RedDevil
JF-Expert Member
- Apr 30, 2009
- 2,368
- 1,518
Ndugu wanaJF, nimekuwa nikifikiria sana ni namna gani sisi wapenda mabadiliko katika nchi yetu tunawezaje kupata wimbo wenye kusisimua kila mtu bila kujali itikadi yake, ili wakati huu wa kampeni utumike kama wimbo wa ukombozi wa nchi yetu toka kwa wakoloni mamboleo.
Najua jamii yetu wengi hawapati ujumbe sawa sawa kupitia mtandao wetu kwa vile kuna ugumu sana kupata habari kupitia mitandao tokana na watu wengi kutojua matumizi ya mitandao. Lakini tukiweza kuhamisha mawazo yetu kwenda katika wimbo naimani kuwa wengi watapata habari zenye kuleta mabadiliko kwa watu walio maeneo mbali mbali nchini. Hivyo ningependa waJF tuwe wakwanza/waanzilishi wa huu wimbo. Kama inawezekana wimbo uweze kutumika hata kwenye hizi kampeni.
Naomba mwenye kusahihisha, maoni, na kutoa uelekeo kwa faida ya nchi yetu najua hapa jamvini kuna waimbaji wengi na wabunifu.
Naomba kutoa hoja. :A S-coffee:
Najua jamii yetu wengi hawapati ujumbe sawa sawa kupitia mtandao wetu kwa vile kuna ugumu sana kupata habari kupitia mitandao tokana na watu wengi kutojua matumizi ya mitandao. Lakini tukiweza kuhamisha mawazo yetu kwenda katika wimbo naimani kuwa wengi watapata habari zenye kuleta mabadiliko kwa watu walio maeneo mbali mbali nchini. Hivyo ningependa waJF tuwe wakwanza/waanzilishi wa huu wimbo. Kama inawezekana wimbo uweze kutumika hata kwenye hizi kampeni.
Naomba mwenye kusahihisha, maoni, na kutoa uelekeo kwa faida ya nchi yetu najua hapa jamvini kuna waimbaji wengi na wabunifu.
Naomba kutoa hoja. :A S-coffee: