natafuta mtu wa kubadilishana nae kituo cha kazi jamani

Kwa nini hutaki huko Ileje? nakushauri uende tu kwa sababu maisha ni popote. Kikubwa unachotakiwa kikufanya ni kwanza kutochukia mazingira na ukifanikiwa katika hilo utaziona opportuniyies kibao. Kuna watu ambao zamani walikuwa wakikataa kuhamishiwa mikoa ya kusini, baadhi walikubali kwenda. Hivi leo, waler waliokwenda wameji-establish huko kiasi kuwa hawana kabisa wazo la kuhamia sehemu nyingine

Kuna watu wanafanya kosa la kuchukia sehemu kwa kuona jina tu, au kusikia kwa watu.. mimi nadhani huyu bwana/bibi aende tu akapaone kama hapajui.. , kaa muda kidogo then utajua kama mbivu au mbichi .. mimi nilisema wala sitakwenda kufanya kazi Mtwara, nilikuja kwenda nikaona mbona pazuri tu.. Maisha popote jamani
 
mi sijapangwa kabisa kama vipi nigee hiyo nafasi wewe uendelee kusubiri ajira zingine!!
 
Kanuni na taratibu za ajira zinaelekeza kuwa unaweza kufanya kazi eneo lolote Tanzania. Hiyo tabia ya kupenda kukaa mijini tu haifai, kuwa tayari kuishi mazingira yoyote yale, ili siku ukiwa Mwakilishi wa Jimbo lako ukae kijijini kwenu.

sina mpango wa kuwa m,wakilishi wa watu by the way,mie ni mwakilishi wa mimi tu!
 
Jamani naomba kuuliza, ukipangiwa halmashauri fulani, unaweza kubadilishana na mwingne aliyepangiwa sehemu nyingne. Na process znakwendaje?
 
Kuna watu wanafanya kosa la kuchukia sehemu kwa kuona jina tu, au kusikia kwa watu.. mimi nadhani huyu bwana/bibi aende tu akapaone kama hapajui.. , kaa muda kidogo then utajua kama mbivu au mbichi .. mimi nilisema wala sitakwenda kufanya kazi Mtwara, nilikuja kwenda nikaona mbona pazuri tu.. Maisha popote jamani

mkuu mtwara ni mbali watu wanatishiwa na umbali wakati pako mzuka sana
 
jina la mkoa au wilaya visikutishe mkuu,mfano hapa ndani ya jiji la Mwanza kuna sehemu hadi ufike mjini safari yako inaanzia na mwendo wa baiskeli kisha pikipiki baadae basi (leyland daf) ndio unafika mjini, hapo ni wakati wa kiangazi wakati wa mvua mambo ni tofauti....mfano upo Kabusungu.
 
Back
Top Bottom