Nasa yatuma bomu kuulipua mwezi

ituganhila

Member
Aug 25, 2009
24
0
Wana JF salaam.Naomba mnisaidie kwa hili ni zito.Shirika la NASA limetuma bomu kwenda kuulipua mwezi.Lengo lao ni kupata barafu iliyopo katika mwezi. Je hatua hiyo si hatari kwa wanadamu? Gharama za bomu hilo ni $79 Milioni za kimarekani. Je bomu hilo halitaharibu mfumo wa mwenendo wa mwezi katika axis yake? Je hapatakuwa na madhara ya mfumo uliopo kati ya Jua, Mwezi na Dunia? je kitakachotokea huko juu baada ya kulipua hakitawaathiri wanadamu?Je wamekosa katika barafu huku duniani mpaka waktafute mwezini? Dunia ina matatizo makubwa sana kama magonjwa na njaa, vita, matetemeko typhoon yote haya yanahitaji majibu. Pamoja na hayo Marekani kwenye matatizo ya kiuchumi na ukosefu wa ajira kwao pia.Je ni vema kutumia fedha hiyo kwakutafuta maji ya barafu katika mwezi ni matumizi halali? Japokuwa mimi si mmarekani lakini ni mkazi wa duniani. Je athari zitakazo tokea baada ya mlipuko hazitaathiri dunia nzima?Chembe chembe zitakazotoka huko hazitakuwa na madhara kwa viumbe wa duniani. Au dunia( Nchi zote) zimeshirikishwa kwa hili?
Wanajamii nisaidieni.
 
Wana JF salaam.Naomba mnisaidie kwa hili ni zito.Shirika la NASA limetuma bomu kwenda kuulipua mwezi.Lengo lao ni kupata barafu iliyopo katika mwezi. Je hatua hiyo si hatari kwa wanadamu? Gharama za bomu hilo ni $79 Milioni za kimarekani. Je bomu hilo halitaharibu mfumo wa mwenendo wa mwezi katika axis yake? Je hapatakuwa na madhara ya mfumo uliopo kati ya Jua, Mwezi na Dunia? je kitakachotokea huko juu baada ya kulipua hakitawaathiri wanadamu?Je wamekosa katika barafu huku duniani mpaka waktafute mwezini? Dunia ina matatizo makubwa sana kama magonjwa na njaa, vita, matetemeko typhoon yote haya yanahitaji majibu. Pamoja na hayo Marekani kwenye matatizo ya kiuchumi na ukosefu wa ajira kwao pia.Je ni vema kutumia fedha hiyo kwakutafuta maji ya barafu katika mwezi ni matumizi halali? Japokuwa mimi si mmarekani lakini ni mkazi wa duniani. Je athari zitakazo tokea baada ya mlipuko hazitaathiri dunia nzima?Chembe chembe zitakazotoka huko hazitakuwa na madhara kwa viumbe wa duniani. Au dunia( Nchi zote) zimeshirikishwa kwa hili?
Wanajamii nisaidieni.

Hakuna athari zozote kwa dunia zitakazotokea, ni ungaunga tu utaofika huku, na hauna madhara, maana mwezi ni jiwe/mwamba wa kawaida, hauna sumu!Hakuna athari katika mzunguko wa dunia katika axis yake. Hakuna madhara kwa majira ya mwaka.Hakuna madhara yoyoye kwa viumbe hai wala gesi ya duniani huku.Ni kweli kabisa zoezi hilo ni ghali kwa habari ya pesa, lakini tukumbuke kwamba utafiti ni lazima kwaajili ya maendeleo. Huwa inafikia wakati inabidi tusihesabu gharama kama tunataka kutimiza haja fulani.Unaweza kukuta hatimaye kwambamatokeo ya utafiti huo ni mazuri kuliko uwoga wa gharama wanazotumia, na huenda dunia nzima ikafaidika na watoto wetu wakapata elimu mpya kabisa kuhusu anga hizo za juu!Lets be patient pals!
 
Back
Top Bottom