Natafuta mtu au taasisi ya kuingia nayo ubia(joint venture) katika ujenzi wa apartment

Akiri

JF-Expert Member
Sep 21, 2010
1,445
212
Nina eneo kubwa zaidi ya nusu heka hapa Upanga Dar - Es - Salaam,eneo ni zuri kwa ajiri ya kitega uchumi , kama apartment n.k , eneo lipo kiharali na kila nyaraka muhimu ipo. eneo limezungushiwa ukuta na ndani lina nyumba moja.ni karibu na mjini na linafikika kwa urahisi. kwa aliyetayari tuwasiliane 0657 145555, thomasnelson564@yahoo.com
 
Jaribu kuzungumza na National Housing mbona nasikia wanaingia ubia kujenga nyumba na watu au wanafanya hivyo na wahindi tu?
 
Jaribu kuzungumza na National Housing mbona nasikia wanaingia ubia kujenga nyumba na watu au wanafanya hivyo na wahindi tu?

Unampa Idea halafu hapohapo unamrudisha nyuma kwa kuhisi!!! it's a lack of confidence.
Waswahili wanasema penye nia pana njia,sidhani kama NH wanabagua kwa rangi gani isipokuwa nadhani hutegemea uchumi wako wa kiasi gani pengine huendana na asilimia ngapi ya ubia unahitajika.Ukishakuwa na dhana kichwani mwako basi huwezi kujifanikisha lolote ktk dunia hii,tumia akili yako jenga imani yako na kuwa positive wakati wote u can do it.
 
Jamani bado sijapata mdau wa kufanya naye ubia, sio lazima iwe taasisi hata mtu binafsi anakaribishwa
 
Jamani bado sijapata mdau wa kufanya naye ubia, sio lazima iwe taasisi hata mtu binafsi anakaribishwa

Akiri hebu ifafanue zaidi hii ishu ipo vipi haswa.

Je hiyo nyumba au ardhi ipo kwa jina la nani?
Na ubia wenyewe upo vipi ni 50% au ni ngapi?
Je upo tayari kuandikishana mahakamani?
Na je ubia wenyewe ni kwenye ujenzi tu au ni moja ya kumuuzia na nusu au robo kiwanja?
Nadhani watu wengi wanaweza kupata jibu la haraka kwasababu wengine ni wavivu au hawapendi kumtafuta mtu na pengine wanauwezo wa kipesa.

Labda majibu yanaweza kumuweka mtu sawa kwa alie na uwezo wa kuin-vesti,
 
Akiri hebu ifafanue zaidi hii ishu ipo vipi haswa.

Je hiyo nyumba au ardhi ipo kwa jina la nani?
Na ubia wenyewe upo vipi ni 50% au ni ngapi?
Je upo tayari kuandikishana mahakamani?
Na je ubia wenyewe ni kwenye ujenzi tu au ni moja ya kumuuzia na nusu au robo kiwanja?
Nadhani watu wengi wanaweza kupata jibu la haraka kwasababu wengine ni wavivu au hawapendi kumtafuta mtu na pengine wanauwezo wa kipesa.

Labda majibu yanaweza kumuweka mtu sawa kwa alie na uwezo wa kuin-vesti,

Hii aridhi ipo kwa jina la mmiliki wa eneo ambaye yupo hai, na ndiye aliyenipa kazi ya kumtafutia mbia, yeye anatoa yeye anachangia arithi tu, ( ni jambo ambalo kwa sasa nanafanyika sana hasa maeneo ya kariakoo ambapo kuna mtu anamiliki arithi lakini hana pesa ya kujenga kitega uchumi na wala hataki kuuza eneo lake. na wakati huo kuna mtu ana pesa na kuna eneo karipenda lkn wenye eneo hawauzi sasa wanakubaliana kisheria huyu anatoa arithi na huyu anatoa pesa na kufanikisha ujenzi kwa makubaliano ya kisheria inaweza kuwa miaka 10, 50 , ....)

Mwenye arithi yuko tayari kuandikisha mahari popote ambapo mbia ataona panafaa, ( kwa uzoefu wangu huwa inakuwa kila upande unakuja na mwanasheria wake kisha wanakubaliana na kuandika mkataba)

Huu ubia sio kwenye ujenzi tu, kwa baadhi ya sehemu nilizoona huwa wanakubaliana mfn unaweza jenga majengo 2 makubwa kwenye hiyo arithi na nyumba ikikamilika unaweza wapa sehemu ya nyumba wale wenye arithi,

hapana arithi hii haiuzwi ni kwa ubia tu na hakuna hila yoyote iliyofichika.

Asante na karibu tena
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom