Rapture Man
JF-Expert Member
- Dec 29, 2010
- 439
- 145
Wana JF,
Nina rafiki zangu kadhaa wa kiislamu. Tunapendana na kuheshimiana licha ya tofauti ya ki-imani. Muislamu mmoja alikuwa 'group study' moja na mimi. Rafiki yangu tangu Form I hadi Form IV na room mate wangu University. Huyu ndugu alikuwa mtaratibu na mpole sana. Enzi hizo pale UDSM mlimani kulikuwa na muungano wa wanafunzi wa kiislamu ulioitwa MSAUD. Na itikadi za MSAUD na za huyu rafiki yangu zilikuwa hazipishani sana (at least theoretically) na misimamo ya waislamu wa 'itikadi' kali. Kwa kuwa tulikuwa marafiki tulioshibana nilimuuliza kuhusu usahihi wa misimamo yake ya kidini, ya ki-MSAUD, ya kiislamu (itikadi kali). Rafiki yangu, kwa utaratibu kabisa, kwa ukweli wa moyoni, akaniambia chanzo cha msimamo wake ni KORAN yenyewe. Kwamba yeye anashikilia misimamo yake kwa sababu KORAN inamtaka afanye hivyo. Kama isingekuwa KORAN asingekuwa na misimamo hiyo.
Sasa mimi sijasoma KORAN hata kidogo. Natamani kupatikane wasomi wa kiislamu wenye nia ya kutuelimisha kuhusu KORAN, kama misimamo ya itikadi kali ni ya ki_KORAN au ni uzushi. Na pia wapatikane wasomi wa ki-kristo wenye nia ya dhati ya kuelimisha wasioufahamu ukristo. Haya makundi mawili yakutanishwe ktk mdahalo wa ana kwa ana, wenye nia ya kujenga, lakini wenye nia ya kufahamishana ukweli toka mioyoni mwetu. Tufanye hivyo huku tukitarajia kwamba hoja zikipishana sana TUTAKUBALIANA KUTOKUKUBALIANA.
Napendekeza mdahalo huu uandaliwe kinamna fulani na wazito wa JF. Kwa baadae utaweza kurushwa hewani, sote tuone na tusikie. JF itaweza ku-raise fund kwa mtindo huu toka kwa wadhamini wa kipindi maana ni wazi kipindi hiki kitakuwa hot-cake.
Bado naamini kuna waislamu wengi hawana misimamo ya kiitikadi kali. Lakini tunataka wao kwa wao pia wasimame na watoe maoni kuhusu KORAN yao kama inafagilia itikadi kali au la. Na kama ni ndiyo basi tutafute namna ya kudumu ya kuishi huku waislamu wakitimiza KORAN na wakristo wakitimiza BIBLIA.
Rafiki yangu huyu alinieleza kuwa KORAN inadai nchi itawaliwe na sharia.
Sasa wasomi wengine wa kiislamu mnasemaje? Tukutane tutafakari mambo haya kwa uwazi na ukweli wa moyo. Inawezekana KORAN inadai hivyo na tunaposhindana na 'itikadi kali' tunapoteza muda. Tukiamua tunaweza kuleta kitu tofauti cha kuigwa duniani.
Humu JF naona hoja kadhaa kuhusu suala hili nyeti zinakuja kimzahamzaha, utani, na matukano fulani. Tukiwa ana kwa ana tutakuwa serious zaidi. Mnaonaje?
PENYE WENGI HAPAHARIBIKI NENO.
NAWAKILISHA.
Nina rafiki zangu kadhaa wa kiislamu. Tunapendana na kuheshimiana licha ya tofauti ya ki-imani. Muislamu mmoja alikuwa 'group study' moja na mimi. Rafiki yangu tangu Form I hadi Form IV na room mate wangu University. Huyu ndugu alikuwa mtaratibu na mpole sana. Enzi hizo pale UDSM mlimani kulikuwa na muungano wa wanafunzi wa kiislamu ulioitwa MSAUD. Na itikadi za MSAUD na za huyu rafiki yangu zilikuwa hazipishani sana (at least theoretically) na misimamo ya waislamu wa 'itikadi' kali. Kwa kuwa tulikuwa marafiki tulioshibana nilimuuliza kuhusu usahihi wa misimamo yake ya kidini, ya ki-MSAUD, ya kiislamu (itikadi kali). Rafiki yangu, kwa utaratibu kabisa, kwa ukweli wa moyoni, akaniambia chanzo cha msimamo wake ni KORAN yenyewe. Kwamba yeye anashikilia misimamo yake kwa sababu KORAN inamtaka afanye hivyo. Kama isingekuwa KORAN asingekuwa na misimamo hiyo.
Sasa mimi sijasoma KORAN hata kidogo. Natamani kupatikane wasomi wa kiislamu wenye nia ya kutuelimisha kuhusu KORAN, kama misimamo ya itikadi kali ni ya ki_KORAN au ni uzushi. Na pia wapatikane wasomi wa ki-kristo wenye nia ya dhati ya kuelimisha wasioufahamu ukristo. Haya makundi mawili yakutanishwe ktk mdahalo wa ana kwa ana, wenye nia ya kujenga, lakini wenye nia ya kufahamishana ukweli toka mioyoni mwetu. Tufanye hivyo huku tukitarajia kwamba hoja zikipishana sana TUTAKUBALIANA KUTOKUKUBALIANA.
Napendekeza mdahalo huu uandaliwe kinamna fulani na wazito wa JF. Kwa baadae utaweza kurushwa hewani, sote tuone na tusikie. JF itaweza ku-raise fund kwa mtindo huu toka kwa wadhamini wa kipindi maana ni wazi kipindi hiki kitakuwa hot-cake.
Bado naamini kuna waislamu wengi hawana misimamo ya kiitikadi kali. Lakini tunataka wao kwa wao pia wasimame na watoe maoni kuhusu KORAN yao kama inafagilia itikadi kali au la. Na kama ni ndiyo basi tutafute namna ya kudumu ya kuishi huku waislamu wakitimiza KORAN na wakristo wakitimiza BIBLIA.
Rafiki yangu huyu alinieleza kuwa KORAN inadai nchi itawaliwe na sharia.
Sasa wasomi wengine wa kiislamu mnasemaje? Tukutane tutafakari mambo haya kwa uwazi na ukweli wa moyo. Inawezekana KORAN inadai hivyo na tunaposhindana na 'itikadi kali' tunapoteza muda. Tukiamua tunaweza kuleta kitu tofauti cha kuigwa duniani.
Humu JF naona hoja kadhaa kuhusu suala hili nyeti zinakuja kimzahamzaha, utani, na matukano fulani. Tukiwa ana kwa ana tutakuwa serious zaidi. Mnaonaje?
PENYE WENGI HAPAHARIBIKI NENO.
NAWAKILISHA.