ituganhila
Member
- Aug 25, 2009
- 24
- 0
Wana JF salaam.Naomba mnisaidie kwa hili ni zito.Shirika la NASA limetuma bomu kwenda kuulipua mwezi.Lengo lao ni kupata barafu iliyopo katika mwezi. Je hatua hiyo si hatari kwa wanadamu? Gharama za bomu hilo ni $79 Milioni za kimarekani. Je bomu hilo halitaharibu mfumo wa mwenendo wa mwezi katika axis yake? Je hapatakuwa na madhara ya mfumo uliopo kati ya Jua, Mwezi na Dunia? je kitakachotokea huko juu baada ya kulipua hakitawaathiri wanadamu?Je wamekosa katika barafu huku duniani mpaka waktafute mwezini? Dunia ina matatizo makubwa sana kama magonjwa na njaa, vita, matetemeko typhoon yote haya yanahitaji majibu. Pamoja na hayo Marekani kwenye matatizo ya kiuchumi na ukosefu wa ajira kwao pia.Je ni vema kutumia fedha hiyo kwakutafuta maji ya barafu katika mwezi ni matumizi halali? Japokuwa mimi si mmarekani lakini ni mkazi wa duniani. Je athari zitakazo tokea baada ya mlipuko hazitaathiri dunia nzima?Chembe chembe zitakazotoka huko hazitakuwa na madhara kwa viumbe wa duniani. Au dunia( Nchi zote) zimeshirikishwa kwa hili?
Wanajamii nisaidieni.
Wanajamii nisaidieni.