Kigugumizi (Stuttering): Chanzo na Tiba kwa watu wazima na watoto

Usikute ni agano baya la kipepo walifanya wazazi mababu na mababu, kataa hilo agano huku ukiomba na kusema navunja agano na shetani likome kizazi na kizazi chako kijacho katika jina la YESU
 
Usikute ni agano baya la kipepo walifanya wazazi mababu na mababu, kataa hilo agano huku ukiomba na kusema navunja agano na shetani likome kizazi na kizazi chako kijacho katika jina la YESU

Amen ön high Gaga. Wil definately do it. Thanks
 
Aaaaaamen!
Usikute ni agano baya la kipepo walifanya wazazi mababu na mababu, kataa hilo agano huku ukiomba na kusema navunja agano na shetani likome kizazi na kizazi chako kijacho katika jina la YESU
 
Uko BONGO au ULAYA ,.?mtafute SPEECH THERAPIST,.huyo ana elimu ya kuwasaidia watu kama hao,.hata mabubu,wenye vithemi,waliozaliwa na midomo ya sungura[cleft palate] na watu waliopatatwa na stroke pia,.kwa bahati mbaya kwa Tazania to the best of my knowladge hayupo,.aliyekuwepo aliondoka,..mdogo wangu aliyepo marekani alihudhuria mafunzo yake na sasa hivi anaongea vizuri
 
Ushauri ninaoweza kukupa ambao utapunguza taratibu kigugumizi cha mtoto wako ni huu:
1. Wakati anapozungumza na kukwama, asitokee mtu kutaka kumkwamua kwa kumalizia neno aliloanza. Mwacheni ajitahidi mwenyewe hata kama itapita dakika nzima.

Kumsaidia/kumkwamua kunamfanya ajihisi vibaya na kisaikolojia hii inamuathiri kwa kuhisi kuwa "hana anachokijuwa). Hapa itawabidi uwaeleze wanafamilia wote na watu wanaomzunguka wasimsahihishe, wasimsaidie, wasimkwamue. Ikiwa yuko nursery zungumza na walimu wake tatizo lake na wao wachangie therapy hii.

2. Muda wote muonesho upendo, muwache kumkemea hasa akiwa yumo katika juhudi za kutaka kutamka neno. Kisaikolojia nayo hii inamfanya awe moga, aone haya kusema na inapunguza kujiamini kwake.

3. Anapokwama muda mrefu na baadaye kujikwamua mwenyewe, apongezwe badala ya kukemewa au kupuuzwa.

4. Kama utakuwa umechunguza, mtu mwenye kigugumizi hupungua au hutoweka kabisa wakati anaimba. Mnunulie/mtafutie nyimbo za kitoto na watu wa familia wawe wanaimba naye mara kwa mara. Hata michezo ya kitoto iliyo na nyimbo ndani yake inasaidia sana.

5. Njia nyengine ambayo nimeona kwenye filamu ya karibuni inayoitwa Hotuba ya Mfalme "The King's Speach" inayohusu mfalme mwenye kigugumizi ni kusoma kipande cha habari wakati mtu akiwa anasikiliza mziki kwa sauti ya juu kidogo. (Tahadhari isiwe sauti kubwa sana kiasi cha kuumiza masikio).

Hii ni kwa sababu mtu mwenye kigugumizi huwa anajisikiliza sauti yake wakati anapozungumza, kwa hiyo akiwa anasikiliza mziki huku anasema huwa hasikii sauti yake na hufanya juhudi ya kushindana mziki ili ajisikie. Njia hii ni nzuri zaidi kwa watu wazima, sijui kama kwa watoto wadogo wasiojua hata kusoma inaweza kufaa.
 
Kuna tafauti baina ya dawa na tiba.
Dawa kwa maana ya vidonge zipo: benzodiazepines, anti-convulsanta, anti-pressants, antipsychotic na antihypetensive (Nimeziona hizi kutoka Wikipedia, lakini mti akiamua kutumia dawa SIKU ZOTE IWE NI KWA USHAURI WA DAKTARI.

Tiba za kigugumizi ni pamoja na baadhi nilizozieleza ambazo ni pamoja na mazoezi ya kuzungumza, mbinu za kudhibiti kigugumizi, ukaribu, upole na mapenzi.

Kwa kawaida watoto wote wanaanza kuongea kwa kigugumizi, na kawaida kinaondoka wenyewe mtoto anapofikia miaka 5 ikiwa sio cha kurithi au sababu nyengine. Ukipita muda huu ndipo mzazi unapaswa kuhangaika kutafuta ufumbuzi.

Cha kufanya si kukata tamaa. Tunaweza kupata mengi kwa kutumia wavuti husika, ushauri na kubadilishana maoni na wazazi wenye matatizo kama haya pamoja na kuwaona wataalamu wa mogonjwa ya sauti (Speach pathologists)
 
Uko BONGO au ULAYA ,.?mtafute SPEECH THERAPIST,.huyo ana elimu ya kuwasaidia watu kama hao,.hata mabubu,wenye vithemi,waliozaliwa na midomo ya sungura[cleft palate] na watu waliopatatwa na stroke pia,.kwa bahati mbaya kwa Tazania to the best of my knowladge hayupo,.aliyekuwepo aliondoka,..mdogo wangu aliyepo marekani alihudhuria mafunzo yake na sasa hivi anaongea vizuri

Bawa, thanks, niko bongo, nilipanga kununua dvd za hi therapy. Nasikia huwa ni user friendly. Kasheshe ni kwenye hapa kilugha cha ughaibuni
 
Ushauri ninaoweza kukupa ambao utapunguza taratibu kigugumizi cha mtoto wako ni huu:
1. Wakati anapozungumza na kukwama, asitokee mtu kutaka kumkwamua kwa kumalizia neno aliloanza. Mwacheni ajitahidi mwenyewe hata kama itapita dakika nzima. Kumsaidia/kumkwamua kunamfanya ajihisi vibaya na kisaikolojia hii inamuathiri kwa kuhisi kuwa "hana anachokijuwa)...

Mamamia, asante mno, what a piece of advice! I should keep reading ur post for my own good. Asante sana
 
Kuna tafauti baina ya dawa na tiba.
Dawa kwa maana ya vidonge zipo: benzodiazepines, anti-convulsanta, anti-pressants, antipsychotic na antihypetensive (Nimeziona hizi kutoka Wikipedia, lakini mti akiamua kutumia dawa SIKU ZOTE IWE NI KWA USHAURI WA DAKTARI...

Mamamia, again i say thank you! Asante kwa huduma yako
 
Mamamia thx for ur advice, na raia fulani don't just generalize kwa kusema hakina dawa,

Pia mwanangu alipoanza kuongea alikuwa nacho bahati nzuri watoto wadogo walikuwa wengi mtaani kwetu na walipenda sana kuimba, basi tulishahama ila kiliisha kabisa, sijui ni zile nyimbo ama ni nini?
Namshukuru Mungu
 
Mamamia thx for ur advice, na raia fulani don't just generalize kwa kusema hakina dawa,

Pia mwanangu alipoanza kuongea alikuwa nacho bahati nzuri watoto wadogo walikuwa wengi mtaani kwetu na walipenda sana kuimba, basi tulishahama ila kiliisha kabisa, sijui ni zile nyimbo ama ni nini?
Namshukuru Mungu

Nsiande, namshukuru Mungu kwa ajili ya upönyaji wa mtoto wako.
 
Pole sana, najua unavyojisikia ksb nami nilikuwa mhanga wa tatizo hili.

Mwanangu alikuwa na kigugumizi kikali kweli (anajipiga mikono au kichwa anainama na kuinuka mpaka ) mimi nilikuwa najihisi kulia, nilikosa amani hata nilipompeleka shule,nilimwambia mwalimu wake tatizo lake, bahati nzuri yule mwalimu wake alipokuwa mdogo naye alikuwa na tatizo kama la mwanangu akanambia wala nisijali atakwenda naye vizuri tu wala nisiwe na wasiwasi.

Alichonisisitiza ni kama ushauri alioutoa mammamia hasa wa kumsikiliza na kutokumkatisha pindi anapoongea au kumalizia neno lake. Nilizingatia yooote na kuyafanyia kazi, hivi ninavyoandika nina furaha sana mwanangu hana tena kigugumizi na wala sijui hasa ni siku gani kimemwisha, muda si mrefu atatimiza sita, japo alidumu nacho kwa karibia miaka mitano
fuata hayo naamini kigugumizi kitamwisha mwanao itabaki historia tu,pole sana......
 
Pole sana, najua unavyojisikia ksb nami nilikuwa mhanga wa tatizo hili.

Mwanangu alikuwa na kigugumizi kikali kweli (anajipiga mikono au kichwa anainama na kuinuka mpaka ) mimi nilikuwa najihisi kulia, nilikosa amani hata nilipompeleka shule,nilimwambia mwalimu wake tatizo lake, bahati nzuri yule mwalimu wake alipokuwa mdogo naye alikuwa na tatizo kama la mwanangu akanambia wala nisijali atakwenda naye vizuri tu wala nisiwe na wasiwasi..

NNUNU, nashukuru sana kwa pole. Honestly! Asante pia kwa ushuhuda wako. Ushuhuda huu unanitia matumaini, mamamia ushauri wake unazingatiwa. Amina
 
Kuna speech therapist mmoja ambaye yupo kcmc hospital na kwa maelezo ndie pekee tanzania ukiacha hawa wanaokuja kama visitors. Kama utapenda kumuona waweza kumtafuta huyo.

Mtoto mwenye kigugumizi anahitaji kupewa muda zaidi wa kujieleza na kumsikiliza, mara nyingi kinapanda akiwa na furaha, huzuni au akiwa na hamu ya kuongea jambo.

Unaweza kuanza nae mazoezi nyumbani kwa kumpa muda wakuongea na usimuharakishe pia onyesha kuwa uko interested na kile anachoongea, mfanye ajiamini. Ukionana na mtaalamu utapata ushauri zaidi
 
Nakubaliana na wadau wanosema kigugumizi si urithi. Nimewahi soma kwenye mtandao kuwa wazazi kama wana kigugumizi mtoto anaiga kwani anajua hivyo ndivyo anavyopaswa kuzungumza yaani ni kama vile mtu anapoiga lafudhi fulani tokana na mazingira.

Kwa hiyo nina imani mnaweza kumtrain mtoto wenu kuzungumza straight mkizingatia ushauri mliopewa na wadau. Na kingine jitahidini asijue kama ana upungufu kwenye kuzungumza kwani mtamfanya asiwe na confidence.
 
Kigugumizi hakirithiwi ila kinaigwa. Kinapanda zaidi akiwa na hasira,furaha au shauku ya kueleza kitu. Mpe muda wa kutosha akiongea,usimkatishe wala kumuonyesha kuwa ana tatizo. Kwa umri wake ana uwezo wa kuacha kama ata interact na watoto wenzie wanaoongea kawaida.
 
Naona mdau Ennie hapo juu na wewe umeshasikia kuwa kigugumizi hakirithi kinaigwa. NAdhani kama kuna uwezekano mtoto aende akakae na ndugu zenu kwa muda ambao hawana hilo tatizo ili awe kwenye mazingira ya watu wasio na hilo tatizo ataongea tu vizuri.
 
Kigugumizi hakirithiwi ila kinaigwa. Kinapanda zaidi akiwa na hasira,furaha au shauku ya kueleza kitu. Mpe muda wa kutosha akiongea,usimkatishe wala kumuonyesha kuwa ana tatizo. Kwa umri wake ana uwezo wa kuacha kama ata interact na watoto wenzie wanaoongea kawaida.

Nakubaliana na wewe. Mwanangu nilishangaa ameacha kigugumizi bila hata kujua. Halafu mtoa mada lazima atambue kuwa watoto wengi huwa wanakuwa na kigugumizi halafu baadaye huwa kinapotea tu.
 
Tatizo la kikgugumizi kwa asilimia kubwa linasababishwa na genetics (kurithi toka kizazi kimoja hadi kingine) kwa mtu mzima ni vigumu kupona kabisa japo linaweza kupungua. ila kwa mtoto wa kuanzia miaka 2-6 anaweza kupona...kwa msaada wasiliana na wataalamu wa saikolojia kupitia psychologicalsupport@hotmail.com kwani hilo sio tatizo la kibiolojia kusema daktari atampa dawa apone ila.. ni speech development ambapo ni la kisaikolojia zaidi.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom