Sajunne
Senior Member
- Jul 19, 2011
- 104
- 58
Wadau mimi ninajambo ambalo mwenzenu nashindwa kulifafanua na kulipatia ufumbuzi suala lifuatalo, Nina girl friend wangu anapenda sana kuchukua kitu chochote kizuri atakacho niona nacho, mfano juzi kati kuna cm mpya nilinunua alichokifanya aliomba atumie kwa muda, licha ya kuwa ana cm yake. Tulikubaliana baada ya wiki mmoja airudishe, lakini cha kushangaza kila ninapomuomba hiyo cm hataki kunipa na muda huo huo anaibua ugomvi. Bt nashindwa kumuelewa kabisa kwani kitu chochote anachochukua huwa harudishi nikimwambia anaibua ugomvi. Namthamini sana, na ninajitahidi kumpa kilicho ndani ya uwezo wangu lakini kwa anayonifanyia nashindwa kuelewa lengo lake kwangu. Wakati mwingine ninafikiri kama haniheshimu na mengine mengi. Je hebu toeni mchango wenu wadau kuhusu hili.