Kuna mama ana duka la spare za mazda na ford pale tabata. Kama unatoka ubungo, ukishapita mataa yanayokwenda tabata, endelea kama unaenda buguruni angaliaa upande wa pili wa barabara yaani unaotoka buguruni kuja ubungo, utaona kuna kituo cha basi na nyuma/pembezoni mwa hicho kituo kuna duka kubwa la pale blue limeandikwa mazda na ford... Unaweza kupata au kumuagiza akakuletea ndani ya muda mzuri...ila ana bei sana... Anasema vitu vyake vyote ni genuine... (Sina uhakika na siwezi kuthibitisha) japo binafsi nimeshanunua air cleaner ya Mazda MPV...
By the way, hiyo tribute ni auto au manual? Vipi unaweza kunipa mrejesho wake kidogo, kwani nafikiria kuichukua 2.0 manual...ila nikifikiria spare ndio nasita.
Actually mi naendesha ford maverick ambayo ni sawa kabisa na ford escape, ni manual 2.0. Ni gari nzuri kwa kweli,nimesafiri nayo sana sema sasa mashock up hayo yananizingua ila asante sana kwa ushauri
mkuu ulipata spare kwa huyo mama buguruni? na Plan kuagiza Ford escape 2.0 lakini naogopa ishu za spare parts..vipi kwenye ishu ya service oil filter zinaingiliana na gari zingine?
mkuu ulipata spare kwa huyo mama buguruni? na Plan kuagiza Ford escape 2.0 lakini naogopa ishu za spare parts..vipi kwenye ishu ya service oil filter zinaingiliana na gari zingine?
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.