Napinga kwa nguvu zote CHADEMA kutokata rufaa

Naloli

JF-Expert Member
Aug 26, 2010
416
81
Baada ya hukumu ya kupinga matokeo ya Ubunge Arusha Mjini kutoka na Mh. Godbless Lema kuvuliwa Ubunge, nimesikia kauli ya Mh. Godbless Lema na Viongozi wa CDM kuwa wako tayari kutokata Rufaa ili uchaguzi ufanyike mapema na warejeshe jimbo lao. Kiukweli mimi sihafikiani na Uamuzi huo. Sababu zangu ni kama zifuatazo:-

MOJA; Kwa mujibu wa hukumu Lema amepatwa na hatia kwa kukiuka kifungu cha108 kifungu kidogo cha pili A (kimsingi anaye kutwa na hatia kwa kiuka kifungu hiki anaruhusiwa kugombea tena UBUNGE) yaani kukutwa na kosa chini ya kifungu hicho uzuhiwi kugombea tena Ubunge. Lakini ajabu ya mwaka Jaji katika majumuisho ya hukumu jaji ametumia kifungu cha 114 cha sheria ya Uchaguzi kumzuia Mh. Lema kugombea tena UBUNGE baada ya kupatikana na hatia. Kwa kifupi kifungu hiki cha 114 utumika kumzuia kugombea Ubunge Mbunge aliyetenguliwa Ubunge wake kwa kukutwa na hatia ya kujihusisha na makosa ya RUSHWA. Kwangu mimi mkanganyiko huu si wa Bahati mbaya bali ulikusudiwa.( kwanini naamini hivyo) Wiki hii nilituma POST hapa JF na kueleza kuwa nimepata taarifa ya Mh. Lema kuvuliwa Ubunge wake na kuwa atazuiwa kugombea Ubunge tena, niliweka wazi kuwa taarifa hizo zimezagaa Arusha na CCM wamepanga hadi sherehe ya kujipongeza, na Mpango huo wa kumvua UBUNGE Lema uliasisiwa na kiusimamiwa na timu nzima ya EL. Na kweli nilichokieleza kimetimia. SWALI. Je kumzuia Lema kugombea tena Ubunge kwa kosa ambalo hajakutwa nalo yaani kosa la RUSHWA ni sahihi? au ndio Jaji alikuwa anatekeleza Maagizo ya MABWANA ZAKE? kwa kuamua KUIBAKA HAKI.
PILI napinga CDM kukokata Rufaa kwa sababu HUKUMU hii (yaani kipengele cha kumzuia LEMA kugombea Ubunge) kinakiathiri chama kwa upande mmoja lakini ni athari ndogo kwa CDM maana wanaruhusa ya kumsimamisha mtu mwingine isipokuwa Lema tu. Lakini hukumu hiyo ina athari zaidi kwa LEMA maana kwa kusimamishwa miaka mitano kutogombea UBUNGE kuna maanisha hata mwaka 2015 haruhusiwi kugombea. Sasa kwanini CDM na LEMA wakubari LEMA abebe msalaba wa dhulma peke yake? Kwanini CDM wakae kimya wakati wanajua wazi hukumu hiyo si ya haki kwa LEMA? Kwanini CDM imtelekeze LEMA kwa ajili ya kulipata JIMBO la ARRUSHA MJINI?

TATU; CDM
iliwavua Uanachama na Udiwani Madiwani wake watano wa kata tofauti Arusha mjini kwa sababu ya kuingia makubaliano na CCM kuhusu UMEYA wa Manispaa ya Arusha bila Ridhaa ya CHAMA. N ukiangalia Idadi ya madiwani wa cdm na ccm ukiweka na wa Tlp ni wazi CDM hata kama UCHAGUZI wa MEYA ungefanyika na wao kuweka mgombea walikuwa na nafasi finyu ya kushinda LAKINIA msimamo wa CDM ulikuwa ni lazima UCHAGUZI urudiwe ili sheria na Haki ziheshimiwe bila kujali wao watashinda au kushindwa cha msingi HAKI ITENDEKE. Kama HAKI nia msimamo na msingi wa CDM hadi kuwatosa Madiwani watano ambao walishindwa kusimamia hilo, Je kwanini wamtose LEMA eti kwakuwa wana uhakika wa kupata Jimbo la Arusha Mjini?

NNE: kuna wapiganaji watatu waliuwawa na polisi kwa kushiriki maandamano ya kupinga CCM kubaka Demokrasia na kujipitishia MEYA kibabe, Marehemu hawa waliandamana na kupoteza maisha yao sababu ya kusimamia HAKI na walikufa wakiamini CDM wanasimamia HAKI kwa gharama yoyote. Sasa leo inakuwaje CDM wanashindwa kuwaENZI marehemu hao kwa kuendelea kusimamia HAKI kwa gharama yeyote hata kwa kupoteza jimno la LEMA ili HAKI dhidi ya LEMA yaani HAKIA ya kugombea arejeshewe?

TANO; (Hapa wanasheria watanisaidia) kisheria kuana kitu kinaitwa (RUFAA) APPEAL na JUDICIAL REVIEW, Kwanini CDM wasitumie hiki kipengele cha pili yaani JUDICIAL REVIEW kuiomba mahakama KUU au ya RUFAA kuifanyia REVIEW mwenendo mzima wa kesi ili kuona kama Hukumu ya kumzuia LEMA kugombea ndani ya miaka mitano hipo sahihi au la< kama haipo sahihi imtake Jaji kurekebisha kipengele hicho katika HUKUMU yake?

MWISHO; Hoja kuwa wananchi wa ARUSHA watakosa muwakilishi BUNGENI kwangu siioni kuwa ya msingi maana ni CDM haohao ambao wanawakosesha haki ya uwakilishi ktk baraza la madiwani wananchi wa ARUSHA wa KATA TANO baada ya kuwavua uanachama kwakuwa madiwani hao hawakuheshimu msimamo wa chama kuhusiana na HAKI. Je ni sahihi wananchi wa ARUSHA wawe na MBUNGE wa kuwawakilisha BUNGENI wakati MBUNGE wao LEMA hakutendewa HAKI kwa kuzuia kugombea? kwanini haki wapewe wanajimbo la ARUSHA Lema anyimwe? Hivi ni sahihi kumnyima mtu haki kwa kigezo kuwa wengi watakosa uwakilishi Bungeni? Mbino kwa miaka 50 wamepata UWAKILISHI lakini hadi leo wanalalamika kuwa Wawakilishi hao hawakuwasaidia na kuwafanyia kazi waliyowatuma? Hivi si kuna majimbo yana WABUNGE lakini uwajibikaji huo wa wabunge hao kwa wananchi ni sawa na JIMBO kuto kuwa na MBUNGE?
 
Umejitahidi sana kuandika na kuweka wazi nawazo yako.Lakini kumbuka kuwa kesi hii mi ya kisiasa. Kesi za kisiasa mara nyingi za haki, kwa maana kuwa haki huwa haifuatwi bali hufuatwa matakwa ya aliye juu.
Kwa hili la Arusha mjini ni kuwa kama Chadema wakikata rufaa basi huenda ikawa hakuna uchaguzi hadi ule wa 2015.Kazi hapa ya mahakama itakuwa ni kuahirisha kesi hadi uchaguzi mkuu ujao.
Kwa hiyo ni heri kupambana tena ksms kuna uhakika wa kushinda tena.
 
Umejitahidi sana kuandika na kuweka wazi nawazo yako.Lakini kumbuka kuwa kesi hii mi ya kisiasa. Kesi za kisiasa mara nyingi za haki, kwa maana kuwa haki huwa haifuatwi bali hufuatwa matakwa ya aliye juu.
Kwa hili la Arusha mjini ni kuwa kama Chadema wakikata rufaa basi huenda ikawa hakuna uchaguzi hadi ule wa 2015.Kazi hapa ya mahakama itakuwa ni kuahirisha kesi hadi uchaguzi mkuu ujao.
Kwa hiyo ni heri kupambana tena ksms kuna uhakika wa kushinda tena.


Hebu nisaidie kitu kimoja mkuu ambacho labda mimi sijakipata vizuri, kwa mujibu wa hukumu ya jana, LEMA anaruhusiwa kugombea tena au la??
 
Hebu nisaidie kitu kimoja mkuu ambacho labda mimi sijakipata vizuri, kwa mujibu wa hukumu ya jana, LEMA anaruhusiwa kugombea tena au la??

KWA kwa mujibu wa HUKUMU LEMA haruhusiwi kugombea. Embu soma vizuri kipengele cha kwanza cha post yangu nilicho kiandika MOJA
 
Kwa kifungu alichokieleza mleta mada ni kweli hawezi gombea.

Judge amepitiwa maana hakuna ushahidi kuhusu rushwa ambao ulielekezwa katika mwenendndo mzima.

Hivyo the only way nikupeleka maombi Mahakama Kuu ili iweze yenyewe ku rectify error on judgment au vinginevyo kuomba marejeo "Revision" Mahakama ya Rufaa, lakini kama kuna kamchizo kanachezwa utasikia Mahakama haina fungu mara hooo sijui ..... kibao mara 2015.
 
Umejitahidi sana kuandika na kuweka wazi nawazo yako.Lakini kumbuka kuwa kesi hii mi ya kisiasa. Kesi za kisiasa mara nyingi za haki, kwa maana kuwa haki huwa haifuatwi bali hufuatwa matakwa ya aliye juu.
Kwa hili la Arusha mjini ni kuwa kama Chadema wakikata rufaa basi huenda ikawa hakuna uchaguzi hadi ule wa 2015.Kazi hapa ya mahakama itakuwa ni kuahirisha kesi hadi uchaguzi mkuu ujao.
Kwa hiyo ni heri kupambana tena ksms kuna uhakika wa kushinda tena.

Sasa ndugu yangu kwa kuwa ni hukumu ya kisiasa tukubali kumtelekeza LEMA asigombee kwa miaka mitano kwakosa ambalo hajatenda ila CCM na Mafisadi wamemtengenezea kwa kumuamuru Jaji aliweke katika hukumu?
 
Kwa kifungu alichokieleza mleta mada ni kweli hawezi gombea.

Judge amepitiwa maana hakuna ushahidi kuhusu rushwa ambao ulielekezwa katika mwenendndo mzima.

Hivyo the only way nikupeleka maombi Mahakama Kuu ili iweze yenyewe ku rectify error on judgment au vinginevyo kuomba marejeo "Revision" Mahakama ya Rufaa, lakini kama kuna kamchizo kanachezwa utasikia Mahakama haina fungu mara hooo sijui ..... kibao mara 2015.
progress.gif
Edit Post Reply Reply With Quote





[h=2]JamiiForums Message[/h]


Cancel Changes


[h=3]Errors[/h] [h=3]The following errors occurred with your submission[/h]
Okay


[h=3]
reply_40b.png
[/h]
 
Kwa kifungu alichokieleza mleta mada ni kweli hawezi gombea.

Judge amepitiwa maana hakuna ushahidi kuhusu rushwa ambao ulielekezwa katika mwenendndo mzima.

Hivyo the only way nikupeleka maombi Mahakama Kuu ili iweze yenyewe ku rectify error on judgment au vinginevyo kuomba marejeo "Revision" Mahakama ya Rufaa, lakini kama kuna kamchizo kanachezwa utasikia Mahakama haina fungu mara hooo sijui ..... kibao mara 2015.

Hivyo sehemu niliyo iwekea rangi Blue ndio naona ni suluhisho la tatizo hili kuliko lulimbilia katika uchaguzi huku tukimtelekeza Mpiganaji mwenzetu eti tu ARUSHA inaweza kukosa mbunge hadi 2015
 
Kwa kifungu alichokieleza mleta mada ni kweli hawezi gombea.

Judge amepitiwa maana hakuna ushahidi kuhusu rushwa ambao ulielekezwa katika mwenendndo mzima.

Hivyo the only way nikupeleka maombi Mahakama Kuu ili iweze yenyewe ku rectify error on judgment au vinginevyo kuomba marejeo "Revision" Mahakama ya Rufaa, lakini kama kuna kamchizo kanachezwa utasikia Mahakama haina fungu mara hooo sijui ..... kibao mara 2015.

OK, nashukuru kwa hii explanation. Pamoja kamanda.
 
Umetumwa wewe manake plan zenu ilikuwa si kurudia uchaguzi kwa sababu kwanza hela hamna, mtu wa kumsimamisha ili apambane na cdm lazima atakunya makundi matatu c mawili lakini la muhimu na ambalo lipo wazi ni kushindwa vibaya hivyo ninyi kuaibika zaidi!
Sasa usituchorenge! pateni mlichotaka sisi tunawasubiri kwenye kura! siku zote mwisho wa ubaya aibu!!
 
Asante sana Mkuu kwa maelezo safi kabisa! Natumaini baadhi ya viongozi watapitia hii pia itawasaidia kutoa maamuzi sahihi hapo kesho ila naomba Jamani kama amepigwa stop kugombea naomba chadema wakate rufaa jamani kuliko kumpoteza kamanda wetu hivihivi!
 
Mpaka sasa sielewi nani mkweli na nani ananipotosha, wengine ooooooh Lema haruhusiwi kugombea, wengine oooooh Lema anaruhusiwa kugombea, kipi ni kipi hapa?
 
Hukumu imekaa kimtegeo jamani! tusirudi mahakamani! haiwezekani uambiwe njia hii kuna chatu usipite wewe unapita! Jaji mkuu wa majaji JK alishajaji kama alivyomjaji babu sea na papii! so hakuna kurudi mahakamni 5 years Lema anakwenda kukijenga chama na sisi wana waarusha tunafungua mfuko wa kulipa mshahara kama wa mbunge wetu finito
 
Asante sana Mkuu kwa maelezo safi kabisa! Natumaini baadhi ya viongozi watapitia hii pia itawasaidia kutoa maamuzi sahihi hapo kesho ila naomba Jamani kama amepigwa stop kugombea naomba chadema wakate rufaa jamani kuliko kumpoteza kamanda wetu hivihivi!

Yani mzee unategeka haraka! huyu katumwa yupo kazini huyo! we twende kwenye uchaguzi Lema ni mbunge wetu na sisi tutamlipa!
 
Ilisemekana kwamba , Lema anaruhusiwa kugombea tena , Basi haruhusiwi basi Lema atate rufaa, ili jimbo libaki hadi 2015, Lema atakuwa anahirimalisha Chama , nasi wana Arusha tutakuwa tunamtambua lema kama Aliyekuwa mbuge wa Arusha mjini. ili Ccm wapoteze na CC tupoteze
 
Baada ya hukumu ya kupinga matokeo ya Ubunge Arusha Mjini kutoka na Mh. Godbless Lema kuvuliwa Ubunge, nimesikia kauli ya Mh. Godbless Lema na Viongozi wa CDM kuwa wako tayari kutokata Rufaa ili uchaguzi ufanyike mapema na warejeshe jimbo lao. Kiukweli mimi sihafikiani na Uamuzi huo. Sababu zangu ni kama zifuatazo:-

MOJA; Kwa mujibu wa hukumu Lema amepatwa na hatia kwa kukiuka kifungu cha108 kifungu kidogo cha pili A (kimsingi anaye kutwa na hatia kwa kiuka kifungu hiki anaruhusiwa kugombea tena UBUNGE) yaani kukutwa na kosa chini ya kifungu hicho uzuhiwi kugombea tena Ubunge. Lakini ajabu ya mwaka Jaji katika majumuisho ya hukumu jaji ametumia kifungu cha 114 cha sheria ya Uchaguzi kumzuia Mh. Lema kugombea tena UBUNGE baada ya kupatikana na hatia. Kwa kifupi kifungu hiki cha 114 utumika kumzuia kugombea Ubunge Mbunge aliyetenguliwa Ubunge wake kwa kukutwa na hatia ya kujihusisha na makosa ya RUSHWA. Kwangu mimi mkanganyiko huu si wa Bahati mbaya bali ulikusudiwa.( kwanini naamini hivyo) Wiki hii nilituma POST hapa JF na kueleza kuwa nimepata taarifa ya Mh. Lema kuvuliwa Ubunge wake na kuwa atazuiwa kugombea Ubunge tena, niliweka wazi kuwa taarifa hizo zimezagaa Arusha na CCM wamepanga hadi sherehe ya kujipongeza, na Mpango huo wa kumvua UBUNGE Lema uliasisiwa na kiusimamiwa na timu nzima ya EL. Na kweli nilichokieleza kimetimia. SWALI. Je kumzuia Lema kugombea tena Ubunge kwa kosa ambalo hajakutwa nalo yaani kosa la RUSHWA ni sahihi? au ndio Jaji alikuwa anatekeleza Maagizo ya MABWANA ZAKE? kwa kuamua KUIBAKA HAKI.
PILI napinga CDM kukokata Rufaa kwa sababu HUKUMU hii (yaani kipengele cha kumzuia LEMA kugombea Ubunge) kinakiathiri chama kwa upande mmoja lakini ni athari ndogo kwa CDM maana wanaruhusa ya kumsimamisha mtu mwingine isipokuwa Lema tu. Lakini hukumu hiyo ina athari zaidi kwa LEMA maana kwa kusimamishwa miaka mitano kutogombea UBUNGE kuna maanisha hata mwaka 2015 haruhusiwi kugombea. Sasa kwanini CDM na LEMA wakubari LEMA abebe msalaba wa dhulma peke yake? Kwanini CDM wakae kimya wakati wanajua wazi hukumu hiyo si ya haki kwa LEMA? Kwanini CDM imtelekeze LEMA kwa ajili ya kulipata JIMBO la ARRUSHA MJINI?

TATU; CDM
iliwavua Uanachama na Udiwani Madiwani wake watano wa kata tofauti Arusha mjini kwa sababu ya kuingia makubaliano na CCM kuhusu UMEYA wa Manispaa ya Arusha bila Ridhaa ya CHAMA. N ukiangalia Idadi ya madiwani wa cdm na ccm ukiweka na wa Tlp ni wazi CDM hata kama UCHAGUZI wa MEYA ungefanyika na wao kuweka mgombea walikuwa na nafasi finyu ya kushinda LAKINIA msimamo wa CDM ulikuwa ni lazima UCHAGUZI urudiwe ili sheria na Haki ziheshimiwe bila kujali wao watashinda au kushindwa cha msingi HAKI ITENDEKE. Kama HAKI nia msimamo na msingi wa CDM hadi kuwatosa Madiwani watano ambao walishindwa kusimamia hilo, Je kwanini wamtose LEMA eti kwakuwa wana uhakika wa kupata Jimbo la Arusha Mjini?

NNE: kuna wapiganaji watatu waliuwawa na polisi kwa kushiriki maandamano ya kupinga CCM kubaka Demokrasia na kujipitishia MEYA kibabe, Marehemu hawa waliandamana na kupoteza maisha yao sababu ya kusimamia HAKI na walikufa wakiamini CDM wanasimamia HAKI kwa gharama yoyote. Sasa leo inakuwaje CDM wanashindwa kuwaENZI marehemu hao kwa kuendelea kusimamia HAKI kwa gharama yeyote hata kwa kupoteza jimno la LEMA ili HAKI dhidi ya LEMA yaani HAKIA ya kugombea arejeshewe?

TANO; (Hapa wanasheria watanisaidia) kisheria kuana kitu kinaitwa (RUFAA) APPEAL na JUDICIAL REVIEW, Kwanini CDM wasitumie hiki kipengele cha pili yaani JUDICIAL REVIEW kuiomba mahakama KUU au ya RUFAA kuifanyia REVIEW mwenendo mzima wa kesi ili kuona kama Hukumu ya kumzuia LEMA kugombea ndani ya miaka mitano hipo sahihi au la< kama haipo sahihi imtake Jaji kurekebisha kipengele hicho katika HUKUMU yake?

MWISHO; Hoja kuwa wananchi wa ARUSHA watakosa muwakilishi BUNGENI kwangu siioni kuwa ya msingi maana ni CDM haohao ambao wanawakosesha haki ya uwakilishi ktk baraza la madiwani wananchi wa ARUSHA wa KATA TANO baada ya kuwavua uanachama kwakuwa madiwani hao hawakuheshimu msimamo wa chama kuhusiana na HAKI. Je ni sahihi wananchi wa ARUSHA wawe na MBUNGE wa kuwawakilisha BUNGENI wakati MBUNGE wao LEMA hakutendewa HAKI kwa kuzuia kugombea? kwanini haki wapewe wanajimbo la ARUSHA Lema anyimwe? Hivi ni sahihi kumnyima mtu haki kwa kigezo kuwa wengi watakosa uwakilishi Bungeni? Mbino kwa miaka 50 wamepata UWAKILISHI lakini hadi leo wanalalamika kuwa Wawakilishi hao hawakuwasaidia na kuwafanyia kazi waliyowatuma? Hivi si kuna majimbo yana WABUNGE lakini uwajibikaji huo wa wabunge hao kwa wananchi ni sawa na JIMBO kuto kuwa na MBUNGE?

Wellsaid mkuu jinsi hiyo issue ilivyokaa ni kweli jaji alijichanganya wakati wa majumuisho kosa alilopatikana nalo lema ni illegal campaign na siyo illiegal practice.
Mytake:Wakili wa Lema inabidi awasiliane na jaji iliaclarify kuwa huo mkanganyiko wa vifungu alikosea au lah! Lengo la magamba ilikuwa ni lema akate rufaa ambayo ingemuweza kuendelea kuwa mbunge kitu ambacho kingepeleke delidali na hukumu ingetoka mwakani na kama bado mahaka ya rufaa ingemtia lema hatiani jimbo la arusha lingebaki wazi mpaka 2015 coz sheria ya uchaguzi inasema kama jimbo litaachwa wazi miaka miwili kabla ya uchaguzi mkuu hakutakuwa na ujazwaji wa hiyo nafasi.
Wanasheria mtanirekebisha kama nimekosea.
 
mtoa maada ana mantiki, tusimame katika kutetea hati za jamii na raia mmoja mmoja(lema) anastahili kukata rufaa kwa ajili ya kurekebisha hayo makosa ya kisheria ili haki ya mtu isipotee.
 
Mie nashauri chadema wakate rufaa! Haki tunayoidai kila siku lazima tuendelee kuidai! Mambo ya kusema jaji alijichanganya sio kweli. Hivi mnataka kuniambia kuwa huyo jaji alikaa mezani mwenyewe na kutoa hukumu? Hamuoni kuwa hiki ni kikundi cha watu wasomi wahuni wanaotumiwa na mafisadi? Ninapata hasira sana ninapoona mtu anasema jaji alijichanganya katika hukumu!!!!! Naamini mapambano ya kudai haki ya vyama vya upinzani ni zaidi ya vita yoyote iliyowahi kupiganwa hapa duniani: let fight we will win, if not us our children will find us on the way fighting.
 
Back
Top Bottom