Napenda WanaJF Tusaidie kupata Wimbo Wa Kizalendo

RedDevil

JF-Expert Member
Apr 30, 2009
2,368
1,518
Ndugu wanaJF, nimekuwa nikifikiria sana ni namna gani sisi wapenda mabadiliko katika nchi yetu tunawezaje kupata wimbo wenye kusisimua kila mtu bila kujali itikadi yake, ili wakati huu wa kampeni utumike kama wimbo wa ukombozi wa nchi yetu toka kwa wakoloni mamboleo.
Najua jamii yetu wengi hawapati ujumbe sawa sawa kupitia mtandao wetu kwa vile kuna ugumu sana kupata habari kupitia mitandao tokana na watu wengi kutojua matumizi ya mitandao. Lakini tukiweza kuhamisha mawazo yetu kwenda katika wimbo naimani kuwa wengi watapata habari zenye kuleta mabadiliko kwa watu walio maeneo mbali mbali nchini. Hivyo ningependa waJF tuwe wakwanza/waanzilishi wa huu wimbo. Kama inawezekana wimbo uweze kutumika hata kwenye hizi kampeni.

Naomba mwenye kusahihisha, maoni, na kutoa uelekeo kwa faida ya nchi yetu najua hapa jamvini kuna waimbaji wengi na wabunifu.

Naomba kutoa hoja. :A S-coffee:
 
Naunga mkono hoja hii muhimu, unahitajika wimbo wa kusisimua zaidi.

Wimbo wa sasa unafanana mno na ule wa Afrika Kusini (Nkosi Sikeleli ....). Actually sauti ya wimbo huo ilitungwa na mtu wa Afrika Kusini. Sasa sioni ni kwa nini tusitunge wimbo wetu wenyewe tukawa kila tunapoimba wimbo wetu tunaiga wa wa-sauzi?

Hekima, Umoja na Amani ... tunahitaji kuongeza umuhimu wa Kazi, Upendo kwa Nchi yetu (Uzalendo) .....

Tena naunga hoja.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom