Naloli
JF-Expert Member
- Aug 26, 2010
- 416
- 81
Baada ya hukumu ya kupinga matokeo ya Ubunge Arusha Mjini kutoka na Mh. Godbless Lema kuvuliwa Ubunge, nimesikia kauli ya Mh. Godbless Lema na Viongozi wa CDM kuwa wako tayari kutokata Rufaa ili uchaguzi ufanyike mapema na warejeshe jimbo lao. Kiukweli mimi sihafikiani na Uamuzi huo. Sababu zangu ni kama zifuatazo:-
MOJA; Kwa mujibu wa hukumu Lema amepatwa na hatia kwa kukiuka kifungu cha108 kifungu kidogo cha pili A (kimsingi anaye kutwa na hatia kwa kiuka kifungu hiki anaruhusiwa kugombea tena UBUNGE) yaani kukutwa na kosa chini ya kifungu hicho uzuhiwi kugombea tena Ubunge. Lakini ajabu ya mwaka Jaji katika majumuisho ya hukumu jaji ametumia kifungu cha 114 cha sheria ya Uchaguzi kumzuia Mh. Lema kugombea tena UBUNGE baada ya kupatikana na hatia. Kwa kifupi kifungu hiki cha 114 utumika kumzuia kugombea Ubunge Mbunge aliyetenguliwa Ubunge wake kwa kukutwa na hatia ya kujihusisha na makosa ya RUSHWA. Kwangu mimi mkanganyiko huu si wa Bahati mbaya bali ulikusudiwa.( kwanini naamini hivyo) Wiki hii nilituma POST hapa JF na kueleza kuwa nimepata taarifa ya Mh. Lema kuvuliwa Ubunge wake na kuwa atazuiwa kugombea Ubunge tena, niliweka wazi kuwa taarifa hizo zimezagaa Arusha na CCM wamepanga hadi sherehe ya kujipongeza, na Mpango huo wa kumvua UBUNGE Lema uliasisiwa na kiusimamiwa na timu nzima ya EL. Na kweli nilichokieleza kimetimia. SWALI. Je kumzuia Lema kugombea tena Ubunge kwa kosa ambalo hajakutwa nalo yaani kosa la RUSHWA ni sahihi? au ndio Jaji alikuwa anatekeleza Maagizo ya MABWANA ZAKE? kwa kuamua KUIBAKA HAKI.
PILI napinga CDM kukokata Rufaa kwa sababu HUKUMU hii (yaani kipengele cha kumzuia LEMA kugombea Ubunge) kinakiathiri chama kwa upande mmoja lakini ni athari ndogo kwa CDM maana wanaruhusa ya kumsimamisha mtu mwingine isipokuwa Lema tu. Lakini hukumu hiyo ina athari zaidi kwa LEMA maana kwa kusimamishwa miaka mitano kutogombea UBUNGE kuna maanisha hata mwaka 2015 haruhusiwi kugombea. Sasa kwanini CDM na LEMA wakubari LEMA abebe msalaba wa dhulma peke yake? Kwanini CDM wakae kimya wakati wanajua wazi hukumu hiyo si ya haki kwa LEMA? Kwanini CDM imtelekeze LEMA kwa ajili ya kulipata JIMBO la ARRUSHA MJINI?
TATU; CDM iliwavua Uanachama na Udiwani Madiwani wake watano wa kata tofauti Arusha mjini kwa sababu ya kuingia makubaliano na CCM kuhusu UMEYA wa Manispaa ya Arusha bila Ridhaa ya CHAMA. N ukiangalia Idadi ya madiwani wa cdm na ccm ukiweka na wa Tlp ni wazi CDM hata kama UCHAGUZI wa MEYA ungefanyika na wao kuweka mgombea walikuwa na nafasi finyu ya kushinda LAKINIA msimamo wa CDM ulikuwa ni lazima UCHAGUZI urudiwe ili sheria na Haki ziheshimiwe bila kujali wao watashinda au kushindwa cha msingi HAKI ITENDEKE. Kama HAKI nia msimamo na msingi wa CDM hadi kuwatosa Madiwani watano ambao walishindwa kusimamia hilo, Je kwanini wamtose LEMA eti kwakuwa wana uhakika wa kupata Jimbo la Arusha Mjini?
NNE: kuna wapiganaji watatu waliuwawa na polisi kwa kushiriki maandamano ya kupinga CCM kubaka Demokrasia na kujipitishia MEYA kibabe, Marehemu hawa waliandamana na kupoteza maisha yao sababu ya kusimamia HAKI na walikufa wakiamini CDM wanasimamia HAKI kwa gharama yoyote. Sasa leo inakuwaje CDM wanashindwa kuwaENZI marehemu hao kwa kuendelea kusimamia HAKI kwa gharama yeyote hata kwa kupoteza jimno la LEMA ili HAKI dhidi ya LEMA yaani HAKIA ya kugombea arejeshewe?
TANO; (Hapa wanasheria watanisaidia) kisheria kuana kitu kinaitwa (RUFAA) APPEAL na JUDICIAL REVIEW, Kwanini CDM wasitumie hiki kipengele cha pili yaani JUDICIAL REVIEW kuiomba mahakama KUU au ya RUFAA kuifanyia REVIEW mwenendo mzima wa kesi ili kuona kama Hukumu ya kumzuia LEMA kugombea ndani ya miaka mitano hipo sahihi au la< kama haipo sahihi imtake Jaji kurekebisha kipengele hicho katika HUKUMU yake?
MWISHO; Hoja kuwa wananchi wa ARUSHA watakosa muwakilishi BUNGENI kwangu siioni kuwa ya msingi maana ni CDM haohao ambao wanawakosesha haki ya uwakilishi ktk baraza la madiwani wananchi wa ARUSHA wa KATA TANO baada ya kuwavua uanachama kwakuwa madiwani hao hawakuheshimu msimamo wa chama kuhusiana na HAKI. Je ni sahihi wananchi wa ARUSHA wawe na MBUNGE wa kuwawakilisha BUNGENI wakati MBUNGE wao LEMA hakutendewa HAKI kwa kuzuia kugombea? kwanini haki wapewe wanajimbo la ARUSHA Lema anyimwe? Hivi ni sahihi kumnyima mtu haki kwa kigezo kuwa wengi watakosa uwakilishi Bungeni? Mbino kwa miaka 50 wamepata UWAKILISHI lakini hadi leo wanalalamika kuwa Wawakilishi hao hawakuwasaidia na kuwafanyia kazi waliyowatuma? Hivi si kuna majimbo yana WABUNGE lakini uwajibikaji huo wa wabunge hao kwa wananchi ni sawa na JIMBO kuto kuwa na MBUNGE?
MOJA; Kwa mujibu wa hukumu Lema amepatwa na hatia kwa kukiuka kifungu cha108 kifungu kidogo cha pili A (kimsingi anaye kutwa na hatia kwa kiuka kifungu hiki anaruhusiwa kugombea tena UBUNGE) yaani kukutwa na kosa chini ya kifungu hicho uzuhiwi kugombea tena Ubunge. Lakini ajabu ya mwaka Jaji katika majumuisho ya hukumu jaji ametumia kifungu cha 114 cha sheria ya Uchaguzi kumzuia Mh. Lema kugombea tena UBUNGE baada ya kupatikana na hatia. Kwa kifupi kifungu hiki cha 114 utumika kumzuia kugombea Ubunge Mbunge aliyetenguliwa Ubunge wake kwa kukutwa na hatia ya kujihusisha na makosa ya RUSHWA. Kwangu mimi mkanganyiko huu si wa Bahati mbaya bali ulikusudiwa.( kwanini naamini hivyo) Wiki hii nilituma POST hapa JF na kueleza kuwa nimepata taarifa ya Mh. Lema kuvuliwa Ubunge wake na kuwa atazuiwa kugombea Ubunge tena, niliweka wazi kuwa taarifa hizo zimezagaa Arusha na CCM wamepanga hadi sherehe ya kujipongeza, na Mpango huo wa kumvua UBUNGE Lema uliasisiwa na kiusimamiwa na timu nzima ya EL. Na kweli nilichokieleza kimetimia. SWALI. Je kumzuia Lema kugombea tena Ubunge kwa kosa ambalo hajakutwa nalo yaani kosa la RUSHWA ni sahihi? au ndio Jaji alikuwa anatekeleza Maagizo ya MABWANA ZAKE? kwa kuamua KUIBAKA HAKI.
PILI napinga CDM kukokata Rufaa kwa sababu HUKUMU hii (yaani kipengele cha kumzuia LEMA kugombea Ubunge) kinakiathiri chama kwa upande mmoja lakini ni athari ndogo kwa CDM maana wanaruhusa ya kumsimamisha mtu mwingine isipokuwa Lema tu. Lakini hukumu hiyo ina athari zaidi kwa LEMA maana kwa kusimamishwa miaka mitano kutogombea UBUNGE kuna maanisha hata mwaka 2015 haruhusiwi kugombea. Sasa kwanini CDM na LEMA wakubari LEMA abebe msalaba wa dhulma peke yake? Kwanini CDM wakae kimya wakati wanajua wazi hukumu hiyo si ya haki kwa LEMA? Kwanini CDM imtelekeze LEMA kwa ajili ya kulipata JIMBO la ARRUSHA MJINI?
TATU; CDM iliwavua Uanachama na Udiwani Madiwani wake watano wa kata tofauti Arusha mjini kwa sababu ya kuingia makubaliano na CCM kuhusu UMEYA wa Manispaa ya Arusha bila Ridhaa ya CHAMA. N ukiangalia Idadi ya madiwani wa cdm na ccm ukiweka na wa Tlp ni wazi CDM hata kama UCHAGUZI wa MEYA ungefanyika na wao kuweka mgombea walikuwa na nafasi finyu ya kushinda LAKINIA msimamo wa CDM ulikuwa ni lazima UCHAGUZI urudiwe ili sheria na Haki ziheshimiwe bila kujali wao watashinda au kushindwa cha msingi HAKI ITENDEKE. Kama HAKI nia msimamo na msingi wa CDM hadi kuwatosa Madiwani watano ambao walishindwa kusimamia hilo, Je kwanini wamtose LEMA eti kwakuwa wana uhakika wa kupata Jimbo la Arusha Mjini?
NNE: kuna wapiganaji watatu waliuwawa na polisi kwa kushiriki maandamano ya kupinga CCM kubaka Demokrasia na kujipitishia MEYA kibabe, Marehemu hawa waliandamana na kupoteza maisha yao sababu ya kusimamia HAKI na walikufa wakiamini CDM wanasimamia HAKI kwa gharama yoyote. Sasa leo inakuwaje CDM wanashindwa kuwaENZI marehemu hao kwa kuendelea kusimamia HAKI kwa gharama yeyote hata kwa kupoteza jimno la LEMA ili HAKI dhidi ya LEMA yaani HAKIA ya kugombea arejeshewe?
TANO; (Hapa wanasheria watanisaidia) kisheria kuana kitu kinaitwa (RUFAA) APPEAL na JUDICIAL REVIEW, Kwanini CDM wasitumie hiki kipengele cha pili yaani JUDICIAL REVIEW kuiomba mahakama KUU au ya RUFAA kuifanyia REVIEW mwenendo mzima wa kesi ili kuona kama Hukumu ya kumzuia LEMA kugombea ndani ya miaka mitano hipo sahihi au la< kama haipo sahihi imtake Jaji kurekebisha kipengele hicho katika HUKUMU yake?
MWISHO; Hoja kuwa wananchi wa ARUSHA watakosa muwakilishi BUNGENI kwangu siioni kuwa ya msingi maana ni CDM haohao ambao wanawakosesha haki ya uwakilishi ktk baraza la madiwani wananchi wa ARUSHA wa KATA TANO baada ya kuwavua uanachama kwakuwa madiwani hao hawakuheshimu msimamo wa chama kuhusiana na HAKI. Je ni sahihi wananchi wa ARUSHA wawe na MBUNGE wa kuwawakilisha BUNGENI wakati MBUNGE wao LEMA hakutendewa HAKI kwa kuzuia kugombea? kwanini haki wapewe wanajimbo la ARUSHA Lema anyimwe? Hivi ni sahihi kumnyima mtu haki kwa kigezo kuwa wengi watakosa uwakilishi Bungeni? Mbino kwa miaka 50 wamepata UWAKILISHI lakini hadi leo wanalalamika kuwa Wawakilishi hao hawakuwasaidia na kuwafanyia kazi waliyowatuma? Hivi si kuna majimbo yana WABUNGE lakini uwajibikaji huo wa wabunge hao kwa wananchi ni sawa na JIMBO kuto kuwa na MBUNGE?