Maadam swala hili lilipitia Bungeni na wakalipitisha bila kupinga... Inasikitisha sana kuona wabunge hao hao leo wanapinga ongezeko bila kuwa na takwimu kuthibitisha inawezakana kwa njia ipi na sii kusikilizia Upepo wa wananchi wanapozomea..Mnyika anatakiwa kuwa makini sana ktk maswala haya ya utendaji kazi maana sii mara ya kwanza kuvurugana na Magufuli akiwa upande wa JK ktk kutoa ahadi zinazoharibu utendaji kazi...kama lile sakata la Machinga na vibanda vyao Ubungo..Hayo ni maswali ya msingi. Kabla ya kuangalia uboreshwaji wa huduma, mapato ya wananchi, n.k, ni muhimu kwanza tuwe na takwimu juu ya gharama za uendeshaji wa kivuko kile, ambazo wabunge walizembea kuzihoji huko bungeni, na badala yake kuja kutupiga blah blah kwenye vyombo vya habari. Na ndio maana hoja yangu ya msingi ni kwamba kina Mnyika et al. hawana legitimacy kuhoji hayo barabarani. Hawana takwimu zozote zinazowasaidia kujenga hoja kwamba ongezeko la sh. 100 ni kubwa sana; Mbaya zaidi, walizembea kuhoji kamati ile ya bunge kuhusu gharama za uendeshaji wa kivuko kile. Kutokana na mapungufu hayo, hawana legitimacy, na wamekurupuka kwa msukumo wa kisiasa huku mantiki ikiwasuta. Warudie ile kamati ya bunge kwanza. Na mtu sharp kama Mnyika lazima kwa sasa analijua hilo, sina uhakika kuhusu wengine.
Magufuli ana mapungufu mengi kama kiongozi, lakini ni dhahiri kwamba Magufuli sio kiongozi wa 'kupurupuka' katika maamuzi.