only83
JF-Expert Member
- Oct 15, 2010
- 5,343
- 2,525
........Awali ya yote napenda kutoa pole kwa wanafunzi 27 wa chuo cha elimu ya kompyuta katika chuo kikuu cha Dodoma kwa kusimamishwa masomo ambako kwa hali inavyoelekea ni kufukuzwa kabisa..kwanini nasema pole,nasema pole kwasababu haya yote ni mbinu chafu za CCM kupunguza wasomi waliofunguka bongo..wanatamani wabakie na vijana katika vyuo wasio na uwezo wa kufikiri na kuchambua mambo kwa upana wake...Baada ya kupata fununu juu ya ubadhirifu wa pesa za mahitaji maalumu kwa wanafunzi hao,uongozi wa wanafunzi uliazimia kufanya mgomo ili kushinikiza uongozi wa chuo kutoa pesa zao..cha kushangaza waliambia kuwa ni mgomo unaosukumwa na CDM..walikwenda mbali zaidi kwa kusema kuwa wakati Mbunge Godbless Lema akiwa hapa Dodoma kwenye kikao cha bunge alikutana na wanafunzi hao na kuwapa sumu kuwa wagome,na wakaendelea kusema wanazo taarifa za kiitelejensia kuwa ni nguvu ya CDM ndani ya vyuo...kwa hakika mimi napinga ufukuzaji wa wanafunzi katika vyuo sababu ya migomo..wanafunzi wa vyuo ni watu wanaopaswa kupewa uhuru kwa kufikiri kwa makini."CRITICAL THINKING" ili waweze kuja kuwa viongozi bora katika taifa hili..kwa kusema haya simaanishi naunga mkono migomo la hasha! na maana kuwa serikali wanapaswa kujua kuwa kizazi hiki ni tofauti na kizazi cha miaka ya 1947...ni watu wenye uwezo wa kusoma mambo na kufuatilia kujua haki zao za msingi...kwahiyo kazi ya serikali si kufukuza wanafunzi bali ni kubadilika kulingana na mazingira ya kizazi hiki..siku za karibuni nilimshangaa waziri wa Elimu ya juu alipotoa onyo kuwa wahadhiri wasifundishe siasa madarasani..Je wanafunzi wanaosoma POLITICAL SCIENCE wahadhiri wafundishe nini? Huu ni ubwege wa viongozi wetu ambao unadhibitishwa kupitia kauli zao...Mwisho naomba CCM muache tabia hii kwa usalama wenu..
NB:MODs naomba msiipeleke thread hii kwenye jukwaa la Elimu..hapa ndio mahala pake kutokana na siasa chafu za CCM vyuoni kwasasa...Nawakilisha!!!!
NB:MODs naomba msiipeleke thread hii kwenye jukwaa la Elimu..hapa ndio mahala pake kutokana na siasa chafu za CCM vyuoni kwasasa...Nawakilisha!!!!