Mnyamahodzo
JF-Expert Member
- May 23, 2008
- 1,932
- 985
Ili niujue UONGO lazima niwe na UKWELI. Nitaendelea kuuamini uongo kuwa ndiyo ukweli hadi pale nitakapoujua UKWELI.Nikijua ukweli ukaniletea uongo ukisema huu ndiyo ukweli nitakwambia wewe ni MWONGO kwa kwa sababu kile UNACHOSEMA NI UONGO.
Wakati sakata la wizi wa Benki Kuu linaanza kupigiwa kelele, viongozi wa vyama (CHADEMA,CUF,TLP na NCCR-Mageuzi) walitoa matamko yao kupinga wizi uliofanywa na CCM, kuiba fedha za umma na kuzitumia kwenye kampeni 2005. katika mkutanoi huo Dk Slaa ndiye aliyetamka wazi kuwa kiasi cha shilingi bilioni 10 [kupitia kampuni ya Deep Green] waliiba fedha toka Benki Kuu ili zitumiwe na CCM kwenye kampeni mwaka huo.Tundu Lissu pia alikuwepo wakati viongozi hao wakitoa tamko lao.
Taarifa hizo zilipotolewa na vyombo vya habari vikiwemo gazeti la Mwananchi na ThisDay, Yusufu Makamba,Katibu mkuu wa CCM, alijibu mapigo.
""Katibu Mkuu wa Chama hicho, Yusuf Makamba aliliambia gazeti hili (Mwananchi) jana kuwa tuhuma kwamba CCM kiliiba fedha kwa ajili ya kufanikisha kampeni zake za uchaguzi hazina ukweli wowote.
"Siwezi kutoa ufafanuzi juu ya madai ya uongo. Uongo haujibiki unakaliwa kimya," alisema Makamba.
Alisema wapinzani waliotoa tuhuma hizo walipaswa kuzitoa wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu mwaka 2010 ili jamii iweze kuwaunga mkono, badala ya kuzitoa sasa na kumaliza uongo wote uliotakiwa kutolewa wakati wa uchaguzi huo.
"Uongo huo ungewasaidia kama wangetoa wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu mwaka 2010, sasa wanapoumaliza leo watasema nini kipindi hicho kikifika?" alihoji
Mbali na BoT na CCM, watuhumiwa wengine ambao umoja wa wapinzani umewahusisha na ufisadi huo mpya ni kampuni moja ya Afrika Kusini, Benki moja nchini na mawakili wawili wa kampuni moja ya uwakili nchini""
Ikumbukwe kuwa kipindi hicho uchunguzi wa wizi wa fedha za EPA ulikuwa bado haujakamilika ile ripoti ya E&Young ilikuwa haijatolewa.
Sasa mimi nina maswali kadhaa, kwa uchache;
1. Dk Slaa alisema uongo,ili nijue kuwa alichosema ni uongo wafurukutwa na wakereketwa wa CCM niambieni ukweli ili nithibitishe Dk ni mwongo na nimwitwe hivyo.
2. Kwa kuwa uongo haujibiki wanaCCM nipeni ukweli.
3. Ili jamii ukiunge mkono kwa chama chochote ni vizuri kikitoa tuhuma za uongo, kama zile za "tumekamata visu na mapanga vyenye rangi ya chama chao,tunajua wanakusudia kumwaga damu" na "huyu si mtanzania safi wa kwasababu alikuwa mwanachama wa HIZBU"?
4. Katika kampeni za uchaguzi Mkuu 2010, tutarajie vyama vya siasa ikiwemo CCM kusaidiwa na uongo ili vishinde?
Natafakari, niko njia panda, nikitafuta ukweli.
Wakati sakata la wizi wa Benki Kuu linaanza kupigiwa kelele, viongozi wa vyama (CHADEMA,CUF,TLP na NCCR-Mageuzi) walitoa matamko yao kupinga wizi uliofanywa na CCM, kuiba fedha za umma na kuzitumia kwenye kampeni 2005. katika mkutanoi huo Dk Slaa ndiye aliyetamka wazi kuwa kiasi cha shilingi bilioni 10 [kupitia kampuni ya Deep Green] waliiba fedha toka Benki Kuu ili zitumiwe na CCM kwenye kampeni mwaka huo.Tundu Lissu pia alikuwepo wakati viongozi hao wakitoa tamko lao.
Taarifa hizo zilipotolewa na vyombo vya habari vikiwemo gazeti la Mwananchi na ThisDay, Yusufu Makamba,Katibu mkuu wa CCM, alijibu mapigo.
""Katibu Mkuu wa Chama hicho, Yusuf Makamba aliliambia gazeti hili (Mwananchi) jana kuwa tuhuma kwamba CCM kiliiba fedha kwa ajili ya kufanikisha kampeni zake za uchaguzi hazina ukweli wowote.
"Siwezi kutoa ufafanuzi juu ya madai ya uongo. Uongo haujibiki unakaliwa kimya," alisema Makamba.
Alisema wapinzani waliotoa tuhuma hizo walipaswa kuzitoa wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu mwaka 2010 ili jamii iweze kuwaunga mkono, badala ya kuzitoa sasa na kumaliza uongo wote uliotakiwa kutolewa wakati wa uchaguzi huo.
"Uongo huo ungewasaidia kama wangetoa wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu mwaka 2010, sasa wanapoumaliza leo watasema nini kipindi hicho kikifika?" alihoji
Mbali na BoT na CCM, watuhumiwa wengine ambao umoja wa wapinzani umewahusisha na ufisadi huo mpya ni kampuni moja ya Afrika Kusini, Benki moja nchini na mawakili wawili wa kampuni moja ya uwakili nchini""
Ikumbukwe kuwa kipindi hicho uchunguzi wa wizi wa fedha za EPA ulikuwa bado haujakamilika ile ripoti ya E&Young ilikuwa haijatolewa.
Sasa mimi nina maswali kadhaa, kwa uchache;
1. Dk Slaa alisema uongo,ili nijue kuwa alichosema ni uongo wafurukutwa na wakereketwa wa CCM niambieni ukweli ili nithibitishe Dk ni mwongo na nimwitwe hivyo.
2. Kwa kuwa uongo haujibiki wanaCCM nipeni ukweli.
3. Ili jamii ukiunge mkono kwa chama chochote ni vizuri kikitoa tuhuma za uongo, kama zile za "tumekamata visu na mapanga vyenye rangi ya chama chao,tunajua wanakusudia kumwaga damu" na "huyu si mtanzania safi wa kwasababu alikuwa mwanachama wa HIZBU"?
4. Katika kampeni za uchaguzi Mkuu 2010, tutarajie vyama vya siasa ikiwemo CCM kusaidiwa na uongo ili vishinde?
Natafakari, niko njia panda, nikitafuta ukweli.