Jpinduzi
Senior Member
- Feb 26, 2011
- 136
- 68
Kila kitu kina stara yake, hata ndizi. Ndio maana wauza ndizi huwa hawazimenyi kwanza ndio wakaziuza kwa sababu wanajua hakuna atakayezinunua, bali zitangongwa na mainzi. Hivyo hivyo, wale wanawake waliojitoa stara ndio kama ndizi zinazotembezwa zikiwa zimemenywa. Sasa wale wanaowashangilia wakipita uchi si watu bali ni mainzi yanawangonga. Msijidhalilishe kwa kujiweka wazi.
Moja kati ya tofauti ya wanyama nawatu ni kuvaa nguo (kujistiri). Kila unavyozidisha stara, ndivyo unazidisha tofauti yako na mnyama. Na kila unavyopunguza stara ya mwili wako ndio unaukaribia unyama zaidi, yaani unapunguza ule utofauti wako na mnyama.
Hebu tizama wadada wanaovaa vizuri wanavyopendeza!