800 mpaka Tsh.1200 ONE WAY kwa daladala. Na kuhusu maguta, hebu mtu akakodi guta kutoka Kariakoo hadi Bunju uone nauli ikoje? Waulizeni wachuuzi wa sokoni Tegeta wanawalipa kiasi gani hawa jamaa ndiyo mtajifunza maisha!

Kama ni "kuvukavuka" basi wananchi wote wa Dar es Salaam wanayo haki ya kuja na kutoka katikati ya jiji kadri wanavyojisikia. Lakini lazima watu waweze kuweka mipango ya siku ili kupunguza hii "kuvukavuka" kwa lugha nyingine kuplan siku yako vizuri.

Kama kuna mtu hataki kukaa kigamboni, namkaribisha huku Bunju, tena nampangisha chumba miezi sita ya kwanza akae bure, bila kulipa kodi, ili ajifunze kuwa maisha ya mjini sio lelemama.
 
Mtoa mada umewasilisha hoja kwa mapana na marefu yake, ila kuna takwimu hapa hazijakaa sawa: -

Umesema gharama kwa sasa ni 98% ya
(9,000,000) mapato kwa siku kwa nauli ya Tsh 100. Na ukasema nauli ikiwa Tsh 200 salio litakuwa ni sh.333, 332 (laki tatu), badala ya Sh. 166,666? Si kweli. Nauli ikiwa Tsh. 200, Salio litakuwa ni Tsh. 166,666 ongeza 9,000,000 (itayotokana na ongezeko la tsh 100 ktk nauli mpya) mana gharama zitakuwa covered na ile 98% ya 9,000,000 ya mwanzo wakat nauli ni Tsh 100 na sio kuwa nauli ikiongezeka kuwa 200 gharama nazo ztaongezeka kuwa 98% ya (9,000,000+9,000,000).

Pia ungetueleza gharama za uendeshaji kwa kina, Makusanyo kutoka kwenye nauli na ruzuku/subsidy ya serikali kwa siku/mwezi kabla ya kusema kwamba nani yupo sahihi au yupo wrong. Na imani kupitia kivuko hicho serikali inatoa huduma na sio kuwa inafanyabiashara, hivyo hatutegemei serikali kuweka kiwango ambacho kitamuumiza mwananchi as if serikali inafanya biashara. Kama unasema katika uendeshaji wa kivuko hicho zaidi ya nauli wanazotozwa wananchi kuna ruzuku ya serikali. Nina imani kubwa either hiyo ruzuku ni ndogo sana au haipo kbs au kama ipo basi kuna ufisadi mkubwa unaofanyika. Na labda pengine ndio msingi wa kelele za Wabunge

Mana kwa harakaharaka nimegawanya hicho kiasi ulichokitaja cha gharama za uendeshaji (Tsh8.8m) kwa tsh 2000 ya diesel kwa lita. Nimepata jumla ya liter 4400 za diesel zinatumika kwa siku. Ila kwa kuwa kuna mahitaji mengine ktk kuendesha panton hizo, assume lita 500 i.e 1,000,000/= kwa siku itacover hayo mahitaj mengine km grease, mishahara n.k. Bado liter 3900 kwa siku ni nyingi mno kwa matumizi ya panton mbili labda kama kuna mengine ila siamin kwamba gharama za uendeshaji wa panton hizo mbili kwa siku ni tsh Tsh 8.8m.
 
Mkuu usizungumzie badiliko la nauli ya binadamu tu, hebu jaribu kuzungumzia nauli ya kuvusha Guta
Hawa viongozi wetu wabunge hawakulizungumzia hilo sasa unataka Mchambuzi ndio alizungumzie?.. wao wanashindwa nini kusema wazi kwamba hawakukubaliana na sehemu hiii maana kilichopingwa na wananchi ni nauli toka Tsh 100 kwenda 200 na wabunge wamekurupuka kuunga mkono bila kueleza sehemu wanazozipinga wao. Wale wote waliokuwepo ktk mkutano wakizomea hawakuwa wafanyabiashara bali wananchi wapanda kivuko hicho. Na huyo kijana aloogelea toka magogoni hadi kigamboni mbona hakubeba pakacha la ndizi?.
 
Si kweli kwamba mtu anayetoka kigamboni kuja upande wa pili wa Dar kwa kutumia pantoni analipa shilingi 200 tu. Tukumbuke kwamba wakazi wa kigamboni wanatumia nauli kutoka majumbani mwao ili kufika eneo la feri na wanatumia tena shilingi 200 kuvuka. Hivyo ongezeko hilo la 100 sio tu limeongeza nauli ya msafiri wa kigamboni kuwa 200 bali tunatakiwa kujumlisha pia nauli wanazotumia kutoka majumbani mwao kufika hapo feri kwa ajili ya kuvuka. Hivyo basi kuna ambao walikua wanatumia shilingi 300 kwa siku sasa watalipa 400 na ambao walikuwa wanatumia 400 sasa wanalipa 500. Tusiupotoshe umma kwamba nauli imeongeza kutoka 100 kwenda 200 bali tuangalie nauli kutoka kule wakazi hawa wa kigamboni wanapoishi mpaka kuvuka kwa kutumia hilo pantoni.

Una hoja but it fits a different context; nauli ya daladala au bajaji kutokea majumbani kuja feri haipo katika equation tunayoizungumzia; focus hapa ni uamuzi wa kulipa sh 200 ili uje upande wa pili, iwapo hautaamua kughairi na kuchukua daladala au bajaji kurudi nyumbani kwa kukosa sh. 200 ili ikuvushe; Otherwise your variables ni relevant katika general equation ya gharama za usafiri Dar-es-salaam katika mazingira ya poverty among wakazi wengi wa jijini, na hoja hiyo inajadilika;
 
Hawa viongozi wetu wabunge hawakulizungumzia hilo sasa unataka Mchambuzi ndio alizungumzie?.. wao wanashindwa nini kusema wazi kwamba hawakukubaliana na sehemu hiii maana kilichopingwa na wananchi ni nauli toka Tsh 100 kwenda 200 na wabunge wamekurupuka kuunga mkono bila kueleza sehemu wanazozipinga wao. Wale wote waliokuwepo ktk mkutano wakizomea hawakuwa wafanyabiashara bali wananchi wapanda kivuko hicho. Na huyo kijana aloogelea toka magogoni hadi kigamboni mbona hakubeba pakacha la ndizi?.

Well said.
 
Halafu kuna mwenye taarifa juu ya uendeshaji wa daraja la kigamboni utakavyokuwa?

Maana last time nilisikia litajengwa na NSSF kwa mpango wa BoT (Build, Operate and Transfer), kwa maana hiyo hata hilo
daraja likija litatakiwa kulipiwa kwa kila mtu au gari(sijui itakavyokua) litakalokatisha mpaka deni litakapoisha.

Nashauri wabunge wetu wajipange tena kulumbana na waziri wa ujenzi wa kipindi hicho....
 
Mtoa mada umewasilisha hoja kwa mapana na marefu yake, ila kuna takwimu hapa hazijakaa sawa: -

Umesema gharama kwa sasa ni 98% ya
(9,000,000) mapato kwa siku kwa nauli ya Tsh 100. Na ukasema nauli ikiwa Tsh 200 salio litakuwa ni sh.333, 332 (laki tatu), badala ya Sh. 166,666? Si kweli. Nauli ikiwa Tsh. 200, Salio litakuwa ni Tsh. 166,666 ongeza 9,000,000 (itayotokana na ongezeko la tsh 100 ktk nauli mpya) mana gharama zitakuwa covered na ile 98% ya 9,000,000 ya mwanzo wakat nauli ni Tsh 100 na sio kuwa nauli ikiongezeka kuwa 200 gharama nazo ztaongezeka kuwa 98% ya (9,000,000+9,000,000).

Pia ungetueleza gharama za uendeshaji kwa kina, Makusanyo kutoka kwenye nauli na ruzuku/subsidy ya serikali kwa siku/mwezi kabla ya kusema kwamba nani yupo sahihi au yupo wrong. Na imani kupitia kivuko hicho serikali inatoa huduma na sio kuwa inafanyabiashara, hivyo hatutegemei serikali kuweka kiwango ambacho kitamuumiza mwananchi as if serikali inafanya biashara. Kama unasema katika uendeshaji wa kivuko hicho zaidi ya nauli wanazotozwa wananchi kuna ruzuku ya serikali. Nina imani kubwa either hiyo ruzuku ni ndogo sana au haipo kbs au kama ipo basi kuna ufisadi mkubwa unaofanyika. Na labda pengine ndio msingi wa kelele za Wabunge

Mana kwa harakaharaka nimegawanya hicho kiasi ulichokitaja cha gharama za uendeshaji (Tsh8.8m) kwa tsh 2000 ya diesel kwa lita. Nimepata jumla ya liter 4400 za diesel zinatumika kwa siku. Ila kwa kuwa kuna mahitaji mengine ktk kuendesha panton hizo, assume lita 500 i.e 1,000,000/= kwa siku itacover hayo mahitaj mengine km grease, mishahara n.k. Bado liter 3900 kwa siku ni nyingi mno kwa matumizi ya panton mbili labda kama kuna mengine ila siamin kwamba gharama za uendeshaji wa panton hizo mbili kwa siku ni tsh Tsh 8.8m.

Na wewe ni victim kama mimi - wabunge hawana takwimu za kujikinga na hoja yao, na walipoteza nafasi hiyo kwa uzembe wao bungeni kwa kutohoji kamati husika, ndio maana nasema kwamba hawana legitimacy ya kutoa kauli na misimamo yao kwa sasa, warudi wakajipange.

Kuhusu mahesabu niliyopiga, its simple: enzi za sh 100, kamati ya bunge ilisema mapato kwa siku ni milioni tisa, na masalio kwa mwezi ni sh milioni tano. kwa takwimu hizi, hii ina maana kwamba masalio kwa siku ni sh 166,000; sasa ukitoa hiyo katika milioni 9 ambayo ni mapato kwa siku, inakupa gharama kwa siku ni milioni nane na ushee, na surplus inabakia lakini moja na sitini na kitu; figure ya laki tatu nime double tu from 100 to 200 ya ongezeko la nauli, holding other things constant; hizi ni indicative figures tu, vinginevyo tatizo ni wabunge hawajawa wazi juu ya gharama halisi wanazozijua katika kumpinga magufuli; wangetufafanulia, pengine tusingekuwa katika huu mjadala.

Kuhusu gharama ya diesel n.k, kwa maelezo ya kamati ya bunge kwamba surplus kwa mwezi ni milioni tano (laki moja na sitini kwa siku), hii ina maana wameshatoa gharama za diesel etc; kitu muhimu hapa ni kuhimiza wabunge waje na takwimu kama wanazo nyingine, ili wananchi tuelewe kwa undani zaidi, vinginevyo kwa takwimu zilizopo, in my humble opinion, what Magufuli has done is justified.
 
Kauli aliyotoa magufuri ni ya busara sana, kama ukikosa nauli pinga mbizi, sioni ubaya wowote wa kauli hiyo. Tatizo wabongo hatupendi kauli za ukweli, tunapenda kauli za kudanganywa.
 
Umetoa hoja za msingi na zemye mantiki;no comment kwa sasa,namsubiri Mnyika aje atoe utetezi wake hapa;halafu nitachanganya na zangu!!!
 
Dogo nimekushusha leo, kweli sio kila kingaacho ni dhahabu!
Ina maana huoni tofauti ya nauli ya GUTA( Unalijua?) na GARI ndogo?
gta-017a.jpg

Hapa ikiwa imebeba kitowoe!
selling+ndizis+in+town.JPG


Kwetu hata kina mama wanaendesha hizi!

02.JPG
 
Umetoa hoja za msingi na zemye mantiki;no comment kwa sasa,namsubiri Mnyika aje atoe utetezi wake hapa;halafu nitachanganya na zangu!!!

Hakuna hoja huwezi kumfananisha mkaazi wa Kigamboni na hao wanao lipa nauli ya mia tatu kutoka Posta mpaka Feri. Au huoni tofauti?
 
...somo tunalopata hapa ni mfumo wetu waserikali ulivyo, nguvu ya tuliowachagua ni ndogo katika kuisimamia serikali kwaniaba yetu kwenye mfumo uliopo. TUNAHITAJI KATIBA MPYA YA WANANCHI itakayomaliza uzandiki huu. Kwa mfumo uliopo, nguvu ya umma tu ndio inayoweza kuukabili na sio bunge wala mahakama ama chombo kingine kilichopo. Binafsi nilitegemea kuona hizi harakati zilizoanzishwa na wabunge zikienda sambamba na mikutano na wananchi kuwafikishia hizi habari, kuwaelimisha na kupata maoni yao badala yakutumia vyombo vya habari ambavyo vimekuwa vikipotosha na kubaki kujadili kauli ya Magufuli na nauri ya Tsh. 200 kutoka 100 uku ukweli na mambo ya msingi yakiachwa kama kupanga kwa gharama za uchukuzi kwaujumla mf. guta toka 300 hadi 1800 ambako kunaongeza gharama za maisha, wizi na ufujaji wa mali za umma na ubovu wa huduma kwa ujumla wake...

Suala la kivuko cha Kigamboni linawagusa wakazi wengi wa Dar es Salaam na si wale wa Kigamboni pekee, kuna wengi tu wanaofanya kazi na kusoma Kigamboni pia. Zaidi ya hayo kuna bidhaa nyingi zinaingia na kutoka Kigamboni ambazo zitapanda bei na kuhathiri hata wale wasio watumiaji wa kivuko
 
Surplus hata kama ingekuwa Tsh 100, hiyo nihuduma itolewayo na serikali....kwani unafikiri hata hiyo serikali kuu inatengeneza surplus! Ufanisi kwa upande waserikali haupimwi na kiasi cha surplus kinachoweza tengenezwa
 
27 Reactions
Reply
Back
Top Bottom