Nataka kuvunja ndoa yangu; mme amezidi kwa dogo dogo

Status
Not open for further replies.
Nawashukuru sana kwa maoni yenu. ijulikane kuwa ndugu zangu wakubwa wote wamefariki mimi ndo mkubwa sasa. Ktk msg zingine za aliyeolewa zinaonyesha wake na mawifi wakiwasiliana na mwolewaji. Pili nina ngeo ya nyuzi 5 kichwani na ya mdomoni niliona aibu kwenda hospital ili tu nimlindie heshima. Sasa nikiwa mkristo huko kanisani nilikwenda lakini alifika na kuwahonga wachungaji (majina ninayo ili waseme huwa nasali nini huko kanisani), alinambia mwenyewe wakati akiwabeza wachungaji. Nacho hitaji ni ushauri. Huyu ni mtu. Wangapi baba zao walikufa juu ya wasichana ktk magesti house na wapo. Usinibeze hata kidogo, am old enough to ask for your opinions. Ukinibeza nakuona kama ni mmoja wa visichana hivi. we are above 50yrs old.

Ebu kabla ya kunibeza fikiria janga hili la HIV hao watoto wataenda vipi shule? I welcome anyone with positive opinions than humiliations which am suffering from. Usiniongezee hilo.

Thanx. Ni kwa nini mtu aifiche dhambi? Ni maandiko gani yanayotetea dhambi kwa kuificha?
usiogope mama dai kilicho chako uishi kwa amani
na hao mahawara endelea kuleta data
wengine wana ndoa zao kama wameharibu yako na wewe waharibie
toa majina yao na no zao kama kawa
 
hawara mwenyewe ndo huyo,mimi asingenibabaisha kabisa.Mbilia kama kweli wewe ni mke wa ndoa kabisa.Usigombane na mahawara wa mmeo kabisa au hata mmeo,mimi ningewakomesha hata kwa tindikali.
 
Nawashukuru sana kwa maoni yenu. ijulikane kuwa ndugu zangu wakubwa wote wamefariki mimi ndo mkubwa sasa. Ktk msg zingine za aliyeolewa zinaonyesha wake na mawifi wakiwasiliana na mwolewaji. Pili nina ngeo ya nyuzi 5 kichwani na ya mdomoni niliona aibu kwenda hospital ili tu nimlindie heshima. Sasa nikiwa mkristo huko kanisani nilikwenda lakini alifika na kuwahonga wachungaji (majina ninayo ili waseme huwa nasali nini huko kanisani), alinambia mwenyewe wakati akiwabeza wachungaji. Nacho hitaji ni ushauri. Huyu ni mtu. Wangapi baba zao walikufa juu ya wasichana ktk magesti house na wapo. Usinibeze hata kidogo, am old enough to ask for your opinions. Ukinibeza nakuona kama ni mmoja wa visichana hivi. we are above 50yrs old.

Ebu kabla ya kunibeza fikiria janga hili la HIV hao watoto wataenda vipi shule? I welcome anyone with positive opinions than humiliations which am suffering from. Usiniongezee hilo.

Thanx. Ni kwa nini mtu aifiche dhambi? Ni maandiko gani yanayotetea dhambi kwa kuificha?

mkuu kuna watu watakushauri wengine watakubeza lakini pia nakushauri kama wenzangu kuwa uende kwanza kwa Jaji mkuu umweleze ikishindikana basi tafuta mwanasheria akuongoze ili upate haki zako zote. once again pole sana.
 
Nawashukuru sana kwa maoni yenu. ijulikane kuwa ndugu zangu wakubwa wote wamefariki mimi ndo mkubwa sasa. Ktk msg zingine za aliyeolewa zinaonyesha wake na mawifi wakiwasiliana na mwolewaji. Pili nina ngeo ya nyuzi 5 kichwani na ya mdomoni niliona aibu kwenda hospital ili tu nimlindie heshima. Sasa nikiwa mkristo huko kanisani nilikwenda lakini alifika na kuwahonga wachungaji (majina ninayo ili waseme huwa nasali nini huko kanisani), alinambia mwenyewe wakati akiwabeza wachungaji. Nacho hitaji ni ushauri. Huyu ni mtu. Wangapi baba zao walikufa juu ya wasichana ktk magesti house na wapo. Usinibeze hata kidogo, am old enough to ask for your opinions. Ukinibeza nakuona kama ni mmoja wa visichana hivi. we are above 50yrs old.

Ebu kabla ya kunibeza fikiria janga hili la HIV hao watoto wataenda vipi shule? I welcome anyone with positive opinions than humiliations which am suffering from. Usiniongezee hilo.

Thanx. Ni kwa nini mtu aifiche dhambi? Ni maandiko gani yanayotetea dhambi kwa kuificha?

Pole sana,inauma na kuumiza hii. Mungu na akutangulie ktk hali ulionayo, ongeza maombi kwa kufunga kwa Imani. Hakika Mungu anajua haki yako na dhuruma uipatayo kwa mumeo. Atatenda, kila laheri mbilia
 
Pole MBILIA, jambo la kwanza unalopaswa kufanya ni kupeleka suala lako kwenye bodi ya usuluhisihi wa ndoa (Marriage Conciliation Board). Hii ni kwa sababu kulingana na Sheria ya Ndoa Sura ya 29 kesi zote za talaka ni lazima zianzie kwenye bodi ya usuluhishi wa ndoa. Usipopeleka bodi mahakamani utawekewa pingamizi na kesi ya talaka itafutwa.( ila hutapaswa kupeleka suala lako bodi ikiwa kuna mazingira maalumu ya kukuzuia kwenda bodi mfano mumeo hapatikani nk). Bodi itajaribu kuwapatanisha na ikishindikana watatoa karatasi inayoonyesha kuwa wameshindwa kuwasuluhisha, hapo ndo utakuwa na uwezo wa kudai talaka mahakamani. Siku nyingine ukipigwa ni vyema ukaripoti polisi ili uwe na record kuwa ulishawahi kuteswa (kupigwa) na ulirepoti tukio hilo polisi. Huo utakuwa ni ushahidi kuwa ulikuwa wateswa (cruelty). Pia kusanya majina ya hao wanawake wengine wa mumeo pamoja na watoto wa nje ya ndoa wa mmeo, kama wapo na ushahidi kuwa wanamahusiano ili uweze kuthibitisha uzinzi wa mumeo. Kumbuka kutambua mali zote mlizozichuma wakati wa ndoa hata kama zipo kwa jina la mume tu, ili uweze kudai mgawanyo wa mali. Mwisho, ni vyema ukatafuta wakili ili akusimamie shauri lako.
 
Binafsi nawakilisha kilio cha wake za wanasheria duniani.Wengi wameuawa na kupigwa wakakosa hata pa kushitaki. Mfano tunao wa mama yule wa Mkwepu Posta. lakini ushahidi wote ulitupwa kwa kisingizio kuwa yule mtoto wao angekosa mtu wa kumlea. Hivyo for the first time maiti akakosa haki. Je, damu yake ilikuwa maji?

Nitapigania haki yangu hata kama nikifa. Sioni faida ya ndoa iwapo huko ndani mimi ni mtumwa.
 
  • Thanks
Reactions: SG8
MKA thanx very much. Hiyo bodi naendaje? Nipo dar. mali zote najua zilipo hata nyumba alizojengea mahawara najua zilipo.
 
Inawezekana pia ni mke halali wa huyo jaji. So just give her a benefit of a doubt for now. The truth will ultimately come out.
I was married on 27th April 1991 keko Lutherani Church at 16:30. We engaged in year 1988 At the UDSM. Aliyefunga ndoa yetu alikuwa Mzee malasusa (Baba ya..)
 
sielewi yafuatayo.

Mtu wa miaka 45+ kushindwa suluhisha ndoa yako kwa busara bila kuathiri maslahi ya familia. Eti wazazi hawapo, wakati huo huo unajiandaa kupata wakwe toka kwa watoto wako, utawasaidia kusuluhisha nini?

Kuweza muanika mmeo halali kwenye mitandao ya kijamii kama hii, kwa mtu wa miaka 45+ nashinda mwelewa.

Hii panic ya jana kaipata wapi maana ndoa ya miaka 21 tabia ya mmeo kama ya umalaya haijaanza jana tu, huo mshangao wa jana umetoka wapi??

Ukiachana na ushabiki, utafurahi ukiona mama yako kachukua njia hii kusuluhisha mgogoro wa ndoa, hata baba yako mkosaji??

Hajawavua nguo familia nzima? Labda mie nayechangia hapa ndio kijana wake wa chuo kikuu atajuaje??

Katika familia chunga hasira zako zisiathiri watu wako wa karibu, hivi ameshindwa hata shirikisha watoto wake kabla hajaweka details zote hapa??

Haya huyo jaji mahakama kuu ya ardhi si anajulikana, wabaya wake hata wa kazi hawatataumia hili against himu??

Hapo hapo usifikiri kaacha kuwa tegemezi kwa huyo mmewe, bado ni tegemezi kwa jinsi navyomuona.

Hakuna mwanamke mwenye upeo anaweza fanya hili kwa familia yake ni boya tu.
Hapa watu tunashabikia sababu tunataka umbea si kwamba tunaumia naye kivileee, ila kachemsha mbaya, hasa nikiangalia na umri wake.

Kitu gani humuelewi mkuu?
 
Mla nawe hafi nawe ilia mzaliwa nawe!!!!!. CCM sio mama Yangu alisema Nyerere. Kama mapenzi yameisha basi, SANA SANA KINACHOFUATA NI UKIMWI-YOTE YANAWEZEKANA. And in most cases watu kama hao wanatembea na bar maids ambako maambukizi ya ukimwi ni makubwa. Atafakari sana. Jitu lina malaya kibao, TAFAKARI, CHUKUA HATUA

ungevaa viatu vyake ndio ungeeleweka

Hujui pain and humiliation kaisi gani anapitia huyo dada....

kwenye mateso hakuna too late, ndio maana mandela alikaa jela for years but when he got out, he felt as free as a bird

Mbilia hajachelewa, ni fikra za kitumwa zinazoonyesha mwanamke hawezi kuishi peke yake au hana thamani, she can live signle and yet successful and everything

PIA ANAHITAJI MWANAUME WA KUMPA RAHA NA SIA KARAHA

TUSISAHAU LA HIV IWE AMESHAPATA MAAMBUKIZI AU LA

Nenda kwa Jaji Mkuu/ Jaji kiongozi. nakupa mfano: Kuna jaji mmoja ambaye alikuwa anafanya mambo kama hayo, tukamshauri aende mke wake kwa Jaji Mkuu amshitaki/amlalamikie kama usuluishi. Ilisaidia, jaji aliacha upuuzi angalau yale ya kukataa kutunza watoto, kutaka kumfukuza alikoma. jaribu njia hiyo. Ikishindikana tafuta mwanasheria akuongoze. Una haki zote kisheria kugawana chochote mlichopata pamoja-matrimonial assets. Nitakupa reference cases ambazo landmark cases katika tanzania kuhusiana na mgawanyo wa mali kati ya mme na mke. If you like just PM. Pole sana
ninyi watu wawili mmeongea ujinga kama mna akili za kuku wa kisasa vile. nampongeza CHUAKACHARA, ameongea point na nafikiri mama akichukua hatua/ushauri huu utamsaidia. aende kwa jaji kiongozi etc kama alivyoshauriwa. lakini ninyi wengine wawili ambao nimewakoti hapa, akili zenu ni za kinyama sana. hamfai kutoa ushauri kwa mtu ambaye yuko kwenye tatizo, mnaweza hata kumshauri mtu anywe sumu ili afe. akili zenu ni za shetani kabisa. nasema hivi kwasababu ukisoma uyu mama alivyoongea, na thread zake mbili alizoanzisha, utakuta kuwa, pamoja na kwamba anaomba ushauri wa kutaka talaka, sio kwamba anataka talaka. bado anaonekana kumpenda mumewe na anahangaika kumpokonya kutoka katika mikono ya malaya hao aliowataja. kwenye thread yake moja ameongea kuwa amemuona mumewe anaongea na simu akahisi anaongea na mwanamke wake. nafikiri huyu mama ana mpenda sana sana mumewe ndo maana ana wivu wa aina hii. ana wivu sana sana. na amekasirika amefikia mbali sana, anahitaji msaada ili chochote atakachokifanya kwa sasa asijekujilaumu baadae kuwa alienda haraka. kwa kifupi ni kwamba, kama mnasema ukimwi, akiachika, huyu atakayeenda kumpata mpya wa kuzeeka naye atakuwa salama? atakuwa na upendo wa rohoni kuliko yule aliyekaa naye miaka 21? unajua kuwa mtu ukioana naye mkakaa miaka yote hiyo ni sawa tu na mwili mmoja? hatawakuja waachane kamwe hata kama watatengana na kutengana kwa aina hii huleta vidonda ndugu kwenye mioyo na mvurugano wa ajabu. siku ingine muwe na akili kushauri watu mambo mazuri, msiwatumbukike shimoni zaidi wakati mnaona wapo kwenye wakati mgumu. watakuja kuwalaumu hasira zao zikiisha kuwa mliwashauri vibaya. yaani hapa jf kuna watu wengine huwa naweza amini kuwa sio binadamu wa kawaida, labda majini nayo yametengeneza account humu ili kuharibu watu. akili za kishetani kabisa kutoa ushauri kama huo kwa mtu ambaye yuko njia panda.....kama ukimwi unaweza kuupata popote pale, na kama huna mume au mke kama nyie mliotoa ushauri huu ndo ukimwi utaupata haraka kuliko wengine. akitengana huyo atapata ngoma fasta kuliko akiwa kwenye ndoa yake ya 21 years. NINYI MLIO TOA USHAURI MBAYA, KAMA NDOA ZENU ZILIWASHINDA MSITAFUTE WANACHAMA WENZENU WA TALAKA, bakieni na matalaka yenu hukohuko...mnaongea kama vile ndoa ziliwashinda na mnataka kila mtu afuate nyayo zenu..mnakera sana aisee.
 
sielewi yafuatayo.

Mtu wa miaka 45+ kushindwa suluhisha ndoa yako kwa busara bila kuathiri maslahi ya familia. Eti wazazi hawapo, wakati huo huo unajiandaa kupata wakwe toka kwa watoto wako, utawasaidia kusuluhisha nini?

Kuweza muanika mmeo halali kwenye mitandao ya kijamii kama hii, kwa mtu wa miaka 45+ nashinda mwelewa.

Hii panic ya jana kaipata wapi maana ndoa ya miaka 21 tabia ya mmeo kama ya umalaya haijaanza jana tu, huo mshangao wa jana umetoka wapi??

Ukiachana na ushabiki, utafurahi ukiona mama yako kachukua njia hii kusuluhisha mgogoro wa ndoa, hata baba yako mkosaji??

Hajawavua nguo familia nzima? Labda mie nayechangia hapa ndio kijana wake wa chuo kikuu atajuaje??

Katika familia chunga hasira zako zisiathiri watu wako wa karibu, hivi ameshindwa hata shirikisha watoto wake kabla hajaweka details zote hapa??

Haya huyo jaji mahakama kuu ya ardhi si anajulikana, wabaya wake hata wa kazi hawatataumia hili against himu??

Hapo hapo usifikiri kaacha kuwa tegemezi kwa huyo mmewe, bado ni tegemezi kwa jinsi navyomuona.

Hakuna mwanamke mwenye upeo anaweza fanya hili kwa familia yake ni boya tu.
Hapa watu tunashabikia sababu tunataka umbea si kwamba tunaumia naye kivileee, ila kachemsha mbaya, hasa nikiangalia na umri wake.

Usidhani jambo hili limeanza leo hata nipaniki. Since 199... Lakini ninaposema nimechoshwa. Siyo tu ninangeo bali mangeo ya miaka. Ukimwalika msuluhishi anamchukia mtu huyo. Sasa ana marafiki anwalaani kila siku kwa mimi kuomba suluhu toka kwao. Tabia hii sisi wazee tusipoisema vijana itawathili. Unakimbilia kwa watu kakufukuza na midamu tele kisha anawachukia wale watu.
 
Mimi sioni kama amemuanika hadharani mme wake, coz hajamtambulisha kwa jina na hata huyu mama I'm sure MBILIA ni jina la bandia tu! Kwa hiyo kilichotajwa hapa ni situational not personal inawahusu WAKWARE wote.
 
Kwa kweli muhishimiwa kachemka sana kama ni kweli, napenda nichukue nafasi hii kukupa pole sana mama muhishimiwa, najua uko kwenye wakati mgumu sana lakini itakubidi ujitahidi kuwa imara, watoto wanakutegemea sana maana hawa jamaa wakishatekwa huwa wanasahau mpaka watoto. Pole sana!

Kuna haya maneno amabayo kama sikosei yanatoka kwenye maandiko ya Mungu: "Mwanamke mwenye hekima huijenga nyumba yake, na mwanamke mpumbavu huibomoa nyumba yake kwa mikono yake mwenyewe."

Utafiti usio rasmi unaonyesha kuwa kwa kiwango fulani mwanandoa kutokuwa mwaminifu huchangiwa na tabia za mwenzake ambazo hazipalilii uhusiano wa ndoa. Tatizo letu huwa tunafikiria tunakoangukia badala ya kujiuliza tulipojikwaa na sababu zilizotufanya tujikwae.

Ushauri: Badala ya kufikiria kuibomoa nyumba yako jitaidi kufikiria jinsi ya kuijenga, na itakuwa vizuri kama utaomba ushauri wa kuimarisha nyumba yako badala ya kuomba ushauri wa kuivunja, najua JF iko na wataalam wengi watashauri na sisi wengine tutajifunza kupitia kwenye ushauri hasi utakaotolewa.
 
mmmhh, sijui unapitia nini lakini kwa mie siwezi muanika mme wangu hivi.
Hawara sawa nitamwamnika, mme hell no.

Ni aibu yako, ya watoto, ya ndugu zako, ya ndugu zake, na yeyey mwenyewe.

Kama umeshindwa, kwa nini usifanye maamuzi na kuondoka na kushirikisha familia zenu ukapata haki zako??
Umeamua kumuabisha ili akome? Haikusaidii kwa kweli.

Kwa details ulizotoa hapa sijui magazeti ya udaku yapate, yamwanike ukurasa wa mbele, unadhani watoto wako watasoma huko chuo kwa wiki nzima.

Nimekukasirikia sana wewe mama, ume-act kama mala.ya aliyechukuliwa na mwanamme kwa usiku mmoja, kamwaga mboga umemwaga ugali. Nadhani nafasi ya mke wa ndoa ni zaidi ya hicho ulichofhanya.

Unaamini watu wa hapa kuliko hata nduguzo? Nina maswali kibao, umenishangaza kama mke wa kiaka 21 anaweza fanya hivi.

Kosa la umalaya limefuta wema wake mwingine wote aliowahi kufanyia hadi kumvua nguo hivi? Hebu mkumbuke tangu day 1 anakutongoza, hadi mnaoana, hadi mnapata watoto, hakuna jema hata moja??

Umenikumbusha story ya biblia, abrahamu alivyokuwa anambembeleza malaika wasichome sodoma na gomora. Hata ukikuta watu wema 20, utachoma mji, malaika anajibu hapana, nitawasamehe.

Wewe nawe umekosa hata jema moja la kumsamehe mmeo? Afu usipende kupayuka ukiwa na hasira utajuta siku moja.

Mimi sioni kama amemuanika hadharani mme wake, coz hajamtambulisha kwa jina na hata huyu mama I'm sure MBILIA ni jina la bandia tu! Kwa hiyo kilichotajwa hapa ni situational not personal inawahusu WAKWARE wote.
 
wee ni msafi hivyo?

Huna waa hata moja?

Sijaelewa ulivyotumia neno kafiri, pagani na anayemjua Yesu kutokuwa human beings.

Hadhi gani? mtu ambaye ni kahaba au fisadi au mwizi au pagani i.e mtu asiyemtii Yesu au kafiri ana hadhi gani ya kuitwa human being?
 
Status
Not open for further replies.

Similar Discussions

Back
Top Bottom