yaan hii lugha imenitesa kwa muda mrefu sasa lazima nijifunze kwa nguvu, maboss wangu ndio native english speakers, majanga yanakuja pale tunapo Skype, yaani ni full kutetemeka na kuishia kusema yeah yeah, of course, true, duh hii aibu sasa basi!
Ha ha lazima unywe safari lagerNimejaribu kunywa pombe naona nahehuka tu. Hakuna mzungu anaejua kiufasaha anifundishe huenda nami nikawa mtaalamu wa hiyo lugha.
Nimejikuta nacheka peke yangu hii post yako ,some people you can't them.Kuna siku nilienda ofisi fulani nilikuwa na shida na marketing manager katika hiyo ofisi kubwa tu.
Baada ya kumweleza secretary kwa ufupi akaenda kuniitia bwana.
Yule jamaa alikuwa mzungu inaonesha anatokea london mjini kabisa kwa akina blair, kingereza chake kilikuwa hakieleweki yaani anacharaza kama cherehani, labda akiongea ufanye kuandika kwanza. Yaani ilikuwa aibu pale.
Ili kujinasua, nikatema yai broken mfulululizo bila kumpa nafasi ya kuongea halafu nikasema thank you, nikamwambia secretary utamwelekeza vizuri kama nilivyokwambia eeh!
Ndio maana hiyo lugha siipendagi kabisa.
jifunze kuvaa makoti mazito zito ili huo ubaridi usikukute alaf ukiongea kama confidence inapotea cheka kidogo hatakama hakichekeshi utakua ume lose attention alaf unaendelea na broken ili kuonesha unakosea maksudi kila ukiongea broken chekaWadau hii hali inanikuta nikitaka kutema yai sijui kwa nini tena nikiwa kwenye kadamnasi napata ubaridi zaidi. Msaada jamani naaibika mwenzenu.
jifunze kuvaa makoti mazito zito ili huo ubaridi usikukute alaf ukiongea kama confidence inapotea cheka kidogo hatakama hakichekeshi utakua ume lose attention alaf unaendelea na broken ili kuonesha unakosea maksudi kila ukiongea broken chekaWadau hii hali inanikuta nikitaka kutema yai sijui kwa nini tena nikiwa kwenye kadamnasi napata ubaridi zaidi. Msaada jamani naaibika mwenzenu.
Umesahau kwamba kila lugha inamazingira yake.yawezekana mazingira yanamlazimu kuitumia.vilevile hiyo ni lugha rasmi kwa taifa letu.Lugha ziko nyingi ukiongea Kisambaa au Kikurya kuna ubaya gani hapo pengine Lugha ya kwenu hujui hata Salaam unang'ang'ana na ung'enge nao haukutaki.
uwe unakunywa viroba kabla ya kuongea utapata ujasiri wa ajabu mi huwa nafanya hivyo