Napenda siku moja iwe hivi...

Ningependa kama ambavyo mtu anakuwa makini juu ya simu yake, akisahau ndani tu haraka anakumbuka na kurudia, iwe hivyo hivyo juu ya BIBLIA zetu. Siku zikipatikana BIBLIA ndogo za kuweka mfukoni unatembea nayo kama tutembeavyo na simu na iwe na agano jipya na agano la kale. Mtu ukiisahau ndani tu, haraka sana unairudia, siku hiyo itakuwa siku nzuri sana.

Bravo!
 
alafu napenda siku moja mods wote watuachie madaraka ya kuwapiga ban watu flan flan hivi!!! yaani hatuangalii wewe ni mod wala nani
 
1.Napenda siku moja hapa dar matafriki wasiwe kazini jiji zima wala taa zisifanye kazi.Yaani ni madereva tu na magari yao.(lengo nataka kusikia matusi na misele ya madereva wetu)
2.Napenda siku moja benk zote mjini ziruhusu watu 'kujisevia' wenyewe,yaani kama vile kwenye harusi unavyojipakulia msosi.So mtu unaingia tu mle kwa keshia unawekea au unatoa pesa mwenyewee!! Au unaenda pale bodi ya mikopo unajikopesha milion kadhaa hv. Nk
3....!
4....!
Jazia na zako unazopenda siku moja zitokee

Ningependa kama mitandao ya kijamii itumike kuchart mambo ya KIMUNGU NA KIMAENDELEO.
Ningependa vijana wengi watanzania wa jishuhulishe na waache kutegemea serekali juu ya upatikanikaji wa ajira
 
napenda siku moja iwe hivi:
kila ukikanyaga ardhi yenye mmiliki...mguu ukwamie hapo hapo...mngekomaje?
 
Napenda siku moja niwe na uwezo wa kusikia mtu anachowaza kichwani!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom