Wakuu wana JF na wachambuzi wa mambbo ya siasa....!
Nina lengo thabiti la kutaka kulikomboa jimbo la Namtumbo ili niweze kuwatumikia vyema wananchi wa Namtumbo na kuwaletea maendeleo.
Wiki lilopita nilikua huko jimboni kwa kazi maalumu na nilibahatika kupita ktk karibu maeneo mengi....kama vile Msindo, mawa, mlilayoyo, hanga, mputa, kitanda, mgombasi, nambecha, namtumbo yenyewe, suruti, mchomoro, ligera, mkongo, mtwara pachani, namabengo, lumecha hadi mtakanini(kijiji alichozaliwa mama yake Vita kawawa...na ndiko ukweni kwa marehemu mzee kawawa.......!
Kwa kweli hizo sehemu zote nilizopita wanamlaani sana mbunge wao kwa sababu amekuwa mchumia tumbo lake tu bila kujali maendeleo ya wapiga kura wake....mfano...
Hivi sasa ana majumba kadhaa pale namtumbo aliyeyajenga kwa kutumia pesa ya rushwa kutoka kwa wamarekani wanaochimba madini ya Uranium kule mbuga ya Seluu ila asipige kelele kule bungeni,
Wananchi wa namtumbo wakulima wa tumbaku...ni kilio tu mwaka huu...tumbaku imerudishwa toka morogoro hali yeye ni menyekiti wa bodi ya tumbaku tanzania.....
Shule nyingi za st.kayumba..maarufu shule za kata hazina madawati, majengo yamesimama kuendelezwa toka lowasa ajiuzulu kuwa waziri mkuu hadi hii leo....
Kuna baadhi ya vijiji hadi leo wanakunywa maji ya mtoni ambayo sio salama,
Miradi mingi ya afya imesimama toka project ya Tasaf ....hakuna kilichoendelea....!
Nipo huku Arusha lakini nia yangu ni kuikomboa Namtumbo kutoka chama cha ******* na hatimaye CHADEMA ichukue jimbo na kuleta maendeleo kwa wananchi.
NB: Huyu mbunge anaishi dar maeneo ya mikocheni hapo kajenga gorofa yake anakula kuku, huku namtumbo wananchi hawamjui toka wakati wa kuomba kula....sio kura.....hadi hii leo, na akifika huishia kuleee namtumbo ofisini kisha huabiria ndege ya wazungu (watu wa madini ya uranium) na kurudi Dar!
Kifupi wananchi hawampendi kabisaaaa.....nataka kuikomboa namtumbo via Chadema.....Naomba ushauri wako nianze vipi au nitoke vipi ili kuli...ng'oa gambaz huko Namtumbo!!!
karibu kwa ushauri/Maoni yako.
mh! Jamani! Vita ni jirani yangu kabisa! Hilo ghorofa mbona silioni? Napita tu mpaka baadae!