theophilius
Senior Member
- Nov 19, 2010
- 150
- 54
Hivi kwa nini Watanzania wanaochukia rasilimali za taifa kuibwa na mafisadi tusichukue hatua dhidi ya mafisadi, angalau wale wanaojulikana. Tunaweza kuanza kwa kususia bidhaa na huduma za makampuni ambayo ama rostamu na mafisadi wenzake wanamiliki (au kuwa na hisa) ambayo kwa kadri habari zinavyoendelea kujipambanua, rasilimali (wafanyakazi/magari/fedha) za makampuni hayo zinatumika katika vitendo vya kifisadi.
Ikiwa watanzania wataonesha chuki dhidi ya Vodacom, New Habari na mengine wanahisa wasafi wengine wa makampuni hayo watafukuza mafisadi kutoka makampuni hayo vinginevyo yafe kwa kukosa biashara hapa nchini.
Vinginevyo, mafisadi hawa wataendelea kupeta wakichota huku na huku kwani hakuna anayeweza kuwapeleka mbele ya sheria maana wameitia serikali mfukoni, ni budi sasa 'Nguvu ya Umma' itumike na kwa hakika ikifikia mahali ikatumika watakimbia wenyewe nchi na litakuwa funzo kwa wengine!
Ikiwa watanzania wataonesha chuki dhidi ya Vodacom, New Habari na mengine wanahisa wasafi wengine wa makampuni hayo watafukuza mafisadi kutoka makampuni hayo vinginevyo yafe kwa kukosa biashara hapa nchini.
Vinginevyo, mafisadi hawa wataendelea kupeta wakichota huku na huku kwani hakuna anayeweza kuwapeleka mbele ya sheria maana wameitia serikali mfukoni, ni budi sasa 'Nguvu ya Umma' itumike na kwa hakika ikifikia mahali ikatumika watakimbia wenyewe nchi na litakuwa funzo kwa wengine!