Natamani kujiua

Habari zenu wana Jamii Forum. Mimi ni mgeni humu. Ila si mgeni ki hivyo nimekuwa natembelea bila kuwa member. Nimeamua kujiunga ili nipate kushauriwa kwani shida niliyonayo siwezi kushare na mtu ninaye mjua.

Mimi ni mdada wa miaka 32. Ni mrembo sana yaani wale mnaoita 8 figure. Sijisifii ila hilo nimeona nilitamke ili muweze kuielewa vizuri mada yangu.

Nilitokea kumpenda sana kijana mmoja na kuja kugundua baada ya miezi miwili kuwa ni mume wa mtu. Kaka ni muislamu hivyo havai pete na kwa kuwa ni kijana sikuweza kudhania kuwa ni mume wa mtu na kwa kweli ningejua nisinge mpa moyo wangu.

Tatizo niligundua kuwa kaoa wakati nimeshampenda. Na ni yeye mwenyewe alinitamkia kuwa nina mke baada ya kujua sitaweza kumwacha kwani nilikuwa nimekolea.

Tumekaa kwenye uhusiano kwa muda wa mwaka na nusu sasa mpaka pale mkewe alipokuja kugundua. Mimi mkewe nilikuwa nimeshamjua. Ni mdada msomi na ana kazi nzuri sana ila ni wa kawaida na aniingii hata nusu kwa uzuri kwa hiyo nilijua tu kuwa mumewe atakuwa ananipenda mimi zaidi na labda kuna siku nitakuwa mke wa pili kwani ni muislamu.

Tatizo limeanza miezi miwili iliyopita. Jamaa alinipigia simu akanambia mkewe amejua kuwa tuna uhusiano, kwa hiyo mimi na yeye basi kwani hataki kuvunja ndoa yake. Nimeumia sana imagine mwaka na nusu na nimeshampenda sana. Nimejitahidi kumfuata ofisini kwao secretary wake ananambia jamaa kasafiri wakati gari naliona nje ya ofisi. Nimempigia simu simpati naona amebadili namba.

Hivi kweli wanaume mnaweza kuwa wakatili hivi? Kibaya zaidi mkewe kutwa ananipigia simu na kunitisha kuwa atanifukuzisha kazi. Mimi sijali kufukuzwa kazi kwani ninampenda sana huyo mwanaume.

Nishaurini nifanyeje kwa wale wenye uzoefu wa kuwa vimada na wale wenye nyumba ndogo.

Msinitukane jamani. Mimi sijawahi maishani mwangu kutembea na mume wa mtu zaidi ya huyu na sikuwahi kuwaza kuwa yatanikuta. Hivi nyie wanawake wa kwenye ndoa uwa mnawaroga wame zenu? Iweje mtu niliyekuwa nampagawisha the other day leo aseme sitaki kukuona tena kisa tu mkewe kajua?


Na huyu mkewe nimfanyeje aache kunifuata fuata. Maana amekuwa ananipa vitisho kila kukicha mpaka nahofia uhai wangu. Mumewe mwenyewe kesha niacha na yeye bado analeta mikwara wakati nikimwangalia hata ngumi moja namuua.


Adui mkubwa wa mwanamke sio mwanaume, bali ni mwanamke mwenyewe! Dada ulishajua ni mume wa mtu na bado unangangani! What did you expect out of it? Nilitegemea unegweza kuzishinda feelings zako na kuachana na mume wa mtu?

Unashangaa lililokupata? amwache mke wake kwa ajili ya uzuri wako? Unafikiri uzuri wa mwanamke ni kila kitu?

Pole sana. Pick up your pieces na uendelee na maisha. Umeshaona jamaa hayuko tayari kuvunja ndoa yake kwa ajili yako> next time, be more careful na wanaume, usikubali kupelekwa hoteli kila wakati, nenda kaone kwake, mbane awe close na transparent kwako.
 
Jifunze kuwa roho ya toba, kubali umekosea. Jivue gamba. Wewe ni wathamani sio chombo cha mtu cha kupumzikia halafu arudi kwa mke wake. Wakati ukifika Mungu atakupa mtu ambaye atakujali kukulinda na kukuwezesha kufikia malengo yako. Hata ku-hold kwa sababu anataka aendelee kukutumia tu hapana. Mta-share mipango ya maisha, atakufanya uweze ku-move stage moja kwenda nyingine. Hebu jifikirie tangia umekaa na huyo mume wa mtu amekusaidia nn? Ni kipi kipya ulichokipata? Zaidi ya tamaa za hii miili tu? Dah
 
Ana umbo namba 8
Ana miaka 32 hajaolewa
Ni mzuri
Ana kazi
Hajawahi tembea na mume wa mtu kabla ya huyo...
Amekaa na jamaa mwaka 1.5 lakini jamaa hajaamua kumuoa (dini yake ingeruhusu, na kipato bila shaka)

Conclusion
Yeye ni sexy (may be), Beautiful (may be) lakini sio marriage material (sio wife material)

Solution
Aachane nae, atafute mwingine, anaweza kuwa mume wa mtu tena au bachelor, but hatamwoa...
Na akijiuliza hao wa kwanza walikuwa hawajaoa na wakamtosa ndio kabisaaaaaaaa, kweli vizuri haviliki, wiki hii ni maumivu tu kwa wadada wa jf
 
...hovyo kabisa huyo! bora ajiue tukamzike.
Mkuu ana huo uthubutu mimi naona anaongea tu ili watu wapate kumfariji
""Mimi mkewe nilikuwa nimeshamjua. Ni mdada msomi na ana kazi nzuri sana ila ni wa kawaida na aniingii hata nusu kwa uzuri kwa hiyo nilijua tu kuwa mumewe atakuwa ananipenda mimi zaidi na labda kuna siku nitakuwa mke wa pili kwani ni muislamu.""

kwa akili hiyo wanaume watawa2mia kwa sana tu, nani alikuambia kigezo cha kuolewa ni mwanamke kuwa mzuri peke yake? wengine ni wa kawaida kabisa nadhani bac tucngeolewa, pweeehhh wacha wawatumie tu wakiwachoka ndio kama hivyo tena, halafu umezungumzia ishu ya kwamba tunawaloga waume zetu?....yaani wanawake wengine wa ajabu kweli.
Bora umesema wewe dada
LD, kuna wanawake wenzako ambao wanajua jinsi ya kuucheza huu mziki,
wa kuwa na mume wa mtu, na huwaambii kitu kuhusu waume za watu,
na siku zote huwa hawakosei hesabu!wako makini mpaka wanapitiliza...................
kwani mwisho wa siku wakiidhoofisha ndoa ya mzee, basi wanajua hata kwao mambo yatakuwa ovyo,
uimara wa ndoa ya mzee, ndo unawafanya na wao wafurahie mahusiano yao na waume za watu!!!!
Halafu wanasema wanaume wa kuoa hamna wakati yeye yuko busy na mume wa mtu
 
Asanteni kwa ushauri. Nitaufanyia kazi. Ila kumbukeni kuwa huyu mwanaume ni muislamu kwa hiyo nilijua fika kuwa atanioa. Na mara kwa mara alikuwa anaamia kwangu na kukaa hata siku mbili hivyo niliona kama hamna jinsi ya yeye kunitema. Nitajitahidi kumsahau.

Pole Kimada kwa kuwa hukujua ni mme wa mtu ila alivyokuambia ana mke hiyo ndo ilikuwa nafasi ya wewe kumuuliza uhusiano wenu anaenda wapi na kama kuna uwezekano wa wewe kuwa mke wapili au uchape lapa, siku nyingine wuwe unauliza hii kukaa kimya hailipi unakuwa hujui upo na mtu kwa ajili gani,
 
Kimada:
- First of all no man is worth your life! Let alone a married man aliyekutamkia hakutaki with words and actions!!

- Secondly kuhusu urembo na kumpagawisha, you can never relay on that for sure .While you may have been blessed with the looks , labda huyo mkewe has been blessed with cash na ndiye anayemhifadhi huyo jamaa?? Mind you love and/or sex never pays the bills!!

-Lastly, hebu jiulize if this guy really wanted you, kwanini akuache wakati you were willing to be his second wife na yeye imani yake inamruhusu to have more than one missus??


You have said it all.

Women, wake up and stop cheating yourselves eti mimi mzuri kuiko mkewe! Who told you so?
 
Asanteni kwa ushauri. Nitaufanyia kazi. Ila kumbukeni kuwa huyu mwanaume ni muislamu kwa hiyo nilijua fika kuwa atanioa. Na mara kwa mara alikuwa anaamia kwangu na kukaa hata siku mbili hivyo niliona kama hamna jinsi ya yeye kunitema. Nitajitahidi kumsahau.

kwa kweli nasemaga nikimkuta mr na kimada ctamgusa kimada lakini wewe lazima ningekutwanga mangumi ya kichaga walaah tena.
 
Ana umbo namba 8
Ana miaka 32 hajaolewa
Ni mzuri
Ana kazi
Hajawahi tembea na mume wa mtu kabla ya huyo...
Amekaa na jamaa mwaka 1.5 lakini jamaa hajaamua kumuoa (dini yake ingeruhusu, na kipato bila shaka)

Conclusion
Yeye ni sexy (may be), Beautiful (may be) lakini sio marriage material (sio wife material)

Solution
Aachane nae, atafute mwingine, anaweza kuwa mume wa mtu tena au bachelor, but hatamwoa...

Marriage material ndo wanakuwaje
 
...hata kumzika itakuwa tunampandisha daraja..afe tukamfukie! Ebo? Eti mzuri kuliko ...atayethubutu jinnadi hivi kwangu ajue kesha. Soulmate is number one.
 

Fanya hivi mi najitolea siku tujumuike pamoja na wewe ili akikupiga simu huyo mkewe naongea naye mimi .nitakachomueleza kama atarudia kuupigia atakupigia itakuwa ni kukuomba na yaishe.

So nasubiri pm yako kimada.



Mhhh, kuna kitu kimefichwa hapa!
 
Ahaaa ahaaa Gaga naona atakuwa anatizama kwa sura tu hajajua purukushani za wife wa jamaa zikoje ndio maana ana brag sana
Umeona msichana naona hajui, bora kapewa mkwara wake wengine huwa wanakodi watu kabisa ili kumkomesha msichana aache kabisa mchezo huo
 
Wanawake warembo, wazuri, vigoli, visura hawaolewi. It is my general observation kwamba wanaume hatutaki ugonjwa wa moyo! Mwanamke ambaye a man cant resist ni ugonjwa wa moyo kwa mmewe! House makers ni ordinary women kama huyo mke wa jamaa anatoka na kurudi bila usumbufu barabarani. Beautiful women are for leisure! Ni juu yako wewe kuiprove hiyo nadharia kuwa ni wrong! Na hilo unaweza lifanya kwenye uhusiano wako utakao fuata. Achana na mme wa mtu. Badili namba za simu, usikurupukie uhusiano mpya! Nadhani unafahamu madhara ya rebound! Ukishampata mpya determine to keep him no matter what.
 
Habari zenu wana Jamii Forum. Mimi ni mgeni humu. Ila si mgeni ki hivyo nimekuwa natembelea bila kuwa member. Nimeamua kujiunga ili nipate kushauriwa kwani shida niliyonayo siwezi kushare na mtu ninaye mjua. Mimi ni mdada wa miaka 32. Ni mrembo sana yaani wale mnaoita 8 figure. Sijisifii ila hilo nimeona nilitamke ili muweze kuielewa vizuri mada yangu. Nilitokea kumpenda sana kijana mmoja na kuja kugundua baada ya miezi miwili kuwa ni mume wa mtu. Kaka ni muislamu hivyo havai pete na kwa kuwa ni kijana sikuweza kudhania kuwa ni mume wa mtu na kwa kweli ningejua nisinge mpa moyo wangu. Tatizo niligundua kuwa kaoa wakati nimeshampenda. Na ni yeye mwenyewe alinitamkia kuwa nina mke baada ya kujua sitaweza kumwacha kwani nilikuwa nimekolea. Tumekaa kwenye uhusiano kwa muda wa mwaka na nusu sasa mpaka pale mkewe alipokuja kugundua. Mimi mkewe nilikuwa nimeshamjua. Ni mdada msomi na ana kazi nzuri sana ila ni wa kawaida na aniingii hata nusu kwa uzuri kwa hiyo nilijua tu kuwa mumewe atakuwa ananipenda mimi zaidi na labda kuna siku nitakuwa mke wa pili kwani ni muislamu. Tatizo limeanza miezi miwili iliyopita. Jamaa alinipigia simu akanambia mkewe amejua kuwa tuna uhusiano, kwa hiyo mimi na yeye basi kwani hataki kuvunja ndoa yake. Nimeumia sana imagine mwaka na nusu na nimeshampenda sana. Nimejitahidi kumfuata ofisini kwao secretary wake ananambia jamaa kasafiri wakati gari naliona nje ya ofisi. Nimempigia simu simpati naona amebadili namba. Hivi kweli wanaume mnaweza kuwa wakatili hivi? Kibaya zaidi mkewe kutwa ananipigia simu na kunitisha kuwa atanifukuzisha kazi. Mimi sijali kufukuzwa kazi kwani ninampenda sana huyo mwanaume. Nishaurini nifanyeje kwa wale wenye uzoefu wa kuwa vimada na wale wenye nyumba ndogo. Msinitukane jamani. Mimi sijawahi maishani mwangu kutembea na mume wa mtu zaidi ya huyu na sikuwahi kuwaza kuwa yatanikuta. Hivi nyie wanawake wa kwenye ndoa uwa mnawaroga wame zenu? Iweje mtu niliyekuwa nampagawisha the other day leo aseme sitaki kukuona tena kisa tu mkewe kajua? Na huyu mkewe nimfanyeje aache kunifuata fuata. Maana amekuwa ananipa vitisho kila kukicha mpaka nahofia uhai wangu. Mumewe mwenyewe kesha niacha na yeye bado analeta mikwara wakati nikimwangalia hata ngumi moja namuua.
mh! Pole. Ukweli ndo huo kuwa huhitajiki tena. Hali ya kimaisha ya huyo mwanaume yaonekana imeshikiliwa na mkewe. Huwezi fanya kitu hapo. Utaumia moyo sana ila itafika muda yatapita. Mwaka unusu ni muda mchache sana. Hujachelewa kuwa na wako. Nyimbo 3 za jd zisikilize; usiusemee moyo, nitafanya, pamoja na huu mpya aloimba na blue.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom