Sir R
JF-Expert Member
- Oct 23, 2009
- 2,175
- 298
Ninapenda kujitolea kuifanyia CHADEMA kampeni bure mwaka huu. Ni kutokana na uhaba wa fedha CHADEMA na kwa kuzingatia kuwa mabadiliko yanahitajika Tz. Miaka zaidi 40 ya umaskini ni aibu kubwa kwa nchi yenye rasilimali nyingi.
Ninaomba CHADEMA inisaidie kufahamu
i. kujitolea kunaruhusiwa kuifanyia CHADEMA kampeni
ii. Kuna utaratibu wowote uliowekwa na chama wa watu kujitolea kufanya kampeni.
Binafsi nitafurahi kama CHADEMA wanaruhusu kujitolea na kama utaratibu upo, ni vema tukajulishwa mapema ili tushiriki katika shughuli muhimu. Ningependa kuwashawishi wote wenye nia ya dhati ya kuleta mabadiliko ya utawala ndani ya nchi hii ili kuleta maendeleo, washiriki ipasavyo katika kampeni ya kujitolea kwa ajili ya CHADEMA.
Tusisubiri kulipwa,, tutoe kile kidogo tulicho nacho kwa ajili ya wagombea kupitia CHADEMA. Si lazima fedha inaweza kuwa mawazo ya kujenga kama vile kuhamasisha wananchi kkushiriki kuchagua CHADEMA bila uwoga. Kama una fedha unaweza kutoa. Mimi ni raia wa kawaida mwenye nia ya dhati ya kuleta mabadiliko ya kweli.
Ninawahamasisha form six leavers wote na wanachuo wote kwa pamoja kujitolea kwa ajili ya CHADEMA; Tuwe sehemu ya mabadiliko, tusisubiri mabadiliko yatokee. wewe uyasababishe. Ni muda wetu kuleta mabadiliko ya kweli si wakati mwingine.
Ninaomba CHADEMA inisaidie kufahamu
i. kujitolea kunaruhusiwa kuifanyia CHADEMA kampeni
ii. Kuna utaratibu wowote uliowekwa na chama wa watu kujitolea kufanya kampeni.
Binafsi nitafurahi kama CHADEMA wanaruhusu kujitolea na kama utaratibu upo, ni vema tukajulishwa mapema ili tushiriki katika shughuli muhimu. Ningependa kuwashawishi wote wenye nia ya dhati ya kuleta mabadiliko ya utawala ndani ya nchi hii ili kuleta maendeleo, washiriki ipasavyo katika kampeni ya kujitolea kwa ajili ya CHADEMA.
Tusisubiri kulipwa,, tutoe kile kidogo tulicho nacho kwa ajili ya wagombea kupitia CHADEMA. Si lazima fedha inaweza kuwa mawazo ya kujenga kama vile kuhamasisha wananchi kkushiriki kuchagua CHADEMA bila uwoga. Kama una fedha unaweza kutoa. Mimi ni raia wa kawaida mwenye nia ya dhati ya kuleta mabadiliko ya kweli.
Ninawahamasisha form six leavers wote na wanachuo wote kwa pamoja kujitolea kwa ajili ya CHADEMA; Tuwe sehemu ya mabadiliko, tusisubiri mabadiliko yatokee. wewe uyasababishe. Ni muda wetu kuleta mabadiliko ya kweli si wakati mwingine.