Natafuta ardhi ya kilimo ya bei nafuu

kanyagio

JF-Expert Member
Dec 10, 2009
1,021
365
Ndugu wajumbe, nimekuwa nikifikiria sana kuhusu kilimo na kuona kinaweza kulipa hasa ukizingatia kuwa kwa sasa kuna kilimo kwanza (naamini kuna upande mzuri wa huo mkakati). kwa sasa nimeanza kidogooooo kulima miti ya mbao wilaya ya Bagamoyo. nimepata ka-adhi kadogo kama ekari tano kwa ajili ya kupanda miti na nimeshapanda mitiki.

kwa sasa nataka kupanuka na kununua ardhi kubwa kwa ajili ya kilimo kikubwa. kwa msingi huu ninaomba msaada wenu kuhusu masuala haya:

  1. Wapi ninaweza kupata ardhi ya bei nafuu sijalishi mkoa, ila angalau eneo liwe linafikika kwa usafiri wa gari na kuna rutuba na source ya maji (specificity is needed)
  2. Je bei ya mashamba ni kiasi gani? on average?
  3. Je kwa sasa kilimo gani kinalipa kwa kuzingatia huitaji inputs kubwa.
naomba jamani mnisaidie katika hili jamani.
nawasilisha
 
Kanyagio taratibu tu usiwe na wasi humu kuna watu waliobobea kwenye mambo hayo utashindwa wewe tu. Labda nikuulize kidogo unapanga kulima nini zaidi ya mitiki maana kila mkoa una hali ya hewa na mahitaji tofauti na mwingine. Ukishajua hilo ndipo inakuwa rahisi kukadilia bei ya shamba kutokana na eneo unalopendekeza.

......................................

Amani yetu inatumiwa vibaya
 
Kanyagio taratibu tu usiwe na wasi humu kuna watu waliobobea kwenye mambo hayo utashindwa wewe tu. Labda nikuulize kidogo unapanga kulima nini zaidi ya mitiki maana kila mkoa una hali ya hewa na mahitaji tofauti na mwingine. Ukishajua hilo ndipo inakuwa rahisi kukadilia bei ya shamba kutokana na eneo unalopendekeza.

......................................

Amani yetu inatumiwa vibaya

Nenda kwenye point moja kwa moja,kama vile nataka kulima ulezi, nitapata shamba wapi? au kama unataka kupanda mitiki jamani wapi pazuri ili tukusaidie mkuu. Karibu.
 
Mitiki inasitawi vizuri Mheza tanga! Kwa vile kuna shamba la serikali la mitiki huku upatikanaji wa vipando ni rahisi na pia kama utahitaji ushauri wa kitaalamu kuna watalaamu wapo huko!
Pia kilimo cha mpunga kinalipa sana, tafuta mashamba Morogoro hasa wilaya ya Ifakara kwenye bonde la mto rufiji!
 
Mitiki inasitawi vizuri Mheza tanga! Kwa vile kuna shamba la serikali la mitiki huku upatikanaji wa vipando ni rahisi na pia kama utahitaji ushauri wa kitaalamu kuna watalaamu wapo huko!
Pia kilimo cha mpunga kinalipa sana, tafuta mashamba Morogoro hasa wilaya ya Ifakara kwenye bonde la mto rufiji!

Mkuu safi sana, ila Ifakara sio Wilaya, Kilombero pia kuna mashamba ya mitiki makubwa kuliko Tanga,na kiwanda cha kwanza kwa ajili ya mbao za mitiki kitajengwa Ifakara.
 
Wakuu natafuta sana ushauri maana nataka kupanda ile miti ya muda mfupi, say 4-5 years nivune; ni ya aina gani na ardhi ipi inafaa?
Je alizeti inastawi mkuranga?
 
Wakuu natafuta sana ushauri maana nataka kupanda ile miti ya muda mfupi, say 4-5 years nivune; ni ya aina gani na ardhi ipi inafaa?
Je alizeti inastawi mkuranga?

Kimsingi miti ya kuvuna ndani ya miaka hiyo unayosema kwa Tz haipo,labda milonge,au kama unataka kupanda mitiki/milingoti(saligna au grandis) ili uvune kama boriti unaweza, itabidi utafute ardhi yenye maji mengi. Lakini kama unakusudia kuvuna kama mbao,hiyo miti haipo.

Kuna taasisi moja ya Uingereza inafanya mipango ya kuleta pines za miaka 5 kule Kilolo inaitwa NEW FOREST,lakini mbegu hizo ni za maabara,na ni mahsusi kwa ajili ya pulp. Je ukikosa mnunuzi wa pulp utafanyaje mkuu? Kwa sasa mbegu hiyo ya Pulp ipo,ila kuwa makini.

Aliozeti zinamea sehemu kubwa ya Mkuranga,tatizo ukame mkuu wangu. Ila kata ya Talawanda kule Bagamoyo kuna ardhi nzuri kwa alizeti.
 
Mitiki inasitawi vizuri Mheza tanga! Kwa vile kuna shamba la serikali la mitiki huku upatikanaji wa vipando ni rahisi na pia kama utahitaji ushauri wa kitaalamu kuna watalaamu wapo huko!
Pia kilimo cha mpunga kinalipa sana, tafuta mashamba Morogoro hasa wilaya ya Ifakara kwenye bonde la mto rufiji!

EfraizMteman, nashukuru sana kwa taarifa uliyotoa. je huko muheza una taarifa kama mashamba ya kununua yanapatikana. Pia nimefurahi kwa wazo lako kuhusu kilipo cha mpunga Morogoro/Ifakara. kama una taarifa na bei ya mashamba ya huko naomba unijuze!!!
naona tunaelekea kuzuri!!!
 
Kimsingi miti ya kuvuna ndani ya miaka hiyo unayosema kwa Tz haipo,labda milonge,au kama unataka kupanda mitiki/milingoti(saligna au grandis) ili uvune kama boriti unaweza, itabidi utafute ardhi yenye maji mengi. Lakini kama unakusudia kuvuna kama mbao,hiyo miti haipo.

Kuna taasisi moja ya Uingereza inafanya mipango ya kuleta pines za miaka 5 kule Kilolo inaitwa NEW FOREST,lakini mbegu hizo ni za maabara,na ni mahsusi kwa ajili ya pulp. Je ukikosa mnunuzi wa pulp utafanyaje mkuu? Kwa sasa mbegu hiyo ya Pulp ipo,ila kuwa makini.

Aliozeti zinamea sehemu kubwa ya Mkuranga,tatizo ukame mkuu wangu. Ila kata ya Talawanda kule Bagamoyo kuna ardhi nzuri kwa alizeti.
nani anafahamu jina la kitalamu la mitiki ili niweze kutafuta taarifa zake hapa kwenye Google
 
kama unatafuta mashamba kwa ajili ya kilimo unachotegemea kuanza nenda Tanga wilaya inaitwa Kilindi kuna mashamba ya bei nafuu sana ushindwe mwenyewe tu, ila pia ujue sehemu ambayo kuna ardhi yenye rutuba wakati wa masika miundo mbinu huwa ni mibovu, kazi kwako. Pia Mheza kuna jamaa yangu kapata ekari 100 kwa milioni 10.
 
Je kilindi ni kilimo aina gani kinakubali? aidha, nimesikia baadhi ya members wanaongelea samaki wa kufuga,... naomba msaada wenu kupata maelezo zaidi katika hili..
 
Je kilindi ni kilimo aina gani kinakubali? aidha, nimesikia baadhi ya members wanaongelea samaki wa kufuga,... naomba msaada wenu kupata maelezo zaidi katika hili..

Kilindi kuna kilimo cha nafaka na matunda. Kama unataka mambo ya samaki fuatilia thread ya bwawa la samaki,kuna mjumbe alijitolea kutusaidia ili tumpate mtalaamu husika. soma hiyo thread.
 
Kilindi kuna kilimo cha nafaka na matunda. Kama unataka mambo ya samaki fuatilia thread ya bwawa la samaki,kuna mjumbe alijitolea kutusaidia ili tumpate mtalaamu husika. soma hiyo thread.

nimesoma hiyo thread ya bwawa la samaki kwa kweli ina maelezo mazuri
 
Nawashukuru wote kwa msaada mliotoa nimepata mwanga sana kwa kuzingatia maoni yenu naona muheza na iringa kilimo cha miti inafaa sana.pia it seems mkuranga,kibaha, bagamoyo na nkuranga ni strategic kwa kilimo though maeneo kadhaa mazuri yameshatwaliwa.
Nilikuwa napiga stories na wakenya fulani, it seems wanaimezea sana ardhi ya tz.
Kwa kuwa na mimi nimeamua kuingia kwenye kilimo nikitumia kamshahara kangu kama capital naamini mawzo yote niliyopata hapa yatanifaha sana. I want to get something i have never get by doing what i have never done.
 
kama nnataka mali mtaipata shambani

Mkuu na mimi ni mpenzi wa kilimo, vizuri pia wakulima wachanga wakafahamiana wakapeana mawaidha huenda ujirani mwema kwenye kilimo ni nguvu ya maendeleo.
Tuwasiliane basi mkuu kama utaona ni vyema tukayatafute mashamba pamoja. Ni ushauri wangu na wazo. Asante
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom