Nassari afyatuka: Kama maji hatuna flyover za nini?

...CHADEMA hakuna walichotekeleza kwa yale waliyohahidi majimboni mwao wakati wa kampeni mwaka 2010,kama kuna mtu anabisha ataje jina la mbunge wa chadema ,jimbo atakalo na kero alizohaidi kuzitatua na ambao tayari zimetatuliwa mpaka sasa, wananchi wanahoji sana huku mtaani ikibidi nawashauri wabunge wa chadema mfanye mikutano majimboni mwenu muwaambie wananchi ni ahadi ngapi mmeshazitekeleza kati ya zile mlizoahidi wakati wa kampeni za uchaguzi mwaka 2010, watu wamechoka makelele yenu mnaropoka sana vitendo zero!
Panadol;
Umesahau kitu kimoja;
Wabunge wengi walio mahiri ndani ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, wanafanya kazi kama wabunge wa Taifa kwa ujumla na si kama wa majimbo yao ya uchaguzi kule ambako walipigiwa kura.

Tusipokuwa waangalifu tutakuja kupoteza wabunge wa maana sana kwenye chaguzi zionazofuata simply tuna-assess delivery yao kijimbo zaidi kuliko kitaifa. Naomba hili kosa tusije tukalifanya
.

Na ukiangalia vizuri, baadhi ya wabunge ambao concentration yao kubwa sana ni kwenye majimbo yao ya uchaguzi tu, wengi wao hawana tija kitaifa na wako pale kwa ajili ya kujiimarisha majimboni ili wawe na uhakika wa kurudi kwenye chaguzi zinazofuata.

Hata, hivyo, kuna baadhi ambao wana uwezo mkubwa wa kumudu vyote viwili vizuri sana, yaani majimboni kwao na kitaifa kwa ujumla, nawapa hongera zao!
 
Hii ndi faida ya kuchagua vijana wa mission town. Huyu bora amtafute sugu wafanye show nyingine.

kwani kwenye point yake haukuelewa nini? Sidhani kama una kichwa kigumu kiasi hiki!
Kati ya maji na barabara kipi kitangulie?

Nassari anaona ni bora tuhakikishe tunapata maji kwanza alaf barabara zitafuata!

Wewe unaonaje?
 
JAMANI MAJI MAJI MAJI NI KITU MUHIMU MNO....NASSARI ANAJITAHIDI JAMANI.ONGEZA JUHUDI NASSARI..USIROPOKE ..WEWE MWAGA POINT TUNAKUKUBALI..USIWE KAMA MCHEMBA aka chemba chafu
 
Asante Lunyungu, ndo nataka kumwonesha huyo aliyeleta hiyo hoja dhaifu ya maji hapa, tulitakiwa kuzungumzia maendeleo maji sio maendeleo ni basic need, kama mpaka leo tunajadili maji maana yake WAO M kazi imeshawashinda siku nyingi...

Unawezaje kuwa na maendeleo bila basic need?hebu nifafanulie kidogo hapo mkuu.
 
Last edited by a moderator:
wakuu nimemsikiliza nasari muda mfupi uliopita alichosema kweli kina manufaa tunataka fly overs barabara nne nne na madaraja ya kifahali wakati huduma ya msingi hasa na maji kwa wananchi hawana tujadili
nahuduma za afya ni mbovu kabisa yani sijui wana akili gani ila waziri wa afya yuko kimya kabisa kila mtu si ana wizara yake?
 
Huyo Nassari hajuwi uchumi ni nini.

Ikiwa Dar ina wakazi million 5 na kati yao million 1 wanapoteza masaa 4 kila siku barabarani ina maana kwa siku wanapoteza miaka zaidi ya 365 na ukiwapunguzia nusu ya huo muda wanaopoteza njiani ina maana una faida ya miaka 182. Na kila unapowacha hilo tatizo huo muda haupunguwi unazidi.

Toka na pumba zako za kijinga,hujui shida ya maji wanayopata watu ndio maana unalopoka hovyo,unajifanya unatetea ujinga wakati ndugu zako wanapata tabu.
 
Huyu jamaa wakati akigombea ubunge kwenye kampeni zake alihaidi kutatua kero mbalimbali za wananchi kama wakimchagua yeye kero zao zitatatuliwa sasa atatue asilalamike kama ameshindwa ajiuzulu ubunge,CCM mwaka 2010 ilikuwa na ilani yake ya uchaguzi iliinadi nchi nzima na wananchi wakaikubali ndiyo maana waliichagua sasa hasiipangie CCM cha kufanya haiache itekeleze ahadi zilizomo kwenye ilani yake ikiwemo ahadi ya ujenzi wa Flyovers,...

Ukitulia kidogo utagundua kuwa ahadi za vyama vya siasa zilikuwa na uhusiano na "party manifestos". Ndio maana unasikia sana "Ilani ya Uchaguzi ya CCM" kama dira ya mipango ya serikali. Mwaka 2010 kila chama na wagombea walikuwa na ushawishi ili wapewe dhamana ya kutekeleza Manifestos hizo.

Sielewi unataka nini:
a) Kwamba mbunge asizungumzie jambo lolote isipokuwa la jimbo lake tu?
b) Kwamba mbunge asiongelee kitu chochote kwa sababu chama chake hakikishinda uchaguzi wa 2010?
c) kwamba mbunge atumie fedha zake binafsi kutatua matatizo ya maji, elimu, barabara?? Atoe wapi hizo billions?

Kazi kwelli kweli!!
 
Toka na pumba zako za kijinga,hujui shida ya maji wanayopata watu ndio maana unalopoka hovyo,unajifanya unatetea ujinga wakati ndugu zako wanapata tabu.

Cha kushangaza, Ng'ombe mnawahamishia yalipo maji, nyie wenyewe mnabaki kukaa pasipo maji mnangoja mletewe maji. Hii sijui akili ya wapi? hamia kwenye maji.
 
Tabata yenyewe maji hakuna..njoo k'yama..watu wanachota maji asubuhi..wanajaza kwenye vyombo..mpaka asubuhi nyingine tena..hapo ni dar...huko vijijini si ndio balaa..Maji ni tatizo kubwa sana..kuliko hata tujuavyo..
 
Hoja ya Mh. nasari ni ya msingi sana... lakini Mh hakwenda mbali kwenye kufikiri. Jiji la Dsm ndiyo linaongoza kwa uchangiaji wa pato la serikali (zaidi ya 75% nadhani). Mapato makubwa yanapotelea kwenye msongamano barabarani hivyo barabara za juu zitaweza kuokoa kiasi kikubwa ambacho kama kiweza kutumika kwa uadilifu kinaweza kuendeleza miradi ya maendeleo ya maji. Kwa upande wangu naona hii ni kama vile kununua fenicha katika ofisi ya Mbunge wakati bado kuna wanafunzi wanakaa chini......Nina maana ni busara mbunge akawa na ofisi kabla ya kuanza kujenga darasa jipya la shule........ hivyo mimi sidhani kama hoja yake ni ya msingi sana
 
Haya masuala ya maji yalitakiwa yawe yametatuliwa miaka 20 iliyopita. Lakini kutokana na failed Policy of CCM eti leo baada ya miaka 50 bado tunaongelea upatikanaji wa maji ya UHAKIKA na SALAMA katika Capital City ya nchi? Imagine Je huko vijijini WATASEMA nini? This is a shame to CCM Govnt.
 
tanira1 Sio barabara za kifahari, dhumuni ni kupunguza msongamano ili tuwahi kazini tuweze kushughulikia maji, imagine mtu una drive 21 km for three hours (tegeta to masaki) kila siku X2 means 6 hours back and forth... think.

hakuna suala la kujadili hapa,

Kwanini ofisi zote kubwa za serikali zipo Dar tena katikati ya jiji?
 
Last edited by a moderator:
Flyover ziwepo na tuone madawati shuleni na madawa mahospitalini.

Sio kujaribujaribu mambo tu kama walivyofanya kwa issue ya Machinga complex!!

Uzuzu wetu ndo mtaji wao!!

Asee nikiangalia machinga complex nashindwa kuelewa serikali yetu inaongozwa na watu wenye akili za namna gani..yani ivi ile complex ilidizainiwa na professional kweli?au ni meya alikaa akajichorea mchoro wake jioni akiwa amechoka..nafikiria kwenda kuwaomba wanipangishe nifugie kuku kwa sababu vile vyumba vinafaa kwa ajili hiyo tu.
 
Hoja ya Mh. nasari ni ya msingi sana... lakini Mh hakwenda mbali kwenye kufikiri. Jiji la Dsm ndiyo linaongoza kwa uchangiaji wa pato la serikali (zaidi ya 75% nadhani). Mapato makubwa yanapotelea kwenye msongamano barabarani hivyo barabara za juu zitaweza kuokoa kiasi kikubwa ambacho kama kiweza kutumika kwa uadilifu kinaweza kuendeleza miradi ya maendeleo ya maji. Kwa upande wangu naona hii ni kama vile kununua fenicha katika ofisi ya Mbunge wakati bado kuna wanafunzi wanakaa chini......Nina maana ni busara mbunge akawa na ofisi kabla ya kuanza kujenga darasa jipya la shule........ hivyo mimi sidhani kama hoja yake ni ya msingi sana

acha ubwege wewe hakuna chapaa ya kushtusha inayopotelea kwenye foleni ukilinga nisha na minya ya rushwa na ufisani kwenye mali asili za nchi hii, na ufisadi wa viongozi wetu kwenye makampuni binafsi kama ya simu na ya wahindi wengine yaayochafua mazingira kila kukicha
 
acha ubwege wewe hakuna chapaa ya kushtusha inayopotelea kwenye foleni ukilinga nisha na minya ya rushwa na ufisani kwenye mali asili za nchi hii, na ufisadi wa viongozi wetu kwenye makampuni binafsi kama ya simu na ya wahindi wengine yaayochafua mazingira kila kukicha
Sasa sijui nani ni hapo kwenye nyekundu...........anyway mada ilikuwa ni kuhusu maji na barabara za juu .......hayo mengine nadhani yanahitaji uzi mpya........... :iamwithstupid:
 
tanira1 Sio barabara za kifahari, dhumuni ni kupunguza msongamano ili tuwahi kazini tuweze kushughulikia maji, imagine mtu una drive 21 km for three hours (tegeta to masaki) kila siku X2 means 6 hours back and forth... think.

hakuna suala la kujadili hapa,

Kwani mliombwa wote mnganganie ishi Dar, Ili tuweze kukubali hili inabidi viongozi wote wa serikali wahamie dodoma, wao na familia zao, muone kama kutakuwa na jam, hakuna haja ya kupoteza pesa kwa upuuzi mwingine kama huo, tushapoteza za kutosha kujenga mji wa dodoma lakini viongozi wanagoma kuhamia huko.

Raisi anatakiwa ahamishe ikulu Dom kisha pale magogoni pafanywe hotel (napendekeza casino). mawaziri na wizara zote ziamie dodoma, makao makuu ya idara zote za serikali zihamishwe dodoma, ofisi za balozi zote zihamie dodoma, baada ya hili maji yatatosha na tagetabto masaki 45mnts.
 
Kwenye vipaumbele vya mwaka huu cha kwanza ni Miundombinu, ambapo miundombinu ya maji na yenyewe ipo kwenye kundi hilo, ukiacha barabara nk....
 
Back
Top Bottom