Napendekeza cdm wawaamshe wafanyakazi kwa sera bora

Kwaroz

Member
Aug 30, 2009
55
10
KUNA MENGI SANA ambayo siwezi kuyakana ndani ya nafsi yangu yamefanywa kuwa ufanisi na CDM kwa stahili ambayo inawafanya CHAMA CHA MAGAMBA kuweweseka mpaka sasa kwa hilo nawapa pongezi maana mziki wanapiga CDM na WANAMAGAMBA wancheza bila kujijua na wakiulizwa mbona mnacheza mziki wa wenzenu wanabisha, hapo kazi hipo.

kwa sasa naangalia maisha ya mtanzania ambaye ni Nyundo kwa WANAMAGAMBA naona yanakasoro kubwa sana na naona wamesahaulika kwa kiasi kikubwa kiasi kwamba maslahi yao ya msingi hawapati na wala hawajui haki zao. napendekeza kwa CDM kuanza kutayarisha sera ambazo watazisema waziwazi bila kificho kwa kuwa hawa watanzania kwa sasa na wahaanga wa kila kitu, mishahara, kudhurumiwa haki zao, kudharauliwa, kujaliwa wakati wa uchaguzi mkuu tu na wala si kingine nje ya hapo. pia wafanyakazi wengi hawana muongozo thabiti katika kujua haki zao, sheria ya kazi ni vigumu kuipata kuliko katiba ya nchi na wafanyakazi wengi wanategemea viongozi wao waseme na wao wafuate. nadhani kama CDM watajipanga vizuri katika hili watapata wanachama wengi ambao wamekata tamaa ya kudai haki zao kutoka kwa waajili wao ambao ni serikali, wawekezaji, wafanyabiashara na wengine wengi ambao waasifa na waajili. kwa sasa kunasintofaham juu wa wafanyakazi hawana wa kuwatetea ndio maana serikali inawayumbisha kila kukicha na waajili binafsi wanafuata nyayo za serikali wakati sheria za kazi zipo wazi. mkianzisha mchakato wa kuibua madudu ju ya wafanyakazi ninahakika mengi mtayapata ya kujifunza. nikifanya mahesabu ya haraka haraka tuchukulie record ya ****** kwamba kuna wafanyakazi 350,000 ambao kwa namna moja au nyingine kuna watu wanaowategema huko vijijini na hapa mjini tuchukulie ni watu wanane ambao ni watoto wazazi na ndugu wengine kwa kadirio la chini na hapo utakuta unakaribia watu 350,000 * 8 = 3,000,000 na tufanye kwamba wale walio kwenye ajira ambazo hazina tafsiri rahisi ambao wanaitwa vibarua, wafanyakazi wasio na mikataba, wafanyakazi wasio rasmi tuseme ni kama 400,000/= na hao kwa hesabu tuseme kunawatu wanahitaji msaada toka kwao kama wanne hivi ambao wanaweza kuwa watoto, wazazi na wengine, kwa hesabu ya haraka utapata watu 1,600,000. Jumla yao yote kwa kadirio la chini ni watu 4,600,000 ambao wanakaribia idadi ya wanachama wa WANAMAGAMBA.

point yangu ni kwamba kama CDM watafanya kazi nzuri kwa hawa wafanyakazi ambao hawaoni umuhimu wa serikali kuwepo au kutokuwepo na kuwapa uelewa wa kutosha kwa sera nzuri nina hakika CDM itapata kura nyingi sana kuliko inavyoona. ukiangalia mfumo wa mashirika ya pensheni utaona pesa za wafanyakazi zinafanyiwa kazi bila kulipwa faida na mengine mamboi mengi pasua kichwa.

CDM JIPANGE SAWA SAWA WAFANYAKAZI WAHITAJI SERA NZURI NA BORA
 
Back
Top Bottom