Natafuta mtaalamu wa mambo ya mahusiano, matatizo yangu ni makubwa, tafadhali nisaidieni

Everything happens with a reason; you were tested and you managed the tests. Kwanini ukubali ku-give up when you have just crossed the river? Mmhh, hapana, jipange tena Remember; there is no future in the Past.....and future holds more than One can ever think about. Jishauri mwenyewe maana hata hao wataalamu nao wanayakwako mioyoni mwao and no matter what counselling utakayopata, mwishoni you are the one to decide.........Check na mshkaji mmoja pale UDSM anaitwa Chris Mauki (mumewe mwimbaji fulani wa Gospel Miriam Lukindo yupo School of Education; Kitengo cha Psychology
 
naomba ushauri wenu wana JF mambo yamekuwa kama nilivyoupdate hapo. natanguliza shukrani zangu na nitafurahi kukosolewa.
 
...kitanda unachokilalia ndio unajua kunguni wake.......mawazo ya mbayuwayu sisi,changanya na zako utapata maamuzi sahihi tu
 
ni PM kwa maelezo zaidi

ila kwanza shukuru kuwa pamoja wakati wote .. ila pia aminni wanawaadam hubadilika ,.. kuna nyakati watu wanakuwa limukeni na kufanya mambo ambayo yanakuwa ya maksudi au kwa kutokuelewa au kutoelewa tahamni yake na ya mwenzake. hivyo kwa wewe naelewa moyo wako umeingia ukakasi juu ya mwenzi wako na hiyo itapelekea kutoweza kulidhika kwa lolote na hasa unapoweka chuki zaidi utamchukia ..

nini unatakiwa kufanya
  1. jitahidi sana kukaa nae na kuongea nae kama rafiki
  2. kuwa nae karibu zaidi ili uweze kumwelewa zaidi
  3. amini kwamba yeye ndio chaguo
  4. mshirikishe kwenye masuala ya familia na ujitahidi awe kama mtendaji mkuu wa familia
ila kama humhitaji
  1. kuwa nae karibu kwa ajili ya malezi ya watotot
  2. usimbague
  3. ongea nae na umweke wazi
 
Wewe umeshapata mwingine anaesuuza roho yako ndo maana una sema 'not sure' ungesema No! Ningekuelewa. Shika ulicho nacho.
 
All I can say ni pole. Mwamuzi ni wewe mwenyewe; mambo ya ndoa hayanaga ushauri.

Kuna watu walishauriwa waondoke kwenye abusive marriage hawakusikia lakini unashangaa inatokea siku ghafla bila hata ku consult mtu mwanamke anafungasha virango. Asikwambie mtu hayo maamuzi ni very personal.

Hata wewe si umesema nduguzo walikwambia uchape lapa hukuwasikia. Maamuzi siku zote ni yako. Ikifika siku ya siku kama it was never meant to be utashangaa una chapa lapa bila kumtaharifu mtu.

Kama si wa kuchapa lapa hata ushauriwe na shehe au padri hutasikia utabaki kwenye ndoa yako.

Sharing najua inapunguza stress lakini haisaidii kuamua.
 
Jf memberz especial mmu wapo poa, watakusaidia matatizo yao just kuwa na subira! Pole kwa yote!
 
Tutor B; ]Achana na huyo Bwana hata kama akijiua. Mtu ambaye alikuwa akikusumbua hupaswi kuendelea kumbembeleza. We tafuta kidume kingine ambacho utakuwwa unakipenda kikupe raha. Usijinyime raha maisha ni mafupi ndg yangu. Habari ndo hiyo. Kama vipi tukutane kwenye private.

Mkuu Umeoa/Umeolewa? Wewe ndo wale watu wazima hovyo.... mtu anaomba ushauri jinsi ya kuijenga ndoa yake wewe unampa wa kubomoa. AKiondoka kwa huyo mumewe watoto utawalea wewe? Umeshindwa kutafuta mabinti mtaani unataka wake wa watu walio na matatizo,.... atajuwaje kama akija kwako hutamtesa pia? Dunia hii ingekuwa na watu wote kama wewe ingekuwa hasara kubwa sana kwa Mwenyezi Mungu..lol
 
muombe Mungu yote atakuonyesha maana kwake hakuna gumu yote yanawezekana atakupatia faraja na amani ndani ya ndoa yako
 
This subject is very painful but almost 50% ya wanawake wanateseka, na wasioteseka wanaboreka na mahusiano yao for whatever reasons e.g. jamaa mpole sana, haongei, anasoma magazeti tu, anapenda kazi, anapenda kusali, anasafiri sana, anamsikiliza mamake zaidi ya mimi and many more... sijui ni aslimia ngapi that are happily married for over 3 years
 
Mimi ni wife niliyewahi kutendwa mno na hubby wangu for the past 5 yrs yani alikuwa hasikii wala haoni kifupi hakunijali hata, na mungu alinijalia moyo wa kuyavumilia mengi mno(cheating zaidi) japo niliambulia ulcers na BP na wala hakujali. sasa ukafikia wakati mwanzoni mwaka huu moyo ukakataa kabisa yani najitahidi kuwa na hisia za mapenzi na huyu mme wangu lakini wapi yale yote ya nyuma yanajirudia!! sasa ndio kashtuka na mimi moyo umegoma kabisaaaaa yani yeye ndio amekuwa kama mimi nilivyokuwa zamani yani hatulii kwa wivu na kuumwa roho lakini mimi mapenzi kushney nikimuangalia najiuliza hivi nilimpendea nini?? namuonea huruma anavyohangaika lakini roho yangu haitaki tena, nahitaji mtaalamu anishauri sijui kama nataka hii ndoa au siitaki kifupi sijielewi ila najua kuwa mapenzi ya hisia kutoka kwangu kwenda kwa mwenzangu hakuna, japo simchukii namuona kama ndugu yangu hivi.

UPDATE:
Baada ya hapa nilipata vituko zaidi vya huyu bwana, mambo ya wanawake na nikamface na kumueleza l
 
ashangedere awe mkweli ama muongo mie sijui. Ila kisa chake kinawapata wengi hata mie nilifikwa na hali hiyo. Ni kama ameniwakilisha. Kilichonisaidia kurudi ktk upendo ni mtaalamu mmoja na katunga kitabu kiitwacho Ndoa yangu ningejua, nilipokisoma kilinichoma sana. Kitafute na ukimtaka sema nikupe namba zake
 
ashangedere awe mkweli ama muongo mie sijui. Ila kisa chake kinawapata wengi hata mie nilifikwa na hali hiyo. Ni kama ameniwakilisha. Kilichonisaidia kurudi ktk upendo ni mtaalamu mmoja na katunga kitabu kiitwacho Ndoa yangu ningejua, nilipokisoma kilinichoma sana. Kitafute na ukimtaka sema nikupe namba zake
Tafadhali naomba umipatie namba zake
 
ashangedere awe mkweli ama muongo mie sijui. Ila kisa chake kinawapata wengi hata mie nilifikwa na hali hiyo. Ni kama ameniwakilisha. Kilichonisaidia kurudi ktk upendo ni mtaalamu mmoja na katunga kitabu kiitwacho Ndoa yangu ningejua, nilipokisoma kilinichoma sana. Kitafute na ukimtaka sema nikupe namba zake

Kimetungwa na nani?
 
Pole sana mdada,unatakiwa kumsamehe kabisa na jaribu kutoa mauchungu yote yaliyoko moyoni mwako.Pia jaribu kutafuta jambo jema na zuri alilowahi kukufanyia hasa ule upendo uliokuwepo kabla ya ndoa.Amebadilika kwa sababu amekwishatambua amekukosea sana ila tu hawezi kusema samahani.

Ni ngumu! nie mnasema tu kama hayajakukuta unaweza kudhani ni rahisi
 
Kuna sredi ilitolewa hapa kama sijasahau sana taito yake inasema ''what made you stay" (niko tayari kukosolewa), hebu itafute uisome yaweza kukusaidia katika kufanya maamuzi yako sahihi. Nakuombea Mungu akufanyie wepesi katika safari yako ya maamuzi.
 
Pole sana ,
muda wote umemuomba mungu amfanye mumeo awe mpole leo amekua mpole hutaki tena kuwa naye ?
Huwa maisha yanabadilika na kama mna watoto vumilieni tu kwani mtawatesa watoto wenu .
Jitahidi kukaa naye zungumzeni kuhusu uhusiano wenu ninyi wenyewe muone kama mlivyoanza mipango yenu ilikuaje
halafu utajua ni ninin cha kufanya la sivyo hili litakua tatizo kubwa hasa kwa watoto wenu.


"MWANAMKE MWENYE AKILI HUIJENGA NYUMBA YAKE MWENYEWE BAL ASIYE NAYO HUIVUNJA KWA MIKONO YAKE"
 
Mimi ni wife niliyewahi kutendwa mno na hubby wangu for the past 5 yrs yani alikuwa hasikii wala haoni kifupi hakunijali hata, na mungu alinijalia moyo wa kuyavumilia mengi mno(cheating zaidi) japo niliambulia ulcers na BP na wala hakujali. sasa ukafikia wakati mwanzoni mwaka huu moyo ukakataa kabisa yani najitahidi kuwa na hisia za mapenzi na huyu mme wangu lakini wapi yale yote ya nyuma yanajirudia!! sasa ndio kashtuka na mimi moyo umegoma kabisaaaaa yani yeye ndio amekuwa kama mimi nilivyokuwa zamani yani hatulii kwa wivu na kuumwa roho lakini mimi mapenzi kushney nikimuangalia najiuliza hivi nilimpendea nini?? namuonea huruma anavyohangaika lakini roho yangu haitaki tena, nahitaji mtaalamu anishauri sijui kama nataka hii ndoa au siitaki kifupi sijielewi ila najua kuwa mapenzi ya hisia kutoka kwangu kwenda kwa mwenzangu hakuna, japo simchukii namuona kama ndugu yangu hivi.

UPDATE:
Baada ya hapa nilipata vituko zaidi vya huyu bwana, mambo ya wanawake na nikamface na kumueleza live kuwa simfeel tena kila mtu akae chumba chake, tulikuwa wawili tu, basi niliambulia kipigo mwenzenu na ndugu zangu walipoingilia wakatukananwaaa ukoo wote. kwa hiyo issue imekuwa kubwa ndugu zangu hawampendi na wananiambia niondoke ataniua na kipigo au ukimwi. Kama kawaida yake kawa tena mpole na kulia juu anadai harudii tena kunipiga ni kama mara ya nne hii katika hii miaka 5. yani kawa mpole anajifanya baba wa familia, lakini mimi nahisi kipato ndio kinachangia aogope kuachana na mimi kwani hapo nyuma kipato changu kilikuwa kidogo na tulikuwa tukigombana tu ananiambia kama vipi tuachane, sikuhizi maisha yetu yamebadilika sababu ya kipato changu tuna mahitaji yote muhimu kwa maisha ya dar nyumba gari etc basi nahisi labda anaogopa maisha ya peke yake na ninamuonea huruma kwa hilo kwani kipato chake kidogo sana. Zaidi mwenzangu huyu ni muongo katika mambo mengi na anakopakopa hovyo halafu halipi nakuja kudaiwa mimi , lakini kizuri anawapenda wanae sana kuongea nao kucheza nao na yeye wanampenda sana na ndio kitu kinanifanya nisite kuamua. JE kunauwezekano wa mimi kuishi nae nyumba moja lakini kila mmoja awe na chumba chake kisheria? sitaki kutengana nae kwani yeye atapata tabu na watoto pia, pia nimekubali siwezi kumchunga na ninataka afanye mambo yake kwa uhuru ila asiniletee wanawake hapo nyumbani, tatu hiyo italeta amani kwani mimi nitakuwa happy sababu simfeel kimapenzi tena na yeye pia, ushauri tafadhali.

sitaki kutengana nae kwani yeye atapata tabu na watoto pia,

Mkwe wangu nilikuwa na soma na nilijua mwisho utaitimisha na haya maneno na kama kuna mwenye akili timamu atotoa wazo lolote maana umeshamaliza tatizo ..labda hilo la kuishi chumba kingine kisheria..binafsi sijawahikuonahili ila nitapendekeza wachungaji waongeze haya maneno
wakati watu wakila kiapo
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom