mzee wa miba
JF-Expert Member
- Dec 20, 2011
- 759
- 125
Hivi kweli naomba wana JF muijadili hali hii,hivi inakuwaje tuwe na watu wanaoitwa Ma DC,Ma RC wakati hakuna output yoyote wanayotoa katika maendeleo yetu watz? nilidhani wao ndo watakuwa na mashamba ya mfano huko vjijini ili wananchi wajifunze,pia nilidhani kuwa wao ndo watakuwa na mifugo ya mfano,mbona hayo maendeleo wanayodaiwa kuhamasisha siyaoni huku vijijini? Kuna watu pia huku wanaitwa maafisa tarafa,hawa wote wanapokea mishahara na marupurupu ambayo ni jasho lawalipa kodi,napendekeza baada ya CDM 2012 kuchukua nchi vyeo hivi vifutwe.