Fikira wewe na mkeo mmeamka wote asubuhi salama wa salimini, wewe unakwenda kwenye mihangaiko yako kutafuta riziki yeye unamwacha nyumbani unarudi jioni yeye unakuta alitoka na hajarudi wakati unamtafuta kwa simu hapokei, na ghafla anagonga geti kwa nguvu mtoto anamfungulia unamuuliza kulikoni mke wangu anakujibu "nimetoka angaza kupima" bila ya kuagana wala taarifayoyote JE? kama wewe ni mwanamume kiruka njia na huelewi elewi lile tangazo la tuko wangapi utajisikiaje? wakati unatafakari anakupa taarifa kwamba yeye yuko salama hana maambukizi