nasikitika kuwa sijasikia sera na mipango ya vyama arumeru mashariki

FredKavishe

JF-Expert Member
Dec 4, 2010
1,090
318
Nasikitika kusema toka mwanzo wa kampeni sijasikia sera ya chama tuchochote muhimu kwa wananchi wa arumeru ni majibizano mimi wa ukoo wa nyerere,huyu si wa ukoo wa nyerere,dr slaa fisadi alikula hela za ujio wa papa,walete ushahidi well personal attack zimekuwa nyingi arumeru kuliko wagombea kujikita kwenye sera na maendeleo

Ngoja niwaambie CDM,
CCM inachofanya ni kutake attention na kuplay with you minds hili lilikuwa toka igunga na sasa arumeru na msipoangalia mtapoteza hili jimbo wacha niwe muwazi hapa CCM inarusha kashfa za uongo kwa CDM inajua kabisa CDM hawatajadili sera zao watajikita kujibu hoja maji taka kwenye ulingo wa siasa
Sijafika arumeru but nimekuwa naangalia tv taarifa za habari japo nyingi ni za kinafiki lakini ukweli utabaki pale pale tuwaeleze wana arumeru tutarudishaje ardhi ya tutawaleteaje maji tutawapaje ajira na sio kila siku kwenye kampeni kujibu tuhuma.
Sikati viongozi wa CDM kujibu tuhuma but now inazidi hadi inapoteza radha ya uchaguzi sasa.

CCM ni wazuri sana kwenye rafu na hili naona wanafanikiwa tena na hoja zao za ajabu kwasababu wanatake attention yote ya CDM na kubaki kuiongelea CCM hii ni mbaya sana tujikite kwenye sera kama chama.
Sasa kijana Nasari kashatekwa na wazo la kwanini hajaoa na kila siku analiongelea hilo toka liibulie ngoja nikuambie kijana ongelea sera zako tunakoendea wiki ya mwisho

Kingine siamini hizi kamati za maandalizi kama mnakuja na plan nzuri kwa wagombea naweza kusema mnatuangusha sana hili jimbo tulijua siku nyingi litakuwa wazi jee mliaandaa sera za kumu help Nasari mlifanya uchunguzi gani hadi vijijini kujua kuna matatizo gani na mtawasaidiaje wana arumeru jamani
1.Kamati ya maandalizi inatakiwa iwe na kero zote na jinsi ya kuzitatua
2.Kamati ya maandalizi ilitakiwa kujua je kuna miradi gani arumeru ipo kwenye utekelezaji iwe hoja yenu
Leo nimemuona mbunge wa ccm akiongelea mradi wa umeme je mlijua kuna mradi wa umeme kutoka world bank
3.Kamati ya maandalizi ingepaswa kumuandaa Nasari kujikita kwenye sera na kuachana na siasa majitaka je mmeliweza hilo
4.Kamati ya maandalizi ingepanga jinsi ya kuweza kusolve matatizo madogo sio kila tatzo mpaka serikali ije kusolve kama kuchimba visima hata mbunge na wananchi wanaweza je mlianda vitu kama hvyo

Well kwa leo nishie hapo kwenye uchaguzi wa arumeru mengine matokeo yakitoka

Hii kwa wabunge wa CDM hata wachapakazi pia wa vyama vingine
Nashangazwa sana na hizi tabia za wabunge na madiwani kusubiri hadi serikali itoe pesa kutekeleza mambo madogo madogo kwenye jimbo
Hili haliwezekani kuna mambo ya kununua madawati,kukarabati barabara hivi tunaweza hata kufanaya raia na wabunge zetu na madiwani wetu wakijitolea siamini kama jimbo kama ubungo tukiweka system nzuri ya kuchangia hata 1000 kwa mwaka kwenye mfuko wa jimbo la ubungo tunaweza kukosa
Ishu kama kweli mbunge o diwani ulichaguliwa na raia unaweza ukaanzisha mfuko wa jimbo achana na ela zinazotoka bungeni kila mwananchi mwenye kipato akiweka kiasi chake ni uhakika tungejenge shule,hospital ndogo,tungenunua madawati
Kwa hesabu ndogo jimbo lina wakazi 500000 tuseme laki 100000 ndo wenye kazi na kuingiza vipato hapa ukipitisha bakuli mbunge huwezi kukosa milioni 50 za haraka haraka.
Na pia wananchi tuwe tayari kuchangia maendeleo yetu sio kila kitu kitaletwa na serikali hii fisadi tutengeneze mifumo yetu ya kusolve mambo bila kuhusisha serikali

Mwisho kabisa sijasema wagombea hawajasema sera zao sema hawajajikita kusimamia sera zao personal attacks zimekua nyingi.
 
Back
Top Bottom